Mate kujaa mdomoni, tena yenye harufu mbaya wakati wa kuamka asubuhi husababishwa na nini?


Habari,

Utoaji wa mate mengi pamoja na kuwa yenye harufu mbaya inahusisha na:

1: Gastroessophageal reflux (GERD).
Kuwa na hali ya majimaji toka tumboni kurejea kinywani.

2: Nasal congestion/ kutokupitisha hewa vizuri puani kutokana na njia kuwa ndogo.
Mfano: Rhinosinusitis, nasal polyps

3: Matatizo yanayoweza kuhusisha mishipa ya fahamu.

3: Sleep apnea
Kuwa na tatizo la upumuaji na ufikishaji oksijeni wakati wa kulala. Mfano: Unene vs shingo fupi nk.

4: Matumizi ya dawa
Kuna baadhi ya dawa huongeza hali hii.

NB: Ni vyema kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kupata historia yako vizuri, kufanyiwa ukaguzi na vipimo itakapohitajika. Ili uweze kupata suluhisho.
 
Nlikua na tatizo hilo nikaja kugundua nlikua na minyoo,pia usagaj wa chakula ukawa shida kwasababu nlikua natumia pombe,nikatumia dawa za minyoo,nikaanza kula vizur ikiwemo matunda na mboga za majani,kuswaki vizuri haswa ulimi mana weng tunasugua meno badala ya ulimi,ulim ndo unatoa harufu
 
Okay, dawa Gani za minyoo uliitumia, na je Hilo tatizo lako lilipona kabsa
 
Okay, nashukuru Kwa maelezo yko mkuu, ntayafanyia kaz.🙏
 
unda urafiki na mswaki angalau mara mbili au tatu kwa siku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…