Na mie naomba kuchangia hii mada ya hesabati ju ya ufunguo wa siri za ulimwengu,
Hii ipo hivi, kiuhalisia hisabati ndio kufuli ya siri za ulimwengu na sio hisabati pekee masomo yote tunayofundishwa skuli kisaikologia yana kuwa ni kufuli za kuifunga akili ya mwanadamu isotoke nje ya ufahamu unaojengwa na mafunzo hayo,
Hesabati sio zao la uhalisi au nature, hisabati ni man-made structure kama ilivyo mifumo ya masaa tarehe,siku,miezi na miaka, hii yote ni mifumo ya kutunga na sio natural, na sababu za kutunga mifumo yote hii ni kutia kufuli akili ya mwanadamu isitoke nje ya box,akili ya mwanadamu isiwe free kuwaza mambo yake yenyewe na iwe imefungika kwenye hii mifumo ya hesabati na tarehe,n.k
Tuutazame mfano huu wa kufuli ya hesabati¡.
inalazimisha namba zianzie 0 mpaka 9 hii maana yake akili haiwezi tena kutoka nje ya namba 9 na akili haiwezi tena kuvumbua namba mpya zaidi ya namba 9, na haiwezi kuja na maarifa zaidi yatokayo nje ya 0 to 9, yaani kwenye akili zetu mwangaza upo kuanzia 0 mpaka 9 tu baada ya hapo ni kiza kitupu na blockage
Twende kwenye Siri za ulimwengu hizo zinazotarajiwa kufumguliwa kwa hesabati [emoji75],
Siri za ulimwengu haziwezi kufunguliwa na elimu au mfumo wowote tunaoufahamu sisi binadamu, yaani kiuhalisia hizi elimu na mifumo inayotujenga sisi binadamu ipo kwa ajili ya kutuweka mbali na ufahamu wa mifumo halisi ya ulimwengu, na mifumo yote tuliyofunzwa ya ulimwengu sio ya ukweli yote ni uzushi. Na hii mifumo ya uzushi imejengwa kwa kukubaliana na hesabati na kwenye akili zetu chochote kinachokubaliana na hesabati ni kitu halisi.
Kuanzia dunia yenyewe ilivyo, upatikanaji wa seasons, kinachosababisha usiku na mchana, uhalisi wa jua,mwezi,nyota na sayari, upepo ni kitu gani na unasababishwa na nini, mvua inapatikanaje na mengi mengineyo haya yote yanatolewa maelezo yake katika elimu za kutunga za kutunga na sio katika uhalisi wake.
Sisi binadamu sote dunia nzima tunaishi maisha yote hapa duniani hatuwezi kujua kabisa dunia ni kitu gani kiuhalisia, tunaelimishwa kwa kuoneshwa picha za kuchora na video za animations tu, na hakuna hata picha moja ya dunia ambayo ni ya kweli,binadamu hatutakiwi kuijua dunia ni nini na pia hatutakiwi kujua siri halisi za ulimwengu, mambo tunayofunzwa ni mambo ya kutupumbaza tu na kuupoteza wakati wetu wa maisha bure, na kutufanya tusijielewe hata sisi wenyewe ni nani hasa
Nadhani ntarudi tena baadae kuendelea