Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika leo na idadi ndogo ya wapiga kura kujitokeza, vyama vya upinzani kujitoa iwavyo vyovyote iwe mmefurahia, mmeumia, mmechukia, Rais Magufuli chondechonde wewe na chama chako tafakarini na mjue ujumbe ambao Watanzania wameufikisha kwako na serikali yako.
Nchi hii ni yetu sote au labda ikiwapendeza ni mali ya CCM, lakini wanaishi watanzania wote. Ya kujifunza ni haya; umejenga Standard Gauge, Stiegers Gorge, umenunua ndege na kwa mujibu wako umefanya ambayo hata marais waliopita hawajayafanya, iweje leo Watanzania na wanaccm wasijitokeze kwa mamilioni kukuunga mkono?