Matukio yanayoonesha uongo kwenye vitabu vya dini

Matukio yanayoonesha uongo kwenye vitabu vya dini

Matukio haya yanaonyesha kwamba dini imejaa uongo.

Tuanze na Biblia.
1. Biblia inasema mungu ni alpha na Omega, mwanzo na mwisho, ni yeye aliepo na ataendelea kuwepo. Kwa maana kwamba mungu ndio chanzo cha vitu vyote, hakuna kitu kilianza bila yeye. Mungu ni mjuzi wa kila kitu.

Tukiamini hivyo ni sawa, lakini tukienda mbele zaidi kutafakari, kama mungu anajua vyote, je alijua kama shetani atakuja kumuasi? Kama alijua ni kwa nini bado alimuumba?

2. Kama mungu aliamua tu kumuumba shetani pamoja na kujua kua atakuja kuasi, alikua na maana gani? Biblia inasema yeye ni mkamilifu, hakuna kitu kidhaifu/kibovu kinatoka kwake, sasa unajiuliza shetani alietoka kwake ni mbovu ama mzima ama mkamilifu?

Hapo jibu ni moja tu, mungu hakujua kama shetani atakuja kumuasi hivyo mungu hajui kila kitu.

3. Baada ya shetani kuasi na malaika zake, kwa maelezo ya biblia shetani alitupwa Duniani. Kwa maana kwamba Dunia haikua na kiumbe ila shetani alitupwa huku kukiwa ni empty.

Baadae mungu akamuumba binadamu na kumuweka Duniani. Kwa maana kwamba Adam amekuja Duniani tayari shetani yupo muda mrefu anakula maisha. So Adam kamkuta shetani Duniani.

4. Baada ya Adam kuletwa Duniani, hakuwahi kuambiwa kwamba kuna kiumbe mwingine anaeishi Duniani tofauti na yeye, so hakupewa tahadhari yoyote. Kwa maana nyingine aliachwa kua vulnerable kwa shetani kumshambulia. Swali, kwa nini mungu hakumuonya Adam kuhusu uwepo wa shetani Duniani? Kwa nini alikaa kimia, lengo lake ilikua nini?. Mbaya zaidi mungu hakumuonya shetani asimrubuni adam, so akaacha loop hole ya shetani kujifanyia anayoyataka, baada ya shetani kufanikiwa, lawama ni kwa Adam.

Tu-assume alipewa maelekezo kidogo, lakini alipewa yeye, hakuna maonyo aliyopewa Eva mke wa Adam ambae shetani alimtumia kama kichochoro, je hawa makosa yao ni nini?

Jibu: Mungu aliwaingiza kwenye mtego maksudi, kuanguka kwa adam ilikua ni maksudi ya mungu kutafta justification ya kumlaumu Adam.

5. Kati ya binadamu na malaika mungu anampenda nani zaidi. Biblia inasema shetani alikua malaika mkuu, alipoasi alipata baadhi ya malaika waliomuunga mkono. Maelezo mazuri kabisa.

Biblia inaenda mbali na kusema baada ya shetani na malaika zake kuasi mungu aliwatupa Duniani watatange take. Tunakubali sawa kabisa.

Swali, kati ya binadamu na malaika ni nani anamjua vizuri shetani? Jibu ni malaika kwa sababu wameumbwa pamoja, wameishi pamoja hivyo wanajuana vizuri.

Swali lingine, kwa akili ya kawaida, ni nani alipaswa kuletwa Duniani kupambana na shetani? Jibu, alipaswa iwe ni malaika kwa sababu wanamjua vizuri zaidi shetani kuliko binadamu. Kwa maana kwamba ingekua rahisi sana kwao kumkataa shetani mapema na akakosa wafuasi kwa sababu wanamjua.

Masikitiko ni kwamba, mungu hakutaka kuwaleta viumbe wake anaowapenda Duniani akaamua kuumba viumbe wengine ambao hawajui lolote na kuja kuwapambanisha na shetani ambae ana superiority knowledge kuliko wao.

Ni sawa na wewe una rungu unaenda kupigana na mtu ana mizinga, drones, fighter jets, na kila kitu halafu utegemee utashinda. Hiki ndio mungu alichoamua kuwafanyia binadamu.

B. Nitakuja kuelezea upande wa quran(huku ndio madudu yalikojaa). Mkitaka na vifungu nitaweka.
Torati, Biblia na Qur'an vyote si vitabu vya Mungu....vimetungwa na binadamu tu na ndiyo maana kila mmoja anavutia kwake. Kuamini hivi vitabu ni kujitafutia matatizo ya kiakili tu.
 
Unfortunately wengi tunaishi kwa masimulizi ya kuambiwa Biblia na Qur'an ni TOFAUTI sana ikiwa akili yako imetulia: So sad....

Naomba nikupe mifano miepesi:

1. Nabii wa Allah Ibrahim kwenye bibilia anatuhumia kwa Uzinzi LAKINI Nabii huyu kwenye Qur'an amesimuliwa akiwa na Uchamungu wa Hali ya juu mpaka anafikia kuitwa Rafiki wa Mola Mlezi

2. Ukisoma Bibilia utamkuta Nabii wa Allah Nuhu akiwa ni shujaa aliyewaokoa watu na Gharika lakini baadaye akawa Mlevi wa kutupwa [Alcoholic] TOFAUTI kabisa na kwenye Qur'an

3. Nabii wa Allah Luti anaonekana akiwaokoa baadhi ya wafuasi wake na gharika ya sodoma na gomora lakini bibilia hiyohiyo inatueleza baadaye akazini na binti zake LAKINI Nabii huyu kwenye Qur'an qnasimuliwa akiwa ni mchamungu na wakupigiwa mfano na ummah wake

5. Nabii wa Allah Daud anasimuliwa kama kamanda aliyeshinda vita [kumshinda goliati] lakini bibilia hiyo hiyo inatuambia baadaye akazini na mke wa kamanda wake na kumua mwenye mke.... Nabii huyu kwenye Qur'an anasimuliwa ni mwema na mwenye kupigiwa mfano na ummah wake..

5. Nabii wa Allah Iysah AMA YESU anavyosimuliwa kwenye bibilia YEYE pamoja na mama yake na WANAVYOSIMULIWA KWENYE QUR'AN ni TOFAUTI..

6. Lakini matukio kama la YUSUF na ndugu zake linavyosimuliwa kwenye bibilia ni kama kuungaunga LAKINI lilivyosimuliwa kwenye QUR'AN ni very clear [rejea SURATUL YUSUF]

Kwa kifupi wengi wa wakiristo hawasomi vitabu vyao hasa Bibilia wanaishi kwa mistari miwili mitatu ya kuambiwa TOFAUTI na imani ya Kiislam iliyojenga kwenye MSINGI wa elimu...

Nimesoma sana bibilia lakini haijawahi kunibariki kama nilivyopata nafasi ya kusoma Qur'an
Mbona haujaelezea habari za mabikra 72 na mito ya pombe
 
Back
Top Bottom