Matumizi ya chumvi kuondoa mikosi

Matumizi ya chumvi kuondoa mikosi

Huyo ananiacha hoi amewaambia mkojo unamrudisha aliekuacha au unamsahau wadada wanakunywaa mkojo kama hawana akir nzur sasa nimeona somo la chumvi na mshumaa [emoji23][emoji23]jaman jaman na bado wanaingia kwa kiingilio mwez mmoja elfu 5000/=dunia hii jaman
hahah watu wana mbinu hatari sana za kuongeza kipato, watakunywa sana mkojo shubaaamit
 
inatumikaje? Maana Kweli wanatoaga ushuhuda wa kufa mtu. Matumizi yake Tafadhali. Kuliko kwenda kutoa buku 5[emoji16][emoji16]
 
Dawa zipo na wala siyo kila dawa ni uchawi ama ushirikina. Kama ni hivyo basi nabii Elisha alipoyatibu Yale maji kwa chumvi alifanya ushirikina?! Hapana.

Mfano mwingine ni ule wa Kuponywa kwa binti Sara mchumba wa Tobia. (Biblia takatifu kitabu cha TOBITI 6: 17).

Tunaona jinsi malaika Rafael anavyomwongoza Tobia juu ya namna ya kumwondoa jini mbaya aliyemsumbua Sara kwa miaka kadhaa. Kwa kuchoma ubani na kisha kuweka vipande vya ini vya samaki kisha yule jini akaskia harufu ile akakimbia na wala hakurudi tena.

Tunajifunza kwamba; kwanza siyo kwamba Mungu au yule malaika (Rafael) alishindwa kumfukuzia mbali jini Bali kusudio ni kumwambia mwanadamu kuwa solutions za mambo mengi anazo hapahapa katika nchi.

Pili, Jinsi dunia ilivyoumbwa iko very balanced. Ndiyo maana Baada ya uumbaji biblia inasema :" Basi mbingu na nchi zikakamilika". (Mwanzo 2:1). Huko kukamilika maana yake ni kuwa ndani ya nchi kuna kila kitu kwa ajiri maisha yote ya Mwanadamu. E.g kama kuna kutiwa nuksi basi kuna njia za kinyume chake. Namna ya kuondoa nuksi.

Sasa kama kumtia MTU nuksi ni dhambi na kuondoa nuksi ni dhambi, ni lipi lenye kumpendeza Bwana Mungu?!

Tunafahamu Mungu anao uwezo mkuu. Angeweza kuyatibu Yale maji kwa kusema tu bila kuweka chumvi kwa mkono wa Elisha au angeweza kumponya binti Sara (Tobiti 6:17) vile vile pasipo hivyo vitu vya kidunia. Sasa kwa nini avitumie? Yule jini hakutaka Sara aolewe ndiyo maana akawa anaua kila mwanaume aliyemsogelea Sara. Kwa maneno mengine Sara alikuwa na nuksi!

Ndiyo kusema kwamba hayo yote Mungu anayafanya ili kutwambia kuwa solutions za mambo mengi tunayo hapahapa katika nchi.

Shida ni ufahamu wetu tu mdogo. Ndiyo maana akaongeza kusema kuwa :" WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA". Unadhani ni maarifa yapi?!

Tatizo ni kwamba tulio wengi kama hatujui kitu Fulani basi hicho siyo cha kweli. Na tunadhani kwamba maarifa tuliyonayo ndiyo ukomo wa maarifa kwa watu wote.

Find knowledge usidhani umeimaliza dunia.

- JODEO-
 
Kama ilivyo unachanganya na maji na mafuta ya mzeituni unaogea au kumwaga kuzunguka nyumba huku ukinuizia
Brother asante. Ila natamani kujua zaidi,, inaishia hapo tu kwenye kuoga na kunuiza au kuna mambo mengine zaidi? Na je ufanisi wake ukoje? Yaani inaweza kukupa matokeo baada ya muda gani, na je ukishafanya Mara moja inakupasa kurudia tena?

Asante
 
Mshana Jr ongeza nyama kidogo juu ya hili.

Bro mshana nikua nasubiri mchango wako ..sasa shusha madini step by step jinsi ya kufanya..
Kuna baadhi ya shida katika maisha utatuzi wake sio kwa waganga wa kienyeji ambako mara nyingi hukuacha na maagano
Kwahiyo Kuna hii tiba ya kutakasa kwa chumvi na mafuta ya mzeituni ambapo unaweza kutumia kwa kuchoma kuogea au kumwaga kuzunguka nyumba huku ukinuizia kufukuza mambo yote machafu na kukaribisha baraka na mafanikio
unaweza kufanya hivi mara moja kwa siku mara tatu au mara mbili kwa wiki nzima
 
Brother asante. Ila natamani kujua zaidi,, inaishia hapo tu kwenye kuoga na kunuiza au kuna mambo mengine zaidi? Na je ufanisi wake ukoje? Yaani inaweza kukupa matokeo baada ya muda gani, na je ukishafanya Mara moja inakupasa kurudia tena?

Asante
Ina matokeo mazuri kutokana na imani yako kwenye manuizi
Wengi wamefanikisha na kukwamuka hasa kwenye kuuza nyumba viwanja nk....hata katika mahusiano pia na ndoa zinazolegalega
Mafuta ya mzeituni hung'arisha
Chumvi huleta ladha....
Kwahiyo manuizi yako lazima yalenge huko
 
Back
Top Bottom