Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
aahhaaahGaidi Mbowe atakuwa alihusika kwnye haya mauaji, achunguzwe vizuri... nipo tayari kutoa ushahidi... hahahaah!
Kidogo kuna ukweli lkn kuna maeneo umekoseaMuuaji alikuwa ni shemeji yake,(mdogo wa mkewe) ambaye huyo mkewe alikuwa anatoka ktk ukoo wa waarabu (sultani) ambao waliponduliwa na Karume, umeelewa!? Sasaa...
Kwa mapenzi kwa mkewe au labda ilikuwa ni njia ya kuwapooza mkewe na shemejie,
Baada tu ya mapinduzi alimpandisha shemeji yake vyeo vya kijeshi harakaharaka, ndo maana hata wakati anaenda kumuua karume aliwapita walinzi wote wa raisi huku akiwa na smg ndani ya koti!
Alienda mpaka hazizidi m.5 kabla hajafika alipokaa karume na wenzake, akafyatua risasi kadhaa!
Na yeye aliuawa kwa risasi na walinzi wa raisi pale pale.
Sent using Jamii Forums mobile app
Karume, Babu , Hanga na wengineo ndo waliopanga Mapinduzi. Okello alikua ni askari wa kukodi tu au unaweza kumuita mamluki. Hakuhusika kwenye kupanga hayo mapinduzi na wala hakujua chochote. Kinachofanya watu wamuone ni mhusika ni kule kujitangaza kwenye radio na kuranda randa mitaani kutisha watu baada ya Mapinduzi. Okello alirudishwa kwao Uganda baada ya kuonekana anataka kuwa juu ya wenye mapinduzi yao.Naomba nihame kidogo
Hiv ni kwann nchi alipewa karume na sio okello na baada ya mapinduzi okello alienda wap na pia je kama kiongozi wa mapinduz SMZ ilimpa reward gan
Na uraia wake ulikua sababu ya yy kukosa nafasi SMZ
labda tuanzie huku kabla ya kufikia tukio hlo la uhaini
Sent using Jamii Forums mobile app
Karume aliongoza chama cha Afro-Shirazi kupinga muungano wa utawala wa Kiarabu ulioonekana kuwa na lengo la kudumisha utawala wa kisiasa na kiuchumi wa jamii ya Kiarabu.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Karume alichukua hatua yake ya pili muhimu ya kisiasa alipokubali kuunda Muungano na Rais wa Tanganyika Julius Nyerere Aprili. Muungano huo umesababisha nchi mpya iitwayo Tanzania.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Karume hakujali mgawanyo wa mamlaka na madaraka kati ya yale ya Muungano na yale ya Zanzibar. Ukiacha mambo ya Nje, Zanzibar iliendelea kudhibiti kivyake madaraka na mambo yote juu ya Uhamiaji, Biashara ya Nje na Mikopo, Utumishi wa Umma, Bandari, Posta na Simu, Jeshi na Usalama wa Taifa ambayo vinginevyo yalipashwa kusimamiwa na Serikali ya Muungano. Na kwa chukizo kwa Nyerere, alitangaza kuwa asingeruhusu uchaguzi kufanyika Visiwani kwa miaka 50; akatangaza ukuu (supremacy) wa Chama cha Afro Shirazi (ASP) kuwa juu ya taasisi zote, ikiwamo Katiba ya Jamhuri ya Muungano na taasisi zake. Kana kwamba alikuwa akiimarisha Taifa huru la Zanzibar nje ya Muungano, Amri yake (Decree) juu ya ukuu wa ASP ilianzisha Idara za Jeshi, Usalama wa Taifa (la Zanzibar), Polisi, Vijana, kina mama wa ASP ili kwamba mambo hayo yashughulikiwe kiserikali chini ya idara husika nje ya Muungano.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Kufika mwaka 1971, Vyeo kama “Rais wa Zanzibar” (chenye kutambuliwa na Katiba ya Muungano), Mawaziri na Manaibu Mawaziri, vilibadilishwa kuitwa “Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi” (badala ya Rais), Mawaziri na Manaibu Mawaziri wakaitwa Wenyeviti na Manaibu Wenyeviti wa Idara; yote haya ilikuwa ni chenga kimamlaka kufanya Katiba ya Muungano isiwe na pa kushika kiutawala Visiwani.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Na vivyo hivyo, Jamhuri ya Muungano ilitawaliwa na kuongozwa kwa Katiba ya Mpito (Interim Constitution) ambayo ilimpa madaraka Rais wa Jamhuri ya Muungano, kuifanyia marekebisho kadri alivyoona inafaa katika kipindi cha mpito cha mwaka mmoja kuelekea Katiba ya kudumu, isipokuwa kwa mambo kumi na moja ya Muungano (kutopunguza au kuongeza) yenye kulindwa na Mkataba wa Muungano (Articles of Union), uliotiwa sahihi na waasisi wake, Aprili 22, 1964.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Baada ya Tanganyika na Zanzibar kuungana mwaka 1964 katika kipindi hiki cha mpito kwa nchi hizi kuanzisha Benki Kuu na sarafu yake, mgogoro mkubwa ulizuka kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar juu ya mambo matatu: la kwanza, ni kama Zanzibar iendelee kuhudhuria au la, vikao vya EACB kama nchi; pili, kama Zanzibar bado ilistahili gawiwo la faida kutokana na uwekezaji wake baada ya EACB kuvunjwa.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Tangu kufikiwa kwa Muungano, Aprili 26, 1964; na kufuatia kuvunjika kwa EACB, Zanzibar ilikuwa na shauku hai ya kuanzisha Benki Kuu (BoZ) yake. Wizara ya Fedha Zanzibar, chini ya Waziri makini Abdulaziz Twala, ilianza mchakato huo kwa kupeleka vijana nchini Ujerumani Mashariki kwa mafunzo ya Fedha na Usimamizi wa Fedha, Ukaguzi na shughuli za Benki.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Ukwasi wa Zanzibar, ikilinganishwa na Tanganyika, ulikuwa wa kiwango cha juu wakati wa Karume kutokana na bei nzuri ya karafuu katika soko la dunia, ambapo ilipanda kutoka dola za Kimarekani 550 hadi dola 1,500 kwa tani, kiasi kwamba kufikia mwaka 1971, Zanzibar ilikuwa na akiba ya fedha za kigeni ya pauni za Uingereza (£) 14,000,000, ikilinganishwa na 6,500,000 za Tanzania Bara.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Ukakasi juu ya ushiriki au la, wa Zanzibar katika EACB, umiliki wa hisa, gawiwo la faida za EACB na kuhusu uanzishaji wa BoZ kufuatia Muungano na Tanganyika, ulimalizwa na Katibu wa EACB, H.R. Hirst, katika ufafanuzi wake kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha wa Serikali ya Muungano wa wakati huo, D. Namfua, akisema, “Katiba ya Mpito ya Jamhuri ya Muungano, haikuhamishia mambo ya Fedha na Sarafu ya nchi hizi kwa Serikali ya Muungano na hivyo uanachama wa Zanzibar wa EACB haukuathirika”, akimaanisha kuwa, mambo ya Fedha na Sarafu hayakuwa ya Muungano hivi kwamba kila nchi ilikuwa na uhuru wa kuwa na Benki Kuu na sarafu yake.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Kuna Documentary aliandaa Mwandishi Na Mwanahistory Mohamed Said kuhusu KipumbwiMkuu kitabu safi hiki,kilipelekea kupata hii ID name yangu licha ya kuwa nimeshafika sehemu tajwa ya ID ila mchango wake kwenye Uhuru wa Zanzibar uliniongezea maarifa!
Ule ukweli kwamba mambo ya Fedha, Sarafu na uhalali wa Zanzibar kuanzisha BoZ hayakuwa mambo ya Muungano wakati huo, uliipa matumaini na haki isiyohojika kuweza kunufaika na kile ilichowekeza kwenye EACB kabla na baada ya Muungano, jambo ambalo halikupokelewa vyema na Serikali ya Muungano.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.
Muswada wa Marekebisho ya Katiba kufanya mambo ya Fedha na Sarafu kuwa ya Muungano uliwasilishwa kwenye Bunge la kawaida, tarehe 10 Juni 1965, na kupitishwa kwa kasi isiyo kawaida. Wakati huo, Mwalimu Nyerere alikuwa safari nje ya nchi.Wapenda umbea tafuteni hii “Karume aliuliwa sababu ya Muungano”.