Maumivu ya bajeti ya 2021 yako hapa kwa wananchi wa kawaida

Maumivu ya bajeti ya 2021 yako hapa kwa wananchi wa kawaida

Rais wetu ajue kuwa kuongeza kodi kwenye miamala itapunguza mzunguko wa pesa na kuwakatisha tamaa watu kuweka fedha zao benki ambazo ndizo wafanya biashara na wawekezaji wanakopeshwa ili kuwekeza katika uzalishaji!!!
Kutoza kodi zaidi kwenye miamala sio njia sahihi ya kuongeza pato la serikali; ongeza kodi kwenye vileo vikali na pia huko kwa wacheza kamail itapendeza!
 
Ukigusa mafuta hata Kama budhaa zingine zitabaki hivyo hivyo lakini lazima kila kitu kipande kwa sababu mafuta ni injini ya uchumi kwa nchi.
 
Mkuu mapendekezo yote yatamgusa mtu wa kawaida fikiria kuongeza ushuru wa kiasi 100 kwenye mafuta yote hapo lazima gharama za usafiri zipande hivyo kupelekea bidhaa kupanda bei na huenda mfumuko wa bei maana mzigo wote huo anaubeba final consumer

Halafu waziri haoni hayo anajichekesha eti hata akipendwa na watu wa jimbo lake na wa Yanga inatosha watakupendaje ili hali unaibana hali yao ya maisha au wao hawataathirika??
Ametumia kauli ya kibwege sana
 
Rais wetu ajue kuwa kuongeza kodi kwenye miamala itapunguza mzunguko wa pesa na kuwakatisha tamaa watu kuweka fedha zao benki ambazo ndizo wafanya biashara na wawekezaji wanakopeshwa ili kuwekeza katika uzalishaji!!!
Kutoza kodi zaidi kwenye miamala sio njia sahihi ya kuongeza pato la serikali; ongeza kodi kwenye vileo vikali na pia huko kwa wacheza kamail itapendeza!
Watu watumie bank gharama ni ndogo kuliko za simu
 
Kila ninapoweka vocha, kununua muda wa maongezi au kununua bundle huwa ninakatwa kodi ya Vat (18%), sasa inakuwaje tena leo ninaongezewa mzigo mwingine mpya wa kodi?
Sio hivyo tu na gharama ya kutoa pesa kwenye simu itaongezeka licha ya kwamba hata rates za sasa zinatutesa !
 
Sio hivyo tu na gharama ya kutoa pesa kwenye simu itaongezeka licha ya kwamba hata rates za sasa zinatutesa !
Hali lazma izidi kuwa mbaya tu,mm nilidhani hapa ndio pa kuchukua credit kwa mama ila sijui kama alikaa na kuchambua hii baje kabla ya kuwasilishwa
 
Utekelezaji wa hatua hizi nne kwa pamoja unatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 2,033,639.66.

👆👆👆👆
Kwahiyo mabadiliko yote hayo yataiongezea serikali ya Tanzania kiasi cha Tsh 2,033,639.66./milioni mbili, na elfu thelathini na tatu, mia sita thelathini na tisa pointi sita sita? 😊😊

😁Nacheka kwa masikito hapa
Milioni 2,033,639.66 = 2,033,639.66 x 1,000,000. Hiyo ni njia tu ya kufupisha uandishi.
 
Utekelezaji wa hatua hizi nne kwa pamoja unatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 2,033,639.66.

👆👆👆👆
Kwahiyo mabadiliko yote hayo yataiongezea serikali ya Tanzania kiasi cha Tsh 2,033,639.66./milioni mbili, na elfu thelathini na tatu, mia sita thelathini na tisa pointi sita sita? 😊😊
Tarakimu/Hesabu iko sawa mkuu kwa sababu ameanza na neno Milioni maana yake ni kuwa katika tarakimu hizo ongeza 0 sita. Ndiyo Hesabu za Kihasibu zinaandikwa hivyo mkuu.
 
Tarakimu/Hesabu iko sawa mkuu kwa sababu ameanza na neno Milioni maana yake ni kuwa katika tarakimu hizo ongeza 0 sita. Ndiyo Hesabu za Kihasibu zinaandikwa hivyo mkuu.
Hebu andika hapa kwa tarakimu
 
Back
Top Bottom