Maumivu ya bajeti ya 2021 yako hapa kwa wananchi wa kawaida

Maumivu ya bajeti ya 2021 yako hapa kwa wananchi wa kawaida

Ina maana gharama za kutoa pesa Kama mpesa zitaongezeka ?


Hii nchi mbona ngumu Sana lini tutakuwa na unafuu wa maisha ?
Siku CCM ikitolewa madarakani. Iwe ni kwa kupitia sanduku la kura au hata kwa kutumia jeshi au nguvu ya umma.
 
(i) Kutoza tozo ya shillingi 10 hadi shilingi 10,000 katika kila muamala wa kutuma au kutoa pesa. Kiasi cha tozo kinatofautiana kulingana na thamani ya muamala wa fedha unaotumwa au kutolewa. Pendekezo hili litaongeza mapato ya Serikali kiasi cha shillingi milioni 1,254,406.14; na

(ii) Kutoza kiasi cha shilingi 10 hadi shilingi 200 kwa siku kwa kila laini ya simu kulingana na uwezo wa kuongeza salio kwa watumiaji. Pendekezo hili litapelekea kuongeza mapato ya Serikali kiasi cha shillingi milioni 396,306.0.

d. Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147

Kutokana na vinywaji vikali kuwa na kiwango kikubwa cha kilevi, napendekeza kuongeza ushuru wa bidhaa kwa asilimia 30 ili kuwa na uwiano wa viwango vya kodi kati ya Vinywaji kali na Bia. Hatua hii inatarajia kuiongezea mapato Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 60,769.35.

Utekelezaji wa hatua hizi nne kwa pamoja unatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 2,033,639.66.

U. Tarehe ya Kuanza Kutekeleza Hatua Mpya za Kodi

89. Mheshimiwa Spika, hatua hizi za kikodi zinazopendekezwa zitaanza kutekelezwa tarehe 1 Julai, 2021, isipokuwa pale itakapoelezwa vinginevyo. Aidha, Marekebisho hayo yataainishwa katika Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2021 na Matangazo ya Serikali (Government Notices).
[emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516]
Binafsi naona huu ni mzigo kwa wananchi wa kawaida kwa sababu wao ndio watumiaji wakubwa wa huduma hizo. Kwanini hayo makato yasingekuwa kwenye miamala mikubwa ya kibenk badala ya kukata 100 kwenye vocha ya 500!?

Unapandisha bia ya 1500 kwa 30% unataka watu wanywe gongo? Kwanini iyo asilimia usiweke kwenye Hennessy au Jack Daniel? Unataka double kick tuanze kununua 2500 tena? Una hamasisha vijana kubet badala ya kazi?

Mods please msiunge uzi huu nataka kila mtanzania atoe maoni yake kwenye wazi tofauti na uzi wa bajeti yote.
Nadhani hujaelewa chochote kwenye bajeti ile.
 
Watu watumie bank gharama ni ndogo kuliko za simu
Utasemaje gharama za benki ni ndogo wakati sasa wanataka kutoza kodi unapoweka na unapotoa fedha benki? Na pia gharama za uendeshaji benki zinapoongezeka , gharama hizo zinaongeza charges ambazo benki wanawatoza wateja wao!!! So good for financial inclusion!!!
 
Mtoa mada hajaelewa zaidi ya kulalamika tu.
Wabongo ni washamba na wapumbavu. Kila kitu ni kulalamika tu. Kenya wenzetu bajeti yao iko 78 TRILLION ni kwa sababu wamepanua wigo wa kodi. Sisi tunaanza kutanua watu wanaanza lalama. Wapumbavu na malofa.

Bajeti ya bongo haina vyanzo vipya vya kodi hivyo huwezi kusema mnatanua wigo!!! Manaongeza kodi tu kwenye vyanzo vile vile nya siku zote:- pombe, Simu, sigara, petrol basi hakuna wigo mliopanua !!! Halafu kodi yenyewe percentage kuwa inakwenda kwenye matumizi ya kawaida ya mishahara na posho badala ya kuwa kwenye maendeleo!!
 
Bajeti ya bongo haina vyanzo vipya vya kodi hivyo huwezi kusema mnatanua wigo!!! Manaongeza kodi tu kwenye vyanzo vile vile nya siku zote:- pombe, Simu, sigara, petrol basi hakuna wigo mliopanua !!! Halafu kodi yenyewe percentage kuwa inakwenda kwenye matumizi ya kawaida ya mishahara na posho badala ya kuwa kwenye maendeleo!!
Mafuta ya taa ndio yameongezwa kodi mkuu, pombe imeshuka kodi, kwenye kubeti kumeshuswa mpka 15%, kodi ya jengo imerahisishwa na hii itapelekea watu wengi kulipa hii kodi bila kuhisi maumivu kwa miaka ya karibuni hii ndio bajeti nafuu.
 
Mafuta ya taa ndio yameongezwa kodi mkuu, pombe imeshuka kodi, kwenye kubeti kumeshuswa mpka 15%, kodi ya jengo imerahisishwa na hii itapelekea watu wengi kulipa hii kodi bila kuhisi maumivu kwa miaka ya karibuni hii ndio bajeti nafuu.

Kwanini ushushe kodi kwenye kamali halafu upandishe kwenye miamala ya simu na benki? Hapo kuna walakini!!
Hawa wenye hii michezo ya Kamari [ Betting na Casinos] wanavuna mabillion ya shilling kila siku na hizo fecha zinatoroshwa kwenda nje!!!! Eneo hili serikali iliangalie kwa karibu sana.
 
Kwanini ushushe kodi kwenye kamali halafu upandishe kwenye miamala ya simu na benki? Hapo kuna walakini!!
Hata mimi hilo mim nashangaa sana,kuna umuhimu gani wa kumpunguzia mcheza kamari kodi? Kwa mujib wa waziri ni kuwa mcheza kamari ni muhimu zaidi kuliko mawasiliano?
 
(i) Kutoza tozo ya shillingi 10 hadi shilingi 10,000 katika kila muamala wa kutuma au kutoa pesa. Kiasi cha tozo kinatofautiana kulingana na thamani ya muamala wa fedha unaotumwa au kutolewa. Pendekezo hili litaongeza mapato ya Serikali kiasi cha shillingi milioni 1,254,406.14; na

(ii) Kutoza kiasi cha shilingi 10 hadi shilingi 200 kwa siku kwa kila laini ya simu kulingana na uwezo wa kuongeza salio kwa watumiaji. Pendekezo hili litapelekea kuongeza mapato ya Serikali kiasi cha shillingi milioni 396,306.0.

d. Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147

Kutokana na vinywaji vikali kuwa na kiwango kikubwa cha kilevi, napendekeza kuongeza ushuru wa bidhaa kwa asilimia 30 ili kuwa na uwiano wa viwango vya kodi kati ya Vinywaji kali na Bia. Hatua hii inatarajia kuiongezea mapato Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 60,769.35.

Utekelezaji wa hatua hizi nne kwa pamoja unatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 2,033,639.66.

U. Tarehe ya Kuanza Kutekeleza Hatua Mpya za Kodi

89. Mheshimiwa Spika, hatua hizi za kikodi zinazopendekezwa zitaanza kutekelezwa tarehe 1 Julai, 2021, isipokuwa pale itakapoelezwa vinginevyo. Aidha, Marekebisho hayo yataainishwa katika Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2021 na Matangazo ya Serikali (Government Notices).
☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️
Binafsi naona huu ni mzigo kwa wananchi wa kawaida kwa sababu wao ndio watumiaji wakubwa wa huduma hizo. Kwanini hayo makato yasingekuwa kwenye miamala mikubwa ya kibenk badala ya kukata 100 kwenye vocha ya 500!?

Unapandisha bia ya 1500 kwa 30% unataka watu wanywe gongo? Kwanini iyo asilimia usiweke kwenye Hennessy au Jack Daniel? Unataka double kick tuanze kununua 2500 tena? Una hamasisha vijana kubet badala ya kazi?

Mods please msiunge uzi huu nataka kila mtanzania atoe maoni yake kwenye wazi tofauti na uzi wa bajeti yote.
Kuna tozo kwenye petrol, Boda Boda wanashangilia kupunguziwa faini ambayo alikuwa hailipi kila siku, anasahau ongezeko la shilingi Mia moja Kwa kila Lita ya mafuta, ambapo kila Lita tano kuna ongezeko la shilingi Mia tano, endapo kila siku atajaza Lita tano kwenye pikipiki yake Kwa siku thelathini ni elfu 15, hii gharama bodaboda atairudisha Kwa abiria, huyu ndo Yule Yule ambaye ni mpangaji atakayelazimika kulipa Kodi ya jengo kupitia matumizi ya Luku, hii ni tofauti na Kodi ya chumba. Huyu ndo anakatwa shilingi 10 kila siku toka kwenye line yake, maumivu
 
Kuna tozo kwenye petrol, Boda Boda wanashangilia kupunguziwa faini ambayo alikuwa hailipi kila siku, anasahau ongezeko la shilingi Mia moja Kwa kila Lita ya mafuta, ambapo kila Lita tano kuna ongezeko la shilingi Mia tano, endapo kila siku atajaza Lita tano kwenye pikipiki yake Kwa siku thelathini ni elfu 15, hii gharama bodaboda atairudisha Kwa abiria, huyu ndo Yule Yule ambaye ni mpangaji atakayelazimika kulipa Kodi ya jengo kupitia matumizi ya Luku, hii ni tofauti na Kodi ya chumba. Huyu ndo anakatwa shilingi 10 kila siku toka kwenye line yake, maumivu
Tutaiona nchi ya ahadi siku CCM iking'olewa !!
 
faini ya bodaboda itaongeza bei kwenye usafiri wa boda, tunarudi kwenye baiskeli
 
Mama asipoingilia huenda JPM akakumbukwa hasa na wale wananchi wa kawaida,aliozoea kuwaita wanyonge
Kama unadhani wamemsahau JPM basi ww utakuwa unaishi NY ama oysterbay mzee ..no one like JPM
 
Utekelezaji wa hatua hizi nne kwa pamoja unatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 2,033,639.66.

[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]
Kwahiyo mabadiliko yote hayo yataiongezea serikali ya Tanzania kiasi cha Tsh 2,033,639.66./milioni mbili, na elfu thelathini na tatu, mia sita thelathini na tisa pointi sita sita? [emoji4][emoji4]
Mapato Haramu
 
Mkuu mapendekezo yote yatamgusa mtu wa kawaida fikiria kuongeza ushuru wa kiasi 100 kwenye mafuta yote hapo lazima gharama za usafiri zipande hivyo kupelekea bidhaa kupanda bei na huenda mfumuko wa bei maana mzigo wote huo anaubeba final consumer

Halafu waziri haoni hayo anajichekesha eti hata akipendwa na watu wa jimbo lake na wa Yanga inatosha watakupendaje ili hali unaibana hali yao ya maisha au wao hawataathirika??
Hivi kwann sijawahi sikia swala la ruzuku katika biashara ya mafuta.
 
Kama unadhani wamemsahau JPM basi ww utakuwa unaishi NY ama oysterbay mzee ..no one like JPM
Shida ya JPM aliendana na wanyonge na kuwachukia wafanyabishara,akawa na bifu nao. Huyu mama kaleta usawa ila kama bajeti zitabana hivi basi huenda akaanza kupiteza mvuto
 
Back
Top Bottom