Mawakili wa utetezi punguzeni muda wa cross examination, kesi ya Mbowe yaweza kuamuliwa kwa haki kabisa hapa ilipofikia

Mawakili wa utetezi punguzeni muda wa cross examination, kesi ya Mbowe yaweza kuamuliwa kwa haki kabisa hapa ilipofikia

Ni kweli! Lakini lazima wahoji ili kutoacha shaka yo yote kwenye Utetezi.
... na ukichunguza kwa makini utaona mawakili wa serikali kuna vitu vya msingi sana hawawaulizi mashahidi wao kwa sababu wanazozijua wao! Vinakuja kuwekwa hadharani na mawakili wa utetezi.

Mashahidi wa michongo wanatakiwa wawe screwed to the maximum extent possible sio tu kwa ajili ya utetezi wa shauri lililoko mahakamani lakini pia kupeleka "clear and loud" message kwa wahusika kwamba mipango yao ya kishetani inafahamika.
 
Shida yako ni kesi iishe mapema au haki ipatikane haya ni maisha na haki za watu.chakupambania ni haki ipatikane swala la muda halina msingi kwasababu hakunaga kesi ndogo.Kama hujui dhamira ya adui yako lazima kupambana kwa silaha kali kali hadi mwisho.
 
Mkuu Yoda heshima kwako kwanza. Cross examination ni muhimu sana linapokuja swala la kumpima na kumtikisa shahidi. So unaposema wapunguze muda na kuachana na cross examination kwa baadhi ya mashahidi maanaake ni kukubalianana na ushahidi alioutoa. Kwa upande wa utetezi hilo haliwezekani kamwe.
Mashahidi 12 wa Jamuhuri wametosha kabisa kumuonyesha jaji na ulimwengu wote kama Mbowe na wenzake wanapaswa kuachaliwa au kufungwa miaka 30 kwa hayo makosa wanayoshtakiwa nayo. Hakutakuwa na jambo jipya katika mashahidi waliobaki, labda kidogo sana aliyekiwa DCI.
 
Usisahau Mbowe hajasimama kizimbani na atadodoswa kwa miezi 6
 
Hela baba inaingia sio makelele ya bure pale mahakamani
Hela ipi inayokuuma wewe raia mnyonge?
Za mawakili wa Mbowe ambazo hazikuhusu au za mawakili wa Jamuhuri na Jaji ambazo ni kodi yako?
 
Baada ya ushahidi wa Luteni Denis Urio kwa upande wa Jamhuri kesi ya Mbowe ambayo imefikisha mashahidi 12 sasa inaweza kuamuliwa na Jaji. Shahidi aliyekuwa muhimu kuliko wote na ambaye anaweza kuitwa nyota au kiungo muhimu wa mchezo ni Urio ambaye amekwisha toa ushahidi wake...
Huu ni ushauri wa kitasnia au wakisiasa? Mnataka ku-limit damage na aibu mnayoipata kutokana na Cross examination mahiri?
 
Ni vyema waulize maswali yote. Kwenye kuuliza pia unaweza ukagundua vitu kama ukiukwaji wa taratibu, mashahidi wengine haswa maaskari wanaweza shitakiwa baada ya hii kesi kupitia shahidi zao n.k
Hakuna shahidi wa upande wa Jamuhuri atakayeshitakiwa baada ya hii kesi kwisha.
 
Walio mdaganya Raisi kwamba Mbowe ana kesi nzito na atafungwa, Raisi akaanza kuongea uko BBC wajitafakali tu au wajiuzuru, kwa ushahidi ulioletwa so far, Jaji anaona tu aibu kusema kwamba hapa hamna kesi ya kujibu na hamna haja upande wa utetezi kuleta mashahidi.

Kama Urio ndo key witness ana ushahidi manaake hata wale wote tigo airtel wali base kwenye huo ushahidi dhaifu wa Urio eti " mda unaisha" huo ndo ushahidi wa ugaidi ufunge mtu, Raisi wa Tz msiwe mna amiini sana wateuzi wenu sasa ona hi aibu ya Taifa, wewe umeuziwa kesi na mwendazake.
Waendelee tu kuwahoji hawa mashahidi wa mchongo. Tungejuaje kuwa kwa jeshi la polisi mtu akitamka neno "Muda Umeisha" kwao huo ndio Ugaidi wenyewe. Basi Tanzania hii yote imejaa magaidi. Hata Jaji mwenyewe basi ni gaidi maana kuna siku aliwaambia mawakili wasirudie walichokisema wengine ili kuokoa muda, yaani muda usiishe bure.
 
Baada ya ushahidi wa Luteni Denis Urio kwa upande wa Jamhuri kesi ya Mbowe ambayo imefikisha mashahidi 12 sasa inaweza kuamuliwa na Jaji. Shahidi aliyekuwa muhimu kuliko wote na ambaye anaweza kuitwa nyota au kiungo muhimu wa mchezo ni Urio ambaye amekwisha toa ushahidi wake.

Kwa muelekeo wa mashahidi waliopita mambo mengi yatakuwa ni ya kujirudia rudia tu kutoka upande wa mashahidi wengi waliobaki. Kupunguza urefu wa hii kesi Mawakili wa utetezi wafanye cross examination isiyozidi saa moja kwa baadhi ya mashahidi wa kawaida na wasifanye cross examination kabisa kwa angalau mashahidi sita.

Kwa mpango huu itafanya uwezekano wa kuwepo angalau shahidi mmoja kila siku na na kumaliza upande wa mashahidi wa Jamhuri ndani ya wiki tatu ila upande wa utetezi uanze kuletea mashahidi wake na kuimaliza kesi mapema.
Waendelee tu na muda mrefu. Maana maswali mengi hufanya muongo na mpandikizwa kujulikana
 
Lazimz tuhakikishe Jaji hapati kigugumizi cha kufutilia mbali hii kesi. Kila kitu kiwe wazi. Hii kesi imekuwa darasa.
Haitakaa itokee kwa mahakama ya Tanzania ya sasa Jaji kufuta kesi kama hii inayotokana na siasa.
Mwenye kuweza kuifuta ni serikali tu kupitia DPP.
 
Waendelee tu na muda mrefu. Maana maswali mengi hufanya muongo na mpandikizwa kujulikana
Wakiendelea hivi kesi itamaliza mwaka wote huu, hata mawikili wa utetezi watachoka.
 
Baada ya ushahidi wa Luteni Denis Urio kwa upande wa Jamhuri kesi ya Mbowe ambayo imefikisha mashahidi 12 sasa inaweza kuamuliwa na Jaji. Shahidi aliyekuwa muhimu kuliko wote na ambaye anaweza kuitwa nyota au kiungo muhimu wa mchezo ni Urio ambaye amekwisha toa ushahidi wake.

Kwa muelekeo wa mashahidi waliopita mambo mengi yatakuwa ni ya kujirudia rudia tu kutoka upande wa mashahidi wengi waliobaki. Kupunguza urefu wa hii kesi Mawakili wa utetezi wafanye cross examination isiyozidi saa moja kwa baadhi ya mashahidi wa kawaida na wasifanye cross examination kabisa kwa angalau mashahidi sita.

Kwa mpango huu itafanya uwezekano wa kuwepo angalau shahidi mmoja kila siku na na kumaliza upande wa mashahidi wa Jamhuri ndani ya wiki tatu ila upande wa utetezi uanze kuletea mashahidi wake na kuimaliza kesi mapema.
Wafadhili wao wametoa Hela nyingi, ndio maana wanafanya hivyo kuwaridhisha
 
Cross examination ndiyo njia pekee ya kuona namna kesi ya mchongostic ilivyo.
 
Back
Top Bottom