Nilifuatilia mkutano wa waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi na waandishi wa habari uliochukua takriban dakika 70, na jambo muhimu kwangu ni yeye kuzungumza kuhusu ushirikiano wa China na Afrika.
Muhimu zaidi ni yeye kujibu madai kuwa China inaweka mitego ya madeni barani Afrika.
Wang Yi mwanzo alisisitiza kuwa China inaunga mkono maendeleo Afrika, huku akitoa mfano ya miradi kama vile Kilomita 10,000 za reli, zaidi ya kilomita 100,000 za barabara kuu, takriban bandari 100 pamoja na hospitali na shule zisizohesabika zilizojengwa kupitia msaada wa China barani Afrika.
Kwa kweli, hizi sio mitego ya madeni bali ni nguzo za ushirikiano uliopo kati na Africa na China.
Pia nilifurahia kwamba Wang Yi aliweka bayana kuwa mipango 9 ya maendeleo yaliyotangazwa na Rais Xi Jinping kufadhiliwa na China barani Afrika yataanza kutekelezwa mwaka huu. Hii bila shaka itaongeza maendeleo Afrika.
Yeye kusema China itaheshimu ahadi yake kwa Afrika na kwamba kamwe haitatoa ahadi tupu ni ujumbe mwingine muhimu sana.
Ni muhimu pia kwamba mwanadiplomasia huyo wa ngazi za juu wa China aliahidi kuwa China itapanua ushirikiano dhidi ya covid na Afrika hasa kwa kutimiza ahadi ya kutoa dozi bilioni 1 za chanjo kwa Afrika mwaka huu.
Mipango muhimu ya maendeleo yanayofadhiliwa na China kama vile Ukanda Mmoja Njia Moja yatasaidia kuongeza maendeleo na kufufua uchumi wa Afrika baada ya chamuko la covid na ni muhimu kwamba Wang Yi aliahidi kuhakikisha ushirikiano utaendelea kupitia mpango huo wa Belt and Road.
Mbali na masuala ya Afrika na China, nina furaha kuwa alizungumzia mgogoro wa Ukraine. Taarifa yake kuwa China haipendelei pande yeyote ile na kwamba itachukua jukumu la kuwezesha mazungumzo ya amani na kushirikiana na jamii ya kimataifa kutatua mgogoro huo ilikuwa ya maana sana.
Kwa maoni yangu, hii ilikuwa ni ujumbe uliofaa mno na wa kutoa hakikisho kwa washirika wake na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.