Maxence Melo ateuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi

Maxence Melo ateuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi

Kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kumteua Balozi Adadi Mohammed Rajab kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, na Bi. Fatma Mohammed Ali kuwa Makamu Mwenyekiti, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Nape Moses Nnauye (MB.), kwa Mamlaka aliyopewa na Ibara ya 8(2) ya Sheria ya Ulinzi wa Tarifa Binafsi Na. 11 ya 2022, amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwa kipindi cha miaka 3;

1. Bw. Ramadhan Athumani Mungi, Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Polisi Moshi;

2. Bw. Edward Samweli Lyimo, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria, Benki ya Biashara ya Taifa (NBC);

3. Bw. Hamid Haji Machano, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Zanzibar;

4. Bi. Frida Peter Mwera; Mwandishi wa Sheria Mkuu, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
wa Serikali; na

5. Bw. Maxence Melo Mubyazi, Mkurugenzi Mtendaji, Jamii Forums;

Uteuzi huu unaanza leo tarehe 18 Disemba, 2023 hadi tarehe 18, Disemba 2026.
View attachment 2846438
Naipongeza sana JamiiForums kupata seat hapo.
Nampongeza Maxence Melo kwa kuaminiwa na kutruliwa. Sina shaka naye hata kidogo kwani anajua kujenga hoja na ana ushawishi wenye tija.

Tunatarajia wajumbe wa Kamati hii watatimiza majukumu yao kwa maslahi mapana ya Taifa.

Mungu awatangulie
 
Km haina madhara kwake kuukataa uteuzi huo akatae haraka sana,hautakuwa na mwisho mzuri kwa ndege aliyekubali kusogezwa katikati ya kipago cha manati na hapo mlengwa ni Melo hao wengine ni changa la macho.
Kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kumteua Balozi Adadi Mohammed Rajab kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, na Bi. Fatma Mohammed Ali kuwa Makamu Mwenyekiti, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Nape Moses Nnauye (MB.), kwa Mamlaka aliyopewa na Ibara ya 8(2) ya Sheria ya Ulinzi wa Tarifa Binafsi Na. 11 ya 2022, amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwa kipindi cha miaka 3;

1. Bw. Ramadhan Athumani Mungi, Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Polisi Moshi;

2. Bw. Edward Samweli Lyimo, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria, Benki ya Biashara ya Taifa (NBC);

3. Bw. Hamid Haji Machano, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Zanzibar;

4. Bi. Frida Peter Mwera; Mwandishi wa Sheria Mkuu, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
wa Serikali; na

5. Bw. Maxence Melo Mubyazi, Mkurugenzi Mtendaji, Jamii Forums;

Uteuzi huu unaanza leo tarehe 18 Disemba, 2023 hadi tarehe 18, Disemba 2026.
View attachment 2846438
 
Hivi mbwa kwanini Huwa analia huku anajipeleka mwenyewe mdomoni mwa chatu?
Pheromones ni aina ya kichocheo kinachozalishwa kwa wanyama mbalimbali kwa ajili ya kujaamiana, kutafuta chakula/kuwinda n.k

Kuna harufu mbwa anavutiwa nayo ndio maana anajipeleka kwa chatu.

Rabon, unataka kutuambia nini baada ya uteuzi huu? Au ndio tunawindwa na chatu kwa kumtumia max kama chambo ili chatu aweze kula kilaini?
 
Ni wakati sahihi kwa Mkuu Max kujitokeza na kusema jambo au aweke mikakati mipya juu ya utumiaji wa huu .

Afanye ajambo ambalo litawafanya watu walio ndani ya Mtandao wake kupata kuwa na amani na siri zao...
Siku si nyingi hoja ngumu na zenye kuweka mambo wazi yaliyofichika ndani ya jamii na serikarini yatapunguzwa kujadiliwa humu.


Hongera kwako Kaka Max kwa kitengo kipya.
 
Habari zaidi hii hapa

Screenshot_2023-12-18-21-52-00-1.png
 
Baadhi ya watu wameuchukulia huu uteuzi in negative way wanahis labda Melo atawachomesha 😄Wabongo acheni mambo ya ajabu hv nan anatoaga taarifa sensitive humu? Si tunakeshaga wote MMU? Mada nyingi za siasa hazina sensitivity tunayoaminishana kias hicho

Sema wengi wetu tunaogopa kujulikana maana Kuna uongo mwingi tumesema 🤣unakuta jobless aliehitimu 2014 anakaaa mugumu Serengeti au kilombero lkn humu anavojitambulia anajieleza as diaspora anaefanya Kazi denmark
 
Back
Top Bottom