Mbarali: Ng'ombe zaidi ya 400 ambao ni mali ya Wananchi kupigwa mnada leo

Mbarali: Ng'ombe zaidi ya 400 ambao ni mali ya Wananchi kupigwa mnada leo

Ukame una wachapaga huko monduli longido na maeneo mengine simanjiro nk

Mifugo ina pukutika kama kuku wa mdondo
Sahihi kabisa. Lazima tuyalinde mazingira kwa gharama yoyote ile, huo ndio uhai wetu na watoto wetu. Monduli na Lungido hakufai kabisa, ni kukame balaa, nenda huko Shinyanga ni kukame hatari. Mifugo lazima ifugwe kwa kuzingatia usalama wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji. Hiyo mikoa ya kilimo tusiiharibu kwa ufugaji uliopitiliza.
 
Ufugaji wa kuhama hama hauna nafasi tena kwenye Karne hii ya 21. Kama mtu hawezi kufuga kwa kutulia auze tu ng'ombe wake wote. Tukiwachekea wafugaji siku si nyingi nchi hii itageuka jangwa
Mabadiliko ya hali ya hewa yanasababishwa na mengi, wala sio wafugaji pekee, hata hao matajiri wanasiasa wanaochepusha maji ya mito nao wanasababisha mito kukauka, hao wafugaji wasitupiwe kila lawama kwamba ndio chanzo.
 
Umetembelea mikoa ya wafugaji umeona kulivo kukame? Unataka tuharibu na mikoa yenye asili ya kilimo kisha tutaishi vipi? Mkuu lazima tubadilike na hakuna mabadiliko yasiyo na maumivu. Mifugo hiyo ipigwe mnada kama wanaweza watanunua wao wenyewe na wasipoheshimu sheria watanyang'anywa tena. Mazingira lazima tuyalinde kwa nguvu zote kwa kuwa hayo ni muhimu kwa wanadamu na viumbe wengine.
Ukame upo kote, hata huku Dsm ambapo hakuna wafugaji nako kuna ukame, jua kali kila upande, hao wafugaji wameonewa, wao pekee sio chanzo kikuu cha huu ukame unaosababisha ukosefu wa mvua na kuleta migao ya maji.
 
Ukame upo kote, hata huku Dsm ambapo hakuna wafugaji nako kuna ukame, jua kali kila upande, hao wafugaji wameonewa, wao pekee sio chanzo kikuu cha huu ukame unaosababisha ukosefu wa mvua na kuleta migao ya maji.
Hujatembea hii nchi, tembea uone mkuu.
 
Taarifa iliyotufikia hivi punde inaeleza kwamba ng'ombe hao wa wananchi wa Mbarali ambao idadi kamili ni 433, wanaodaiwa kukamatwa na Askari wa Wanyamapori kwenye hifadhi wanapigwa mnada leo 14/11/2022

Bali kampuni iliyopewa tenda ya kupiga mnada ng'ombe hao wa Wananchi inaitwa MBARALI HIGHLAND AUCTION MART LTD, Inayomilikiwa na Mbunge wa zamani wa CCM aliyetajwa kwa jina moja la Haroon , ambaye pia ndiye aliyeuziwa Mashamba ya Wananchi hao kwenye utawala wa awamu ya 4, yaani mtu aliyepora mashamba ya wananchi ndiye aliyepewa tenda ya kuuza mifugo yao.

Lakini Kanuni ya Mungu ile ya KILA UBAYA UTALIPWA ingali bado inafanya kazi.

Mungu wabariki wananchi wa Mbarali .

==
LEO, ng’ombe 433 waliokamatwa katika eneo la ardhi oevu ya Bonde la Ihefu, ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha wilayani Mbarali wanatazamiwa kupigwa mnada mkoani Mbeya.

Hatua hiyo imekuja baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) kufanya oparesheni ili kuondoa zaidi ya mifugo 200,000 iliyovamia eneo hilo.

Mbali na kuhatarisha ikolojia ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, mifugo inahatarisha pia Mto Ruaha Mkuu.

Akitoa taarifa ya uvamizi wa bonde hilo la Ihefu, Mkuu wa Hifadhi ya Ruaha, Godwell Ole Meng’ataki anasema katika kipindi cha miaka miwili wamekamata mifugo 12,758 katika hifadhi hiyo.

Anasema licha ya kuwatoza faini wafugaji kiasi cha kukusanya zaidi ya Sh bilioni 1.2 katika kipindi hicho, wafugaji wameendelea kurejesha mifugo ndani ya hifadhi.

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune anasema eneo lililotengwa kwa ajili ya mifugo katika wilaya hiyo linatosheleza mifugo isiyozidi 60,000, lakini wilaya hiyo ina mifugo zaidi ya 200,000.

Tatizo la mifugo kuvamia maeneo ya misitu haliko Ihefu pekee bali pia maeneo mengi, hasa katika mkoa wa Lindi, Pwani na Morogoro ambayo ina mito muhimu kwa ajili ya kutoa maji ya kunywa na hata mabwawa ya kuzalisha umeme.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, aliwahi kueleza namna misitu mingi ya mkoa wake inavyovamiwa na wafugaji, akisema baadhi ya wafugaji walioko Lindi wanazungumza lafudhi sawa na waliomaliza misitu mkoani Shinyanga ambako aliwahi kuhudumu pia kama mkuu wa mkoa.

Telack ambaye wasifu wake ni pamoja kusomea shahada ya uzamili katika maendeleo ya vijiji, Chuo Kkiku cha Sokoine cha Kilimo (SUA) anasema kilimo tunachosema ni uti wa mgongo kitashindikana kama hatutakuwa na misitu kwa sababu kilimo chetu kinategemea mvua na misitu ina nafasi kubwa ya kuvuta mvua na kulinda vyanzo vya maji.

Faida nyingine ya misitu kwa mwanadamu na viumbe hai wengine ni kunyonya hewa ukaa na kutoa hewa safi, kuwa makazi ya viumbe mbalimbali na kutoa miti-dawa.

Misitu huwezesha pia ufugaji wa nyuki, kutoa mbao za aina mbalimbali na nishati za kupikia kama mkaa na kuni na hasa kama vitu hivyo vitavunwa kwa njia endelevu.

Pamoja na kwamba Watanzania wanahitaji mifugo kwa ajili ya nyama na maziwa na pia kutoa ajira, ni wakati wa kuhakikisha wafugaji wanafuga kisasa, wanatumia maeneo waliyopangiwa, wanapunguza idadi ya mifugo na kulima malisho kwa ajili ya mifugo yao. Lazima wabadilike, ‘wahifadhi’ mifugo na si ‘kuichunga’.

Ni muhimu Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na viongozi wa mikoa mbalimbali kuboresha hali ya ufugaji ili kupunguza pia migogoro ya ardhi. Wahusika wasione kigugumizi kupiga mnada kila mahala ng’ombe walikovamia.

Chanzo: Habari Leo
Hii story imejaa politics nyingi,mala mifugo ya wakulima inapigwa mnada,mala kampuni inayoendesha mnada ni ya Mbunge wa zamani wa ccm aliyeuziwa mashamba ya wakulima!!
Sasa hapa Kuna hoja kama nne,
Mosi,Hawa ngombe wa wananchi,mamlaka iimewafata kwenye makazi yao ikawchukua kwa nguvu,au wafugaji walivunja sheria kwa kuingiza mifugo kwenye hifadhi,serikali ikakamata hiyo mifugo.!
Pili Huyu Mbunge wa zamani,kosa lake lipo wapi kuuziwa mashamba na kampuni yake kupewa kibali,Tena na mahakama ya kusimamia mnada,kwani utaratibu haukufwatwa?
Tatu,kwanini wafugaji hawana eneo la kunyweshea mifugo?walitengewa eneo au la!!
Nne,Hayo mashamba wanayodai,wamepolwa,ni kiasi gani walikuwa wanazalisha,wanalipa Kodi kiasi gani,na huyo Mbunge aliyeuziwa ana plan ya kuzalisha kiasi gani?na kulipa Kodi kiasi gani?
 
Hii story imejaa politics nyingi,mala mifugo ya wakulima inapigwa mnada,mala kampuni inayoendesha mnada ni ya Mbunge wa zamani wa ccm aliyeuziwa mashamba ya wakulima!!
Sasa hapa Kuna hoja kama nne,
Mosi,Hawa ngombe wa wananchi,mamlaka iimewafata kwenye makazi yao ikawchukua kwa nguvu,au wafugaji walivunja sheria kwa kuingiza mifugo kwenye hifadhi,serikali ikakamata hiyo mifugo.!
Pili Huyu Mbunge wa zamani,kosa lake lipo wapi kuuziwa mashamba na kampuni yake kupewa kibali,Tena na mahakama ya kusimamia mnada,kwani utaratibu haukufwatwa?
Tatu,kwanini wafugaji hawana eneo la kunyweshea mifugo?walitengewa eneo au la!!
Nne,Hayo mashamba wanayodai,wamepolwa,ni kiasi gani walikuwa wanazalisha,wanalipa Kodi kiasi gani,na huyo Mbunge aliyeuziwa ana plan ya kuzalisha kiasi gani?na kulipa Kodi kiasi gani?
Bora umeuliza maswali objective sana
 
Naona unyan'ganyi na uporaji, serikali inachangia pakubwa sana kukuza umaskini kwa wananchi wake, kuanzia tozo kila sehemu mpaka kuwanyan'ganya mifugo yao, kwangu faini ingekuwa adhabu ya haki kwa hao wafugaji, unless wakirudia tena, ndio wachukue sehemu ya mifugo yao, na sio yote.
Hivi unashahidi kuwa Ng'ombe waliokamatwa ni mara yao ya Kwanza kukamatwa au unataka kulaumu maamuzi sahihi ya serikali.Mm naunga mkono hoja acha Ng'ombe wapigwe mnada tuuu
 
Hivi unashahidi kuwa Ng'ombe waliokamatwa ni mara yao ya Kwanza kukamatwa au unataka kulaumu maamuzi sahihi ya serikali.Mm naunga mkono hoja acha Ng'ombe wapigwe mnada tuuu
Wangesema kwenye taarifa, wewe kama una ushahidi hao n'gombe kukamatwa hii sio mara yao ya kwanza weka hapa, maamuzi sahihi ya serikali maana yake nini.
 
Taarifa iliyotufikia hivi punde inaeleza kwamba ng'ombe hao wa wananchi wa Mbarali ambao idadi kamili ni 433, wanaodaiwa kukamatwa na Askari wa Wanyamapori kwenye hifadhi wanapigwa mnada leo 14/11/2022

Bali kampuni iliyopewa tenda ya kupiga mnada ng'ombe hao wa Wananchi inaitwa MBARALI HIGHLAND AUCTION MART LTD, Inayomilikiwa na Mbunge wa zamani wa CCM aliyetajwa kwa jina moja la Haroon , ambaye pia ndiye aliyeuziwa Mashamba ya Wananchi hao kwenye utawala wa awamu ya 4, yaani mtu aliyepora mashamba ya wananchi ndiye aliyepewa tenda ya kuuza mifugo yao.

Lakini Kanuni ya Mungu ile ya KILA UBAYA UTALIPWA ingali bado inafanya kazi.

Mungu wabariki wananchi wa Mbarali .

==
LEO, ng’ombe 433 waliokamatwa katika eneo la ardhi oevu ya Bonde la Ihefu, ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha wilayani Mbarali wanatazamiwa kupigwa mnada mkoani Mbeya.

Hatua hiyo imekuja baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) kufanya oparesheni ili kuondoa zaidi ya mifugo 200,000 iliyovamia eneo hilo.

Mbali na kuhatarisha ikolojia ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, mifugo inahatarisha pia Mto Ruaha Mkuu.

Akitoa taarifa ya uvamizi wa bonde hilo la Ihefu, Mkuu wa Hifadhi ya Ruaha, Godwell Ole Meng’ataki anasema katika kipindi cha miaka miwili wamekamata mifugo 12,758 katika hifadhi hiyo.

Anasema licha ya kuwatoza faini wafugaji kiasi cha kukusanya zaidi ya Sh bilioni 1.2 katika kipindi hicho, wafugaji wameendelea kurejesha mifugo ndani ya hifadhi.

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune anasema eneo lililotengwa kwa ajili ya mifugo katika wilaya hiyo linatosheleza mifugo isiyozidi 60,000, lakini wilaya hiyo ina mifugo zaidi ya 200,000.

Tatizo la mifugo kuvamia maeneo ya misitu haliko Ihefu pekee bali pia maeneo mengi, hasa katika mkoa wa Lindi, Pwani na Morogoro ambayo ina mito muhimu kwa ajili ya kutoa maji ya kunywa na hata mabwawa ya kuzalisha umeme.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, aliwahi kueleza namna misitu mingi ya mkoa wake inavyovamiwa na wafugaji, akisema baadhi ya wafugaji walioko Lindi wanazungumza lafudhi sawa na waliomaliza misitu mkoani Shinyanga ambako aliwahi kuhudumu pia kama mkuu wa mkoa.

Telack ambaye wasifu wake ni pamoja kusomea shahada ya uzamili katika maendeleo ya vijiji, Chuo Kkiku cha Sokoine cha Kilimo (SUA) anasema kilimo tunachosema ni uti wa mgongo kitashindikana kama hatutakuwa na misitu kwa sababu kilimo chetu kinategemea mvua na misitu ina nafasi kubwa ya kuvuta mvua na kulinda vyanzo vya maji.

Faida nyingine ya misitu kwa mwanadamu na viumbe hai wengine ni kunyonya hewa ukaa na kutoa hewa safi, kuwa makazi ya viumbe mbalimbali na kutoa miti-dawa.

Misitu huwezesha pia ufugaji wa nyuki, kutoa mbao za aina mbalimbali na nishati za kupikia kama mkaa na kuni na hasa kama vitu hivyo vitavunwa kwa njia endelevu.

Pamoja na kwamba Watanzania wanahitaji mifugo kwa ajili ya nyama na maziwa na pia kutoa ajira, ni wakati wa kuhakikisha wafugaji wanafuga kisasa, wanatumia maeneo waliyopangiwa, wanapunguza idadi ya mifugo na kulima malisho kwa ajili ya mifugo yao. Lazima wabadilike, ‘wahifadhi’ mifugo na si ‘kuichunga’.

Ni muhimu Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na viongozi wa mikoa mbalimbali kuboresha hali ya ufugaji ili kupunguza pia migogoro ya ardhi. Wahusika wasione kigugumizi kupiga mnada kila mahala ng’ombe walikovamia.

Chanzo: Habari Leo
Endeleeni kuishi kwa kutegemea Mungu atalipa, dunia ya hivyo imebaki Tanzania na ndiyo sababu viongozi wamejijengea viburi na kutuambia tuhamie Burundi tunawaghasi.
 
Wacha wapige mnada tu
Nimeshuhudia kwa macho jinsi mifugo inavyoharibu ardhi

Unakuta sehemu kuna umande mwaka mzima ila mifugo ikipita mwezi tu Ukame tayari

Wauze na hela hizo zipandiwe miti na kuchunga vyanzo vya maji

Huwa napinga mengi ila kuhusu haya nasapoti kwa kila hatua
 
Hii story imejaa politics nyingi,mala mifugo ya wakulima inapigwa mnada,mala kampuni inayoendesha mnada ni ya Mbunge wa zamani wa ccm aliyeuziwa mashamba ya wakulima!!
Sasa hapa Kuna hoja kama nne,
Mosi,Hawa ngombe wa wananchi,mamlaka iimewafata kwenye makazi yao ikawchukua kwa nguvu,au wafugaji walivunja sheria kwa kuingiza mifugo kwenye hifadhi,serikali ikakamata hiyo mifugo.!
Pili Huyu Mbunge wa zamani,kosa lake lipo wapi kuuziwa mashamba na kampuni yake kupewa kibali,Tena na mahakama ya kusimamia mnada,kwani utaratibu haukufwatwa?
Tatu,kwanini wafugaji hawana eneo la kunyweshea mifugo?walitengewa eneo au la!!
Nne,Hayo mashamba wanayodai,wamepolwa,ni kiasi gani walikuwa wanazalisha,wanalipa Kodi kiasi gani,na huyo Mbunge aliyeuziwa ana plan ya kuzalisha kiasi gani?na kulipa Kodi kiasi gani?
Umeuliza maswali ambayo majibu yake kila Mtu anayo , ama labda wewe ni mgeni Tanzania au umeamua tu kutusumbua
 
Umetembelea mikoa ya wafugaji umeona kulivo kukame? Unataka tuharibu na mikoa yenye asili ya kilimo kisha tutaishi vipi? Mkuu lazima tubadilike na hakuna mabadiliko yasiyo na maumivu. Mifugo hiyo ipigwe mnada kama wanaweza watanunua wao wenyewe na wasipoheshimu sheria watanyang'anywa tena. Mazingira lazima tuyalinde kwa nguvu zote kwa kuwa hayo ni muhimu kwa wanadamu na viumbe wengine.
We jamaa una dhambi sana !
 
Back
Top Bottom