Uchaguzi 2020 Mbeya: Joseph Mbilinyi(Sugu) akamatwa na Polisi wakati akichukua fomu ya Uteuzi

Uchaguzi 2020 Mbeya: Joseph Mbilinyi(Sugu) akamatwa na Polisi wakati akichukua fomu ya Uteuzi

Lakini polisi walivyokuwa wamewapa nafasi tangu Tundu Lissu amerudi, mliwasifu sana sasa mnawachokoza tena?

Richard ungekuwa ni timu, basi ungekuwa umeshuka daraja kwenye ujengaji wa hoja. Kusifiwa sio sifa ya kudumu. Ni sawa na mkulima kuisifia mvua iliyonyesha vizuri mpaka akapata mavuno ya kutosha. Siku hiyo mvua ikinyesha na kuleta mafuriko, usitegemee ataendelea kuisifia eti kisa kuna siku aliisifia baada ya kunyesha vyema. Kilichofanya polisi kusifiwa ni kwakuwa walifanya kazi kwa weledi, kinyume na tabia yao ya kunyanyasa wapinzani. Unaposema wanachokozwa unamaanisha nini? Au unaamini kwakuwa wao ni vyombo vya dola, basi wako juu ya sheria, na kitendo chochote cha kuwataka wafuate sheria ni kuwachokoza! Nyie ndio mnaomini kuwa polisi mara zote huwa sahihi, hivyo kumdhalilisha mtu ni sawa.
 
Kilichomletea matatizo mkusanyiko sio uchukuaji wa form.
Wewe ungekua ndo RPC wa Mbeya, huo mkusanyiko ungekuletea shida gani??? Umeshaona sehemu zingine wachukuuaji form na hata watafutaji wadhamini mikusanyiko ipo, kuna hata sisimizi tumeshasikia kakanyagwa kutokana na hiyo mikusanyiko??? Kwanini wakati mwingine wasiache ili kusubiri wapate sababu ya kuzuia au kukamata, kuliko kumkamata mtu akiwa anachukua form na hata huo mkusanyiko haujajulikana utafanya nini kibaya??? Nadhani kama ungekua wewe ndo RPC usingefanya hivyo.
 
Mkusanyiko siku zote unaambiwa watawanyike kabla nguvu za Dola hazijatumika.... Na sio kumkamata mmoja tu. Wangekamata wote walio kusanyika waone nguvu ya umma.


Hapo wamekosea Sana... Matumizi mabaya ya nguvu kuliko akili..
Somo hapo ata ukichukua umati kama sehemu ya ulinzi kama Lissu anavyopendekeza jamaa wakija wanaondoka na mgombea kirahisi tu.

Busara ni kwenda mwenyewe na kutowapa sababu za kwenda kubebwa mgombea.
 
Hivi mtu anashindwa kwenda kuchukua form zake taratibu aondoke mpaka akusanye watu kibao aende nao?
hapana polisi wamekosea hapa,huyu mtu atashinda kwa kura za huruma, halafu huu ni msimu wa siasa mbwembwe kama hizo zitakuwepo tu ndo maana lisu anabweka ovyo huko njiani kwenye lami iliyotengenezwa na serikai ya CCM, juzi lipumba amepokelewa kapita kweny flyover waachwe tu tutamalizana nao kwenye sanduku la kura, namna hii si vema.
 
Richard ungekuwa ni timu, basi ungekuwa umeshuka daraja kwenye ujengaji wa hoja. Kusifiwa sio sifa ya kudumu. Ni sawa na mkulima kuisifia mvua iliyonyesha vizuri mpaka akapata mavuno ya kutosha. Siku hiyo mvua ikinyesha na kuleta mafuriko, usitegemee ataendelea kuisifia eti kisa kuna siku aliisifia baada ya kunyesha vyema. Kilichofanya polisi kusifiwa ni kwakuwa walifanya kazi kwa weledi, kinyume na tabia yao ya kunyanyasa wapinzani. Unaposema wanachokozwa unamaanisha nini? Au unaamini kwakuwa wao ni vyombo vya dola, basi wako juu ya sheria, na kitendo chochote cha kuwataka wafuate sheria ni kuwachokoza! Nyie ndio mnaomini kuwa polisi mara zote huwa sahihi, hivyo kumdhalilisha mtu ni sawa.
Kwa nini ameenda na maandamano?? Hilo ndiyo kosa lake hayo mengine ni ubuyu tu!
 
Hivi mtu anashindwa kwenda kuchukua form zake taratibu aondoke mpaka akusanye watu kibao aende nao?

Hao watu wamekuja wenyewe hawajalazimishwa....
Polisi walipaswa kuwaambia watawanyike kwa Amani na sio kutumia nguvu ya kumkamata mh. Sugu..

Hadi hapo wameshaharibu subiri tuone wengine watakavyochukua fomu na wakati wa kuzirudisha...


Yajayo yanasikitisha...
 
Polisi wako makini kuwakamata wabunge wa Chadema pekee, wale wahuni waliochoma ofisi za Chadema Arusha Mjini mpaka muda huu bado sijasikia taarifa yoyote toka jeshi la polisi.

Hii ni aibu kwa jeshi la polisi Tanzania.
Wacha kukufuru kama sisi tuna jeshi la polisi nchi zilizo endelea wao watakua nini
 
Wewe ungekua ndo RPC wa Mbeya, huo mkusanyiko ungekuletea shida gani??? Umeshaona sehemu zingine wachukuuaji form na hata watafutaji wadhamini mikusanyiko ipo, kuna hata sisimizi tumeshasikia kakanyagwa kutokana na hiyo mikusanyiko??? Kwanini wakati mwingine wasiache ili kusubiri wapate sababu ya kuzuia au kukamata, kuliko kumkamata mtu akiwa anachukua form na hata huo mkusanyiko haujajulikana utafanya nini kibaya??? Nadhani kama ungekua wewe ndo RPC usingefanya hivyo.
Kasome ‘police force and auxiliary services act 2002’ mkusanyiko usiokuwa na kibali ni kosa la kisheria.

Nachokubaliana na wewe vitu vingine polisi wanatakiwa kutumia busara.
 
Jee kuna sheria gani au katiba gani inayozuia musitembee zaidi ya watu 4 barabarani
NEC imeshaeleza utaratibu wa kwenda kuchukua fomu! Anadanganywa na Lissu wakati yeye hakwenda na maandamano Dodoma kuchukua fomu.
 
Somo hapo ata ukichukua umati kama sehemu ya ulinzi kama Lissu anavyopendekeza jamaa wakija wanaondoka na mgombea kirahisi tu.

Busara ni kwenda mwenyewe na kutowapa sababu za kwenda kubebwa mgombea.

Hiyo Ni nidhamu ya UOGA... narudia Tena ushauri wako Ni nidhamu ya UOGA...

Polisi wapo kulinda usalama na sio kuchochea Amani ipotee...

Kwani hao watu wameharibu Nini.. wangeachwa tu waondoke bila kashikashi zozote... Sasa Hilo tukio linafanya siku nyingine nao wajipange kwa mapambano...
 
Sijui wakina Sugu hua wanahangaika na nini aisee?Yaani Mbunge anachukuliwa kirahisi tu afu wananchi wamekaa tu wanacheki fresh tu.

Mimi ningekua Sugu,Mbowe,Lema etc wala nisingehangaika na mambo ya kuwatetea watu wasiojielewa,ni kuwaacha tu wale msoto mpk wakome siku wakipata akili wataamua hatma ya maisha yao.
 
hapana polisi wamekosea hapa,huyu mtu atashinda kwa kura za huruma, halafu huu ni msimu wa siasa mbwembwe kama hizo zitakuwepo tu ndo maana lisu anabweka ovyo huko njiani kwenye lami iliyotengenezwa na serikai ya CCM, juzi lipumba amepokelewa kapita kweny flyover waachwe tu tutamalizana nao kwenye sanduku la kura, namna hii si vema.
Ukiwa ccm unakua mshamba wa kupindukia.......

Ungefanikia kutembelea nchi zingine ungeelewa maana ya flyover lkn kwa sababu ya ulimbukeni wenu kuanzia kwa mwenyekiti wenu anayewaaminisha kua kutosafiri nje ni uzalendo ndo mmekua km marehemu wanaotembea....

Hizo barabara hata wakoloni walijenga tena walijenha barabara imara sio hizi zenu za hovyo na za kifisadi mnafuja kodi zetu.......
 
hapana polisi wamekosea hapa,huyu mtu atashinda kwa kura za huruma, halafu huu ni msimu wa siasa mbwembwe kama hizo zitakuwepo tu ndo maana lisu anabweka ovyo huko njiani kwenye lami iliyotengenezwa na serikai ya CCM, juzi lipumba amepokelewa kapita kweny flyover waachwe tu tutamalizana nao kwenye sanduku la kura, namna hii si vema.
Wambie. Siasa zimezuiwa miaka 5, leo hata kwenda kuchukua form rafiki zako waliokumis kwa muda wote huo wanakusindikiza imekua nongwa!!!?? Siasa isiyo na wafuasi ni siasa gani hiyo???
 
Polisi wako makini kuwakamata wabunge wa Chadema pekee, wale wahuni waliochoma ofisi za Chadema Arusha Mjini mpaka muda huu bado sijasikia taarifa yoyote toka jeshi la polisi.

Hii ni aibu kwa jeshi la polisi Tanzania.
Ahahahahahahh! Nilifikiri uko njiani kuelekea Mbeya Mjini. Ahahahahahahh!
 
Back
Top Bottom