Mbeya na Kanda ya Ziwa ziwe semi-autonomous kama Zanzibar!

Mbeya na Kanda ya Ziwa ziwe semi-autonomous kama Zanzibar!

Yani mtu yuko katavi au kagera huko..eti aje hospital ya taifa muhimbili..kwanini kusiwepo hospitali ya taifa mikoa kama mwanza..mbeya arusha.

Y dsm only...hii sio sawa.

Vyuo vikuu vimejaa dsm tu...hii sio sawa.

Miundombinu mizuri ni dsm tu..hii sio sawa kabisa.

Kwengine hakuna watu ama..better kujitafutia serikali za majimbo..kila ukanda ufaidike na rasilmali zake.

#MaendeleoHayanaChama

#MaendeleoHayanaChama
huu mdahalo ni mzuri sana aisee yaani kama ndio ungeanzishwa uzi special watu wangechangia sana

ki ukweli kabisa Dar inatunyonya, na wanaamua kupeleka maendeleo dar kwasababu tu waheshimiwa wengi wanaishi pale,

hapo ndio ukitaka kujua kwamba viongozi wetu hawana uzalendo maana wanajiangalia wao tu bas na si watanzania
 
Inakoelekea bora kila kanda iwe Nchi huru.Haiwezekani kanda kama ya ziwa inachangia pato la taifa kubwa sana lakini kanda hiyo maendeleo yake ni kama enzi za ujima .Viongozi wanatapanya pesa wanavyojisikia.Migodi tu kama GGM,NorthMara.Buzwagi.Williamson diamond ingetosha kuibadilisha kimaendeleo hiyo kanda.

Sent using Jamii Forums mobile app
bonge la point babu

lakini chakuskitisha mapato yake yanaenda kuijenga Dar
 
Ni muhimu sana kwani kila nikiangalia naona Mkoa wa Mbeya na wenyeji wa Mkoa huo pamoja na Kanda ya Ziwa wanapaswa kuwa kama Zanzibar ndani ya Tanzania, naamini kabisa Mbeya kama vile Kanda ya Ziwa watapata maendeleo makubwa sana kama wakiachwa wajitawale wenyewe kama vile Zanzibar.

Watu wa Mbeya na Kanda ya Ziwa wana potential kubwa sana ambayo haitumiki na Mikoa yao hasa Mbeya ni kama imesahaulika, ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
Muandishi kwanza unatakiwa kutofautishs kanda ya ziwa na Mbeya.
Mkoa wa Mwanza pekee ni mkubwa kwa hadhi kuliko Mbeya ila haujaomba 'kujitawala' kama Zenji.

Kanda ya Ziwa ina Mwanza, Geita, Simiyu, Mara, Shinyanga na Kagera (hii ni mikoa 5) unapojenga hoja kufanya mkoa mmoja uwe na hadhi kama mikoa 5, bila shaka inathibitisha namna gani huijui vya kutosha kanda ya Ziwa.

Ikitokea Mbeya imetembelewa mara kwa mara na Mkulu, nini kitaongezeka?
Ikitokea Mbeya imejitenga kwa kuwa na hadhi ya Rais wa Mbeya kama Zenji, itapata nini cha kuifanya ikue?

Mkoa unaweza kukua kwa kutegemea ridhaa ya Rais wa nchi au shughuli za wananchi kuzalisha kwa tija na ufanisi wa hali juu ili kukuza uchumi wa eneo?

Pengine ntakubaliana nawe kama RC alieopo sio mzuri kwa lobbying na anategemea mamlaka ya uteuzi ifanye kila kitu, basi Mbeya kama ilivyo mikoa mingine itasubiri sana.

Kuna shida kubwa toka enzi ya Mwl. JKN, ukuu wa mkoa na sekretariet ya mkoa inakuwa na watendaji wasio wazawa na ina faida ya kutokukuza ukanda, na ina hasara kwa kuwa na watu ambao wanafanya business as usual na wanaweza wasiwe creative na innovative kukuza uchumi wa eneo husika kwa msingi wa kutowajibika kwa wananchi moja kwa moja.
Wengi hujuiona wajubu wao ni kumpendezesha mkulu wa Magogoni/Chamwino.

Kwa kuwa hoja ya Mbeya kupewa hadhi kama ya Zenji ni kama haiwezekani kutokea, fikiria mbadala ya nini kifanyike ili uchumi wa Mbeya ukue, mzunguko wa fedha uwepo kwa watu kufanya biashara na kuwa na fedha za kumudu mahitaji yao.
Purchasing power matters bila kujali mtu yuko Mbeya au penginepo.

Nini kifanyike ili watu wengi wa Mbeya wakuze uchumi wao na hata imvutie Mkulu mara kwa mara awe anatia mguu kuzindua miradi ya uwekezaji Mbeya, hilo kaweza kufanyika haraka pasi kutaka kuipa Mbeya hadhi ya Zenjibar.

Jpili njema.

FAM
 
Yaani sijui Katavi wasemeje maana hata lami yakuunganisha mkoa na mikoa mwingine, mpaka leo wanahangaika na bumbi, yaani unaweza ukawa unasafiri utazani unaenda nchi nyingine unashitukia umeibukia kwenye nyumba za watu, wakati wali unaoliwa Dar unatoka huko, kadarisalamu kapo kama kitongoji cha Mpanda.
 
Ni muhimu sana kwani kila nikiangalia naona Mkoa wa Mbeya na wenyeji wa Mkoa huo pamoja na Kanda ya Ziwa wanapaswa kuwa kama Zanzibar ndani ya Tanzania, naamini kabisa Mbeya kama vile Kanda ya Ziwa watapata maendeleo makubwa sana kama wakiachwa wajitawale wenyewe kama vile Zanzibar.

Watu wa Mbeya na Kanda ya Ziwa wana potential kubwa sana ambayo haitumiki na Mikoa yao hasa Mbeya ni kama imesahaulika, ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
Tulisemaga siku nyingi kuwa sukuma gang ni hatari sana kwa ustawi wa nchi hii. Nia yao ni kumega Kanda ya Ziwa, kwa aibu wanaanza kuingiza Mbeya kuficha nia yao ovu.
 
ni kweli kabisa ulichoongea,

yaani serikali hii ina mikoa yake, ipo mikoa mingi ambayo ina fursa nyingi sana za kiuchumi lakini chakuskitisha mapato yanayopatikana yanatumika kuijenga Dar & Dodoma

sasa hiyo si sahihi kabisa, serikali inapaswa kuliangalia hili kwa jicho la tatu

sasa hivi miradi yote ya maendeleo inafanywa Dar & Dodoma

Mikoani huku hakuna kinachoendelea
Dodoma yenyewe watu wake ni kina matonya [emoji23]
 
Ni muhimu sana kwani kila nikiangalia naona Mkoa wa Mbeya na wenyeji wa Mkoa huo pamoja na Kanda ya Ziwa wanapaswa kuwa kama Zanzibar ndani ya Tanzania, naamini kabisa Mbeya kama vile Kanda ya Ziwa watapata maendeleo makubwa sana kama wakiachwa wajitawale wenyewe kama vile Zanzibar.

Watu wa Mbeya na Kanda ya Ziwa wana potential kubwa sana ambayo haitumiki na Mikoa yao hasa Mbeya ni kama imesahaulika, ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
Kuna watu unataka wafe njaa!
 
Mmeanza kushtuka.
Hapo kwenye mbeya futa weka Kanda ya nyanda za juu kusini(sijui ndio huwa inaitwa hivyo) usifananishe mkoa na Kanda nzima
 
Ni muhimu sana kwani kila nikiangalia naona Mkoa wa Mbeya na wenyeji wa Mkoa huo pamoja na Kanda ya Ziwa wanapaswa kuwa kama Zanzibar ndani ya Tanzania, naamini kabisa Mbeya kama vile Kanda ya Ziwa watapata maendeleo makubwa sana kama wakiachwa wajitawale wenyewe kama vile Zanzibar.

Watu wa Mbeya na Kanda ya Ziwa wana potential kubwa sana ambayo haitumiki na Mikoa yao hasa Mbeya ni kama imesahaulika, ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
Niliweka mada ya kuuliza utaratibu wa mikoa kujitenga Moderator akaifuta.

Katiba inatakiwa kuelekeza utaratibu wa mikoa kujitenga kama wananchi wakidhamiria.
 
Ni muhimu sana kwani kila nikiangalia naona Mkoa wa Mbeya na wenyeji wa Mkoa huo pamoja na Kanda ya Ziwa wanapaswa kuwa kama Zanzibar ndani ya Tanzania, naamini kabisa Mbeya kama vile Kanda ya Ziwa watapata maendeleo makubwa sana kama wakiachwa wajitawale wenyewe kama vile Zanzibar.

Watu wa Mbeya na Kanda ya Ziwa wana potential kubwa sana ambayo haitumiki na Mikoa yao hasa Mbeya ni kama imesahaulika, ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
Huna akili! Rudi kwenu Burundi
 
Ni muhimu sana kwani kila nikiangalia naona Mkoa wa Mbeya na wenyeji wa Mkoa huo pamoja na Kanda ya Ziwa wanapaswa kuwa kama Zanzibar ndani ya Tanzania, naamini kabisa Mbeya kama vile Kanda ya Ziwa watapata maendeleo makubwa sana kama wakiachwa wajitawale wenyewe kama vile Zanzibar.

Watu wa Mbeya na Kanda ya Ziwa wana potential kubwa sana ambayo haitumiki na Mikoa yao hasa Mbeya ni kama imesahaulika, ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
Mbeya ipi unayosema wewe???
 
Hilo jambo haliwezekana,ila naungana na wale wanaosema Tanzania itengenezwe kimajimbo. Ili rasilimali za maeneo hayo zianze kunufaisha Hilo eneo. Hii pia pia itachochea maendeleo kwenye maeneo yasiyo na rasilimali za kutosha.
Chadema walipokuwa wanahubiri haya mliwashutumu kuwa wao ni Wakabila na Wabinafsi,sasa akili zinaanza kuwaingia.
 
ni lini Raisi wa Tanzania aliwahi kufika Mbeya mara ya mwisho ?
'Mbea' mnao Homera, Silinde na Tulia (to mention the few). Msipowasikiliza hao, hata mtu afufuke katika wafu, hatawasaidia kitu...


Screenshot_20220529-111211.jpg
 
Kanda ya ziwa nadhani ilipawa kujitenga kabisa..mji mkuu iwe mwanza pale.

Kanda ya ziwa inaipa utajiri mkubwa serikali ya ccm ila maendeleo yote wanajaza mifukoni mwao na dsm tu...hii sio sawa kabisa.

Chamsingi hapa ni kupambana nia kanda zetu tu..cvm imeshindwa jukumu lake at first.

Tuende na serikali ya majimbo la hizi kanda zione namna gani vipi.

Live long NyanzaNation.

#MaendeleoHayanaChama
Tuanze mchakato na hili ni swala muhimu sana .
 
Niliweka mada ya kuuliza utaratibu wa mikoa kujitenga Moderator akaifuta.

Katiba inatakiwa kuelekeza utaratibu wa mikoa kujitenga kama wananchi wakidhamiria.
Mkoa ukishajitena, wilaya zitajitenga na mkoa pia, tutakuwa na nchi inaitwa kigamboni, au Jamhuri ya watu wa Kibaha,
 
Zanzibar yenyewe wanategemea bara kwa chakula.

Kujitenga hakuleti maendeleo ndio maana huko level nyingine tuna regional intergrations. Kama Saddc, Eac , Au etc maana hakuna kilicho kamilika hapa Duniani.
 
Back
Top Bottom