Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

ulisema ulikuta mbinguni wanaimba je ilitumika lugha gani huko..?
Mtu awapo katika Ulimwengu wa Roho hakuna limit juu ya uelewa wa lugha.

Limits zipo uwapo katika Mwili. Mtu aliyejazwa Roho mtakatifu anaweza kuongea Kwa kijerumani, kichina, kiarabunj bila kuzisomea darasani. Au akaongea lugha za Malaika na za Mbinguni bila kufundishwa sababu Roho ya mtu asili yake ni MBINGUNI.

Mtu aliyepagawa na Pepo anaweza kuongea kiarabu au kiswahili bila kusomea, na Kila siku tunashuhudia wakiongea. Lakini ukimwambia kuwa mtu aweza enda Mbinguni na kuongea lugha za Mbinguni au akajazwa Roho mtakatifu na kusema lugha za Malaika watabisha.

Ni ngumu mtu wa mwilini chini na mtu wa Rohoni Kutoka JUU kuelewana.
 
Shalom Mtumishi wa Mungu!

Binafsi ni Mkristo, ninayeabudu kwenye Kanisa lolote lile pale Moyo wangu ukijiskia Amani kwalo.

Kama Mkristo ambaye namwabudu Mungu, naamini juu ya Mwanae Yesu Kristo, na kama Mkristo ambaye nasoma Biblia, kufunga na Kuomba, ili kuwa karibu na Mungu, na kwa Mkristo yoyote yule aliye hai ndoto yake baada ya Maisha haya ni kwenda Mbinguni kwa Mungu Baba!

Tunasoma Biblia kwa uchache inagusia kuhusu Maisha ya Mbinguni, tumekua na Nadharia nyingi na watu kutaka kufahamu kuhusu Mwonekano, Mazingira ya huko Mbinguni japo watu kujaribu kupata picha kukoje, ila mara nyingi ni kuwa lazima Maisha yako yaishe kwa Wema hapa Duniani ili upate nafasi kufika huko!

Nina furahi kusikia kwamba Mtoa post umefika huko kupitia Ulimwengu wa roho!

Nina maswali machache nataka kukuuliza!

Nitaanza na Maswali, umesema ulipofika Mbinguni ulikuta Watu wanaimba Wimbo ambao pia naupenda sana " Mungu wangu, nashangaa Kabisa........!"

1. Je! Huo wimbo ulikua unaimbwa kwa Lugha gani!?

2. Wewe na Malaika mlikua mnaongea Lugha gani!?

3. Malaika kwa Mwonekano alikua wa Rangi gani!? (Mwafrika, Mzungu, Mchina).

4. Hao watu uliowakuta huko Mbinguni mkiimba wote, walikua katika Mwonekano wa jamii moja, Rangi moja, ama Races mchanganyiko kama tulivyo Duniani!?

5. Katika hao watu huko Mbinguni kulikua na Wazee, Vijana na Watoto ama wote walikua katika rika moja?

Asante Mtumishi, ni katika tu kujifunza.
1. Lugha ya Wimbo. Kiswahili Bwana Mungu nashangaa kabisa. Ulimwengu wa Roho hauna limitation ya Lugha na ndio maana mitume walisikika wakiongea Lugha mbalimbali kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume ile sura ya Pili.

2. Aliniongelesha kiswahili kama nikivyoeleza hapo juu. Aliniambia, nimetumwa kukuchukua.

3. Malaika alikuwa na sura ya muonekano wa kibinadamu huku sura yake ikingaa sana kama mwanga wa jua.

4. Walikuwa wanangaa kwa nuru kwenye nyuso zao na huwezi tofautisha race zao huku wamevaa mavazi meupe na yanayong'ara. Wote walikuwa ni wa rika moja vijana wasio wanene wala wembamba na wanaonekana kama vijana wenye umri kati ya 20-30.

Nawasilisha.
 
Mtu awapo katika Ulimwengu wa Roho hakuna limit juu ya uelewa wa lugha.

Limits zipo uwapo katika Mwili. Mtu aliyejazwa Roho mtakatifu anaweza kuongea Kwa kijerumani, kichina, kiarabunj bila kuzisomea darasani. Au akaongea lugha za Malaika na za Mbinguni bila kufundishwa sababu Roho ya mtu asili yake ni MBINGUNI.

Mtu aliyepagawa na Pepo anaweza kuongea kiarabu au kiswahili bila kusomea, na Kila siku tunashuhudia wakiongea. Lakini ukimwambia kuwa mtu aweza enda Mbinguni na kuongea lugha za Mbinguni au akajazwa Roho mtakatifu na kusema lugha za Malaika watabisha.

Ni ngumu mtu wa mwilini chini na mtu wa Rohoni Kutoka JUU kuelewana.
Amina ubarikiwe Mjoli wa Bwana.
 
Kama akili yako imesalimika bila kuchafuliwa na fikra za wana falsafa na wapuuzi wengine basi hata wewe mwenyewe ukijitizama ni ishara tosha kuwa yupo aliyekuumba, mambo ya moto ni imani ya juu sana jitizame tu kwenye kioo ni ishara tosha.

Kwahyo huu ulimwengu, mvua kunyesha, upepo, bahari kupwa na kujaa, watu kuwa matajiri wengine maskini, wengine kulia machozi wengine kucheka, wengine kufa wengine kuzaliwa, wengine kuishi maisha marefu wengine kufa mapema, mambo yote haya anayafanya putin sio?.
Na hayo uliyo orodhesha hapo ndio Yana dhibitisha hakuna Mungu muweza wa vyote. Angelikuepo hayo yasinge tokea
 
Na hayo uliyo orodhesha hapo ndio Yana dhibitisha hakuna Mungu muweza wa vyote. Angelikuepo hayo yasinge tokea
Kwamba ili awepo ni mpaka aendane na akili yako, kwani ulipokuwa unazaliwa uliambiwa hapa ni peponi mkuu? lazima usote na mara nyingine uneemeke.
 
Kwamba ili awepo ni mpaka aendane na akili yako, kwani ulipokuwa unazaliwa uliambiwa hapa ni peponi mkuu? lazima usote na mara nyingine uneemeke.
Mungu hayupo ndio maana Kuna mateso chuki njaa Vita na mengine mengi Ange kuepo hivyo visinge wezekana. Au labda alishakufa ndio maana Mambo yanaenda randamli
 
Mungu hayupo ndio maana Kuna mateso chuki njaa Vita na mengine mengi Ange kuepo hivyo visinge wezekana. Au labda alishakufa ndio maana Mambo yanaenda randamli
"Hapana shaka tutakujaribuni kwa kitu katika khofu, na njaa, na upungufu wa mali na watu na matunda, na wape bishara njema wanaofanya subra."

Qur'an 2:155
 
"Hapana shaka tutakujaribuni kwa kitu katika khofu, na njaa, na upungufu wa mali na watu na matunda, na wape bishara njema wanaofanya subra."

Qur'an 2:155
Ili kua mfuasi wa hizi Imani inabidi uwe mjinga sana. Sasa mnasema Mungu Ni mjuzi wa yote, Ina maana matokeo ya jaribu teyari anayo. Sasa anakujaribu ili agundue nini? Maana kwa uwezo wake tayari ameshajua matokeo kabla ya mtihani
 
Mbinguni ni wazo lipo kichwani tu, hakuna uhalisia. Ukipata raha ni mbinguni na ukipata shida upo motoni. Ni maisha tu ya hapa duniani, ukifa ndio kupotea tu kama inzi.
 
Nimeona watu wengi humu JF wakimponda na kumkashfu Mwalimu Mwakasege baada ya kusema Mungu alimfunulia kuhusu mbingu na kwenda Mbinguni.

Binafsi nadeclare interest kuwa ninatumika Kanisa la TAG kama Mzee wa Kanisa huku Nyanda za juu kusini pia ni Mtumishi wa Serikali na huwa nahubiri mara moja moja. Siandiki hivi kwa kufurahisha watu au kujisifu wala kutaka kumsafisha Mwalimu Mwakasege ila naeleza kile nilichoshuhudia na kile ambacho Mungu amenitendea.

Kwa umri na muda niliomtumikia Mungu kama Mkristo nafahamu Mungu anajifunua kwa watu wengi yeye binafsi na pia kuwafunulia kuhusu wengi kuhusu mbingu.

Binafsi, nashuhudia leo na kikiwa na akili timamu na dhamira njema Moyoni mwangu kuwa nimemuona mwenye haki "Yesu Kristo" si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na amenitokea kwa namna mbalimbali tofauti na watu wanavyokashfu kuwa tutatokewa na Mapepo yaliyovaa sura ya "Bryan Deacon" yule aliyeigiza "Filamu ya Yesu" Pia nashuhudia, Mungu kunifunulia na kuiona mbingu.

Mafunuo haya ya kutokewa na Yesu kwangu mimi hayakuwa kwa jinsi ya kimwili "yaani kunitokea physically" ila ni katika ndoto na Maono ya usiku pia wakati nasali nikajiona tu nimekutana naye.

Leo sitaelezea kuhusu kutokewa na Yesu ila nitaelezea kuhusu ushuhuda wangu wa kuiona Mbingu ila nasisitiza katika hilo, kila maono, ndoto au mafunuo ya Kimungu yanajengwa chini ya Neno la Mungu. Neno: Ayubu 33:14-16 hapa Mungu anasema kuhusu kusema na wanadamu kuhusu ndoto ns mqono ya usiku.

Neno: Yoel 2: 28-29 Anasema kuhusu "Ndoto na Maono".

Kuhusu Mungu kuwafunulia watumishi wake mbingu, tunaona Paulo anasema namna alivyochukuliwa na kuoneshwa kuhusu Mbingu katika 2 Korintho 12: 2-9 pia Stephano naye anafunuliwa katika Matendo ya Mitume 7:56 na pia Mtume Yohana anafunuliwa kuhusu Mbingu wakati anaandika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Binafsi, Nakumbuka ilikuwa 2016. Mungu alinipa Neno toka Yeremia 33:3 inayosema "Niite nami nitakuitikia na nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua" pia kwa muda mrefu nilikuwa naimba moyoni mwangu wimbo mmoja wa zamani sijui uliimbwa na kwaya gani ila kuna kipande wanaimba " Nimpeleleza nani raha ya Mbingu×2, Yesu ndiye wa Kumpeleleza"

Nakumbuka Siku hiyo niliamka kama kawaida saa 9 alfajiri na kusali. Ilipofika saa 11:45 nikasema nilale kidogo ili nikiamka saa 1 hivi niende kazini. Nilipolala kama saa 12 alfajiri nikaona Malaika mmoja aliye kama mwanadamu amevaa mavazi meupe yenye kung'ara huku akiwa mwenye sura inayong'ara ananiambia "nimetumwa nikufuate". Akanishika mkono, nikaona natoka kwenye mwili upande wenye moyo.

Nikapita kwenye bati la nyumba bila kizuizi. Safari ya kupanda juu ikaanza kwa speed ya ajabu huku akiwa amenishika Mkono. Nikaangalia chini na kuona mwili wangu, mke na mtoto wangu wamelala kitandani. Unaona nyumba na miti ya duniani. Tukapaa juu kwa spidi nikaangalia chini tena na kuona kadunia kalivyo kadogo then tukafika katika nchi ile ambayo "watu" wanaimba na kumuabudu Mungu. Nikaungana nao tuliimba "Bwana Mungu nashangaa kabisa"

Sijui nielezeje muonekano wake nchi ile ila ni nzuri na ya meta meta. Hali ya hewa na mazingira ni tofauti na huku duniani. Nchi ile ni kweli na mji ule ni kweli. Jitahidi usikose kuingia mji ule.

Baadaye nikaambiwa turudi na kwa speed ya ajabu, najikuta naingia mwilini mwangu upande wa kushoto kwenye moyo, mwili ukawa kama umepigwa "shot" nikashtuka.

Binafsi, nimewasikia na kuwaona watumishi wengi wa Mungu wanaoshuhudia kuhusu Mbingu huku kwetu na sehemu myingine. Ukiacha hao maarufu, japo "Zumaridi hapana kwani inaonekana ana shida ya akili" Ukiacha Mwakasege, hata Marehemu Kulola alishashuhudia siku moja kufunuliwa kuhusu Mbingu.

Nami nimeona nishare uzoefu wangu kuhusu Mafunuo ya Mbingu. Siku nyingine nitaeleza kuhusu kutokewa na Yesu ana tutokeaje, yupoje na tunajuaje kama ni Yesu.

Asanteni.
Utukufu kwa BWANA!
 
Hajawahi kunibabaisha kwani najua ana shida gani? Waliopinga uwepo wa Mungu walikuwepo na watakuwepo hadi mwisho wa dahari. Hana mpya na Biblia inawaita "Wapumbavu" kwa umri wangu, hanipati, hanibabaishi, haniyumbishi wala hanipotezei muda wangu kujibizana naye kuhusu uwepo wa Mungu kwani macho yangu yameshuhudia mengi yanayothibitisha pasi na shaka uwepo wa Mungu na wala sina mashaka naye. Najua alikuwepo, yupo na atakuwepo milele na milele. Poleni kwa huo "Upumbavu" uliowajaa ila samahani kwa hilo mkuu.
"Kigogo" mmoja (simkumbuki jina) aliazimia kuziteketeza Biblia zote, kipindi hicho kabla teknolojia ya uchapaji haijagunduliwa. Lakini alikufa akaziacha Biblia zikiwa "hai", na baadaye nyumba yake iligeuzwa kuwa kiwanda cha kuchapia Biblia.
 
Amen kuubwa mimi naamini haya hata kama nitabaki peke yangu nitaamini tu. Japo mi ni mwenye dhambi BWANA UNIREHEMU BWANA UNIREHEMU kuna dhambi moja inanitesa sn ninashindwa kuiacha kbs bt sku nikfanikiwa takuwa mwenye nguvu sn ulimwengu wa roho.
 
Bro tuna mambo genuine ya kufikiria. Peleka mazingaombwe yako shule ya maingi huko. Tuache tuishi uhalisia
Mungu wa mbinguni yupo na ataendelea kuwepo na kujifunua kwa watu wake kwa namna na jinsi impendezavyo. Pia kuamini au kutoamini kwangu juu ya uwepo wake hakumfanyi Mungu kutokuwepo maana yeye haitaji uthibitisho wa mwanadamu ili ajulikane yupo. Yeye ni wa milele na ataendelea kuwepo. Mwana kondoo ameshinda tumfuate.
 
Nimeona watu wengi humu JF wakimponda na kumkashfu Mwalimu Mwakasege baada ya kusema Mungu alimfunulia kuhusu mbingu na kwenda Mbinguni.

Binafsi nadeclare interest kuwa ninatumika Kanisa la TAG kama Mzee wa Kanisa huku Nyanda za juu kusini pia ni Mtumishi wa Serikali na huwa nahubiri mara moja moja. Siandiki hivi kwa kufurahisha watu au kujisifu wala kutaka kumsafisha Mwalimu Mwakasege ila naeleza kile nilichoshuhudia na kile ambacho Mungu amenitendea.

Kwa umri na muda niliomtumikia Mungu kama Mkristo nafahamu Mungu anajifunua kwa watu wengi yeye binafsi na pia kuwafunulia kuhusu wengi kuhusu mbingu.

Binafsi, nashuhudia leo na kikiwa na akili timamu na dhamira njema Moyoni mwangu kuwa nimemuona mwenye haki "Yesu Kristo" si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na amenitokea kwa namna mbalimbali tofauti na watu wanavyokashfu kuwa tutatokewa na Mapepo yaliyovaa sura ya "Bryan Deacon" yule aliyeigiza "Filamu ya Yesu" Pia nashuhudia, Mungu kunifunulia na kuiona mbingu.

Mafunuo haya ya kutokewa na Yesu kwangu mimi hayakuwa kwa jinsi ya kimwili "yaani kunitokea physically" ila ni katika ndoto na Maono ya usiku pia wakati nasali nikajiona tu nimekutana naye.

Leo sitaelezea kuhusu kutokewa na Yesu ila nitaelezea kuhusu ushuhuda wangu wa kuiona Mbingu ila nasisitiza katika hilo, kila maono, ndoto au mafunuo ya Kimungu yanajengwa chini ya Neno la Mungu. Neno: Ayubu 33:14-16 hapa Mungu anasema kuhusu kusema na wanadamu kuhusu ndoto ns mqono ya usiku.

Neno: Yoel 2: 28-29 Anasema kuhusu "Ndoto na Maono".

Kuhusu Mungu kuwafunulia watumishi wake mbingu, tunaona Paulo anasema namna alivyochukuliwa na kuoneshwa kuhusu Mbingu katika 2 Korintho 12: 2-9 pia Stephano naye anafunuliwa katika Matendo ya Mitume 7:56 na pia Mtume Yohana anafunuliwa kuhusu Mbingu wakati anaandika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Binafsi, Nakumbuka ilikuwa 2016. Mungu alinipa Neno toka Yeremia 33:3 inayosema "Niite nami nitakuitikia na nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua" pia kwa muda mrefu nilikuwa naimba moyoni mwangu wimbo mmoja wa zamani sijui uliimbwa na kwaya gani ila kuna kipande wanaimba " Nimpeleleza nani raha ya Mbingu×2, Yesu ndiye wa Kumpeleleza"

Nakumbuka Siku hiyo niliamka kama kawaida saa 9 alfajiri na kusali. Ilipofika saa 11:45 nikasema nilale kidogo ili nikiamka saa 1 hivi niende kazini. Nilipolala kama saa 12 alfajiri nikaona Malaika mmoja aliye kama mwanadamu amevaa mavazi meupe yenye kung'ara huku akiwa mwenye sura inayong'ara ananiambia "nimetumwa nikufuate". Akanishika mkono, nikaona natoka kwenye mwili upande wenye moyo.

Nikapita kwenye bati la nyumba bila kizuizi. Safari ya kupanda juu ikaanza kwa speed ya ajabu huku akiwa amenishika Mkono. Nikaangalia chini na kuona mwili wangu, mke na mtoto wangu wamelala kitandani. Unaona nyumba na miti ya duniani. Tukapaa juu kwa spidi nikaangalia chini tena na kuona kadunia kalivyo kadogo then tukafika katika nchi ile ambayo "watu" wanaimba na kumuabudu Mungu. Nikaungana nao tuliimba "Bwana Mungu nashangaa kabisa"

Sijui nielezeje muonekano wake nchi ile ila ni nzuri na ya meta meta. Hali ya hewa na mazingira ni tofauti na huku duniani. Nchi ile ni kweli na mji ule ni kweli. Jitahidi usikose kuingia mji ule.

Baadaye nikaambiwa turudi na kwa speed ya ajabu, najikuta naingia mwilini mwangu upande wa kushoto kwenye moyo, mwili ukawa kama umepigwa "shot" nikashtuka.

Binafsi, nimewasikia na kuwaona watumishi wengi wa Mungu wanaoshuhudia kuhusu Mbingu huku kwetu na sehemu myingine. Ukiacha hao maarufu, japo "Zumaridi hapana kwani inaonekana ana shida ya akili" Ukiacha Mwakasege, hata Marehemu Kulola alishashuhudia siku moja kufunuliwa kuhusu Mbingu.

Nami nimeona nishare uzoefu wangu kuhusu Mafunuo ya Mbingu. Siku nyingine nitaeleza kuhusu kutokewa na Yesu ana tutokeaje, yupoje na tunajuaje kama ni Yesu.

Asanteni.
Hii ilikutokea ndugu mwenye hii Id au ume copy maelezo ya mtu ?
 
Back
Top Bottom