Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Ulivyorahisisha mambo sasa utadhani wewe ndio muumba mwenyewe, katika ukafiri mkubwa ni mtu kupinga jambo la kufufuliwa na huu ni upagani wa wazi, hivi ninyi vichwa vyenu mnavitumia kufanyaje? haufikirii mambo yote yalivyopangwa kwa ustadi wa hali ya juu? hautizami watu wanavyokuja na kuondoka? hauzingatii wengine wanavyodhulumu wenzao?.

Unataraji hayo yatapita burebure? acha kujipa moyo kwenye hamna mkuu, utatumia muda wako na ukifika wakati unaondoka kwenda kulekule walipo wenzako, huko wanaposubiri tukamilike wote kisha siku ya mwisho ifike na hukmu ipite na kila mmoja alipwe kwa kile alichokifanya.

"Wamedai wale waliokufuru ya kwamba hawatofufuliwa, sema: kwanini msifufuliwe!? ninaapa kwa mola wangu! hapana shaka mtafufuliwa na kisha hapana shaka mtaambiwa {yote} mliyoyatenda, na hayo kwa allah ni mepesi".

Qur'an 64:7

Jiandae na kifo chako mkuu, kikifika hicho ndio kiama chako kidogo kisha kufufuliwa ndio kiama chenyewe, na si busara kujipa matumaini kwenye hamna, no where to run.
Inaonekana una amini Mungu kwa sababu umetishiwa moto. Mbali na hayo matisho Mungu ni Hadith ya kufikirika tu. Hayupo hajawai kuwepo na hatokaa awepo
 
Sasa mkuu hapa najiandaa niende kazini kama Mungu ananipenda kwanini asinipe pesa nilale tu?
Na ukizingatia ni kipindi cha mvua usingizi ulivyo ? Yaani "printed piece of paper" ndio inakutoa utu na kumthaminisha Mungu na pesa?

Kwani umulele wamtu ulipangwa nanani?
Hayo simajukum yaalieniumba ndie anaejua alivyoniprogram kuwa Mimi nitakuwa waupandegan
Hapana bro, Mungu ni muaminifu, wa haki, halazimishi na wala sio mkoloni. Yeye amekupa uhuru wa kuchagua nji uipendayo. Amekuumba mwanadamu ukiwa kiumbe kitimilifu na kukipa mamlaka ya kuchagua wapi pa kwenda. Umilele wako unauandaa wewe mwenyewe kwa kuchagua njia uipendayo. Yeye anasema tazama nimeweka njia mbili kwako njia ya uzima na njia ya mauti. Chagua wewe uzima au mauti. Njia ya uzima ni kumuishia yeye katika kicho na utakatifu ila njia ya mauti ni kuishi katika dhambi. Chagua fungu lako sasa bro.
 
Inaonekana una amini Mungu kwa sababu umetishiwa moto. Mbali na hayo matisho Mungu ni Hadith ya kufikirika tu. Hayupo hajawai kuwepo na hatokaa awepo
Wacha weeeeee kizazi cha dotcom
 
Wangapi pia waliwahi kuwaza na kuota kumiliki magari na majumba ya kifahari kisha wakaamka na kukuta wako mikono tupu?
 
Hapana bro, Mungu ni muaminifu, wa haki, halazimishi na wala sio mkoloni. Yeye amekupa uhuru wa kuchagua nji uipendayo. Amekuumba mwanadamu ukiwa kiumbe kitimilifu na kukipa mamlaka ya kuchagua wapi pa kwenda. Umilele wako unauandaa wewe mwenyewe kwa kuchagua njia uipendayo. Yeye anasema tazama nimeweka njia mbili kwako njia ya uzima na njia ya mauti. Chagua wewe uzima au mauti. Njia ya uzima ni kumuishia yeye katika kicho na utakatifu ila njia ya mauti ni kuishi katika dhambi. Chagua fungu lako sasa bro.
Kwaiyo ndugu ili nipate uzima wa milele natakiwa kumsikiliza pastor wangu kwa mfano akinijambia usoni akikojolea maji tunywe akituambia tunyonye matiti yake akituelekeza tufunge mpaka tufe. Na tukikataa tunakua tumechagua mauti?
 
We nenda kwenye uzi wako wa selfie tu kule huku hupawezi sister angu.😀😃😄😁😆
Kanionyeshe nilipocomment kwenye uzi wa selfie.
Kama utachunguza vzr mada kama hizi ndo zinanivutia. Ili nishuhudie mazombie kama nyie mkipelekwapelekwa hovyo.
 
Kanionyeshe nilipocomment kwenye uzi wa selfie.
Kama utachunguza vzr mada kama hizi ndo zinanivutia. Ili nishuhudie mazombie kama nyie mkipelekwapelekwa hovyo.
Sawa sister, kuwa na siku njema.
 
Hallucinations hizo, hata TEJA nae akipuliza BANGI zake akabwia UNGA, nae anafikw ULAYA akapigwa Story na wanamuziki wakubwa tu...then ALOSTO ikishuka anajikuta yupo TANDALE kwa MTOGOLE[emoji1787][emoji1787]
Wacha weeeeeeeeeeee
 
Weewee, hilo ni wenge lako la mafikira yako unayoshinda nayo na kukesha nayo mtaani ndio reflection yake hiyo ukadhani umeenda kweli mbinguni, kwani mbinguni ni juu au chini ya dunia? Hebu nenda tena Leo mchana, Acha kuweweseka na uchovu wa mwili ukadhani umepaa ni upuuzi
Wacha weeeeeeee. Kizazi cha chanjo hiko kwenye ubora wao.😀😃😄😁😆😅
 
Huyo anajiita muinjilist kwanini asiifanye kazi hiyo bure kwa kuwa ni ya Mungu lakini anadai sadaka?

Kwanini asiishi kwa kuvuta hewa tu iliyo ya bure?

Na kwanini wanakamsemo asiyefanua kazi na asile kwahiyo wanakubali kuwa hiyo ni ajira wako kazini wanaingiza kipato watoto waende chooni?
Wacha weeeeeeeeeeeee
 
Nijaaminishwa katika quran au biblia ili kuamini dini za kimapokeo zilizoletwa na wanyonyaji,dhurumati,wezi,nk.

Ni wapi iwe Afrika,Asia,Amerika au Ulaya amewahi kukufuka au kufufuliwa mtu yeyote?

Basi wale wote wanaomfuata yesu au muhamad hasa masheik na wachungaji wangekuwepo waliowahi kufufuka.

Mtu hupaswa kuamini kinachomtokea au kilichowahi kutokea ktk jamii anayoishi siyo VYAKULETEA /KUHADITHIWA.

Yaani mnaoshinda mnasali miskitini na makanisani mmekithiri kwa umaskini hao wanaodai wanapeleka mbunguni ni wanatajirika kwa ujinga wenu.

Ni wapi unapoweza kuwatenganisha au kuwagundua wanaosali na wasiosali kwa kuwaangalia?

Ongezeni na akili zenu
 
Hakuna uthibitisho wa moja kwa moja zaidi ya kuwa ni story za kubumba na kufikirika.

Kiufupi hata mimi huwa naota napaa, ndoto hazina maana yoyote.

Mara nyingi watu wanaota kile wanachokifikiria sana
 
Back
Top Bottom