Mbinu watumiazo Mafundi Ujenzi kuibia mabosi zao

Mbinu watumiazo Mafundi Ujenzi kuibia mabosi zao

Uko vizuri sana Mkuu

Hopefully upo kwenye field ya Ujenzi ama umejenga sana.

Mara ya mwisho nilimwajiri Fundi rangi MMama, she was good at decorating

Shida yake, alikuwa anaenda Dukani nilipolipia rangi, anamwambia Mzabuni boss kasema badala ya rangi Lita 20 nipe Lita 10....


Hiyo 10 inayobaki alikuwa anabeba anapeleka anapopajua mwenyewe 🙌
Wanatia hasara sana unaweza ua mtu, kuna jirani ghorofa lake walimchakachua vibaya mno ile wanajiandaa kumwaga jamvi la kwanza mvua moja tu nalo likapiga chini.......mbona aliwachomolea bastola walipoteana
 
Kuna jamaa alikuwa anafatua tofari,ila kabla ya kwenda kazini alikuwa anachanganya mchanga na sement yote harafu ndio anawaachia mafundi akijua amewakomesha,kumbe wale walikuwa wanachukua mchanga uleule wanapeleka sehemu nyingine
 
Mkuu unaongea kisiasa na uaminifu, yote hayo ya nini?

Hapa tunataka tuelekezane mbinu chafu zinazotumiwa na mafundi kufirisi matajiri zao.

Zungumzia mbinu za upigaji wanazozitumia mafundi ili kuwanusuru wale wenye mipango ya ujenzi ili wapate mbinu za kujisimamia na kuwadhibiti mafundi pindi waanzapo miradi yao ya ujenzi.
Lakini pia mafundi nao wanadhulumiwa kwa namna moja ama nyingine kupitia malipo duni wapewapo kazi na wateja wao! NAni atawatetea labda.
 
Hivi mnawachukuliaje mafendi eti?
Kwa nini msijenge wenyewe ikiwa mafundi si kitu kwenu?
Pole kwa kukwazika mkuu, tena niwie radhi sana isee.

Mjadala uliopo hapa ni kupeana mbinu na uzoefu kwa ajili ya kuzuia wizi ufanywao na mafundi na si kudhalilisha fani ya ufundi hapana.
Kwa hiyo katika maelezo yangu naomba usinitafsiri vibaya.
Hivi mnawachukuliaje mafendi eti?
Kwa nini msijenge wenyewe ikiwa mafundi si kitu kwenu?
 
Njia nyepesi ya kumpata boss mjuaji. Mfano ww ni mpaka rangi, usiwe na haraka. Hakikisha unajenga uteja dukani. Mpange muuzaji kwanza kuhusu huo mchongo.
Mfano zinahitajika ndoo 6 za weather gurd. Andaa ndoo moja tupu safi, ijaze maji then ipeleke pale shop km bosheni. Siku ya kwenda kununua nenda nae boss wako na usiwe na haraka.
Pakia ndoo hizo peleka site, shusha mzigo then rudi shop uchukue chako. Easy like that.
 
usije mwaga ubongo wa mtu tukusome magazetini mbinu ni kusimamia tu kikamilifu, ukubali kupigwa kidogo

Hivi hakuna kampuni zilizosajiliwa rasmi kusimamia shughuli za ujenzi? Hii ni fursa nzuri sana basi tukutoaminiana
Kupigwa ni lazima. Hizi mbinu nyingi wanatumia haswa kwa wanaofanya ujenzi kwa mara ya kwanza. Usikubali kufanya manunuzi maduka anayoshauri fundi. Lakini umakini mkubwa unahitajika kwenye manunuzi ya vifaa vya umeme. Hapa ndiyo unapigwa vibaya. Mimi nililetewa Main Switch ya laki 3 wakati dukani nimelipia Main Switch ya laki 8. Hii nilikuja kugundua baadaye sana baada y kucheki bei ya Main Switc niliyoletewa.
 
Kwenye hii thread tutakuwa tuna share Mbinu za wizi za mafundi ujenzi ili kusaidia wale wanaotaka kujenga "wasipigwe ".

Wengi tumepigwa sana hadi kuzijua hizi mbinu.

Karibuni.
Ngoja niweke Kambi hapa.
 
Njia nyepesi ya kumpata boss mjuaji. Mfano ww ni mpaka rangi, usiwe na haraka. Hakikisha unajenga uteja dukani. Mpange muuzaji kwanza kuhusu huo mchongo.
Mfano zinahitajika ndoo 6 za weather gurd. Andaa ndoo moja tupu safi, ijaze maji then ipeleke pale shop km bosheni. Siku ya kwenda kununua nenda nae boss wako na usiwe na haraka.
Pakia ndoo hizo peleka site, shusha mzigo then rudi shop uchukue chako. Easy like that.
Hakuna baraka, ndiyo maana asilimia kubwa hubaki kwenye level hiyohiyo ya maisha miaka nenda rudi.
 
Njia unayoitumia nami nimewahi kuitumia.

Changamoto yake Fundi aliniagiza Tiles boksi 160, nikamletea boksi 130.

Baadaye Tiles zikafeli hivyo kazi kusimama Kwa muda.

Nikalazimika kufata Tiles boksi 25 Kariakoo na nikatakiwa kusubiri maana sikuweza kupata nilizotumia Mwanzo🙌
Tiles ni rahisi kuhesabu mwenyewe kiasi kinachohitajika kwa kupiga hesabu ya eneo unalotaka kuweka tiles halafu zidisha kama asilimia 8 kwa ajili ya vipande.
 
Nadhani uzi huu utatusaidia kung'amua janja janja wanazofanya mafundi, kwahiyo tutawamudu, juzi nimemuuliza fundi hii kazi itahitaji mifuko mingapi ya sementi, akanambia 25, nikamuuliza Bei ya sementi ipoje, akasema 16 Hadi 16 Mia 5. Nikaamua kwenda mwenyewe dukani bila kumwambia, nimekuta Bei Ni 14 na 15. Sijamwambia chochote, ntamletea sementi na nitamsimamia bampa to bampa, Kwanza ntampelekea mifuko 20 Kwanza. Ila Kuna mdau katoa wazo la kuulizia ratio kwa mafundi wengine ili kujua idadi halisi, nalo Ni Jambo la busara sana
Cement ya elfu 14-15 umeipata wapi mkuu? Inaweza kuwa magendo hiyo. Bei aliyokutajia fundi wako ni sahihi kwa hali ya soko ya sasa.

Kuna umuhimu pia wa kujenga uhusiano mzuri na fundi ambao ndio utakuwa msingi wa uaminifu.
 
Njia unayoitumia nami nimewahi kuitumia.

Changamoto yake Fundi aliniagiza Tiles boksi 160, nikamletea boksi 130.

Baadaye Tiles zikafeli hivyo kazi kusimama Kwa muda.

Nikalazimika kufata Tiles boksi 25 Kariakoo na nikatakiwa kusubiri maana sikuweza kupata nilizotumia Mwanzo[emoji119]
Hii ndiyo shida ya kutoaminiana!

Uzi Mzima hakuna anayeongelea Contract na BoQ wote tunataka mteremko!
Fundi anayejielewa atakwambia muanze na contract ili iwabane wote, Yeye na Wewe! Just a simple contract kwa hawa mafundi wa uswahilini.
Secondly fundi aliyefocus kwenye kazi hata deal na Materials na Management yake hiyo atamwachia Client maana mwisho wa siku anaweza kugeuka Mlinzi wa vifaa na si Fundi tena!
Katika Suala la Ujenzi vitu vya Msingi ni Vitatu, TIME, QUALITY na COST na hivi huwezi kuvifikia mwenyewe pasipo kushirikiana na Fundi!
Finally, kama huna ABCs za mambo ya Ujenzi tafuta mjuzi atakayekushauri na kukupa mwongozo tuachane na hii tabia ya kudhani tunajua kila kitu.
Huku kwenye mitandao mafundi wa kweli ni wachache kuliko matapeli. Reference ya Fundi ni MUHIMU SANA
 
Hii ndiyo shida ya kutoaminiana!

Uzi Mzima hakuna anayeongelea Contract na BoQ wote tunataka mteremko!
Fundi anayejielewa atakwambia muanze na contract ili iwabane wote, Yeye na Wewe! Just a simple contract kwa hawa mafundi wa uswahilini.
Secondly fundi aliyefocus kwenye kazi hata deal na Materials na Management yake hiyo atamwachia Client maana mwisho wa siku anaweza kugeuka Mlinzi wa vifaa na si Fundi tena!
Katika Suala la Ujenzi vitu vya Msingi ni Vitatu, TIME, QUALITY na COST na hivi huwezi kuvifikia mwenyewe pasipo kushirikiana na Fundi!
Finally, kama huna ABCs za mambo ya Ujenzi tafuta mjuzi atakayekushauri na kukupa mwongozo tuachane na hii tabia ya kudhani tunajua kila kitu.
Huku kwenye mitandao mafundi wa kweli ni wachache kuliko matapeli. Reference ya Fundi ni MUHIMU SANA
Umesema sahihi Mkuu

Nadhani ni Wenye nyumba wachache wanaofunga mikataba na Mafundi wao

Mara zote, Mafundi wameonekana sio waaminifu
 
Back
Top Bottom