mjingamimi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2015
- 42,209
- 51,004
mwenzie alikuja kumchukua.wakawa wawili.Ungemsindikiza mzee... mie niliwahi badiri safari juu kwa juu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mwenzie alikuja kumchukua.wakawa wawili.Ungemsindikiza mzee... mie niliwahi badiri safari juu kwa juu
Sawa tunasubiri.Kuanzia jumanne au Kesho nitaanza kushusha nilikuwa..naandka flan hiv..ila mtaniwiwa radhi kama kutakuwa na typ... errors
Saf uncle nimetingwa na majukumu sijasoma miendelezo kadhaa lakini endelea kunitag nitakuwa nasoma wikiendi uncleNambie ndugu.....
Story nzuri sana nilikuwa sijaona tag nimechelewaInaendelea
Rayns mawardat Tiffay Aaliyyah MIRA01 Statics
Baada ya kukusanya taarifa (Information harvesting) nilifanya processing na kuanda roadmap ya kunifikisha katika hitimisho la hili swala kwa kutumia umakini na akili ya hali ya juu.. nilifanyaje?
Ilipita muda kidogo, sikumbuki exactly ni siku ngapi ila ni kati ya mwezi au mwezi na nusu, yule Dada alipona na kurejea kwa Mumewe akiwa na hasira sana, pia Mumewe nae alikuwa na maswali kichwani kuhusu hiyo Mimba iliyotoka na kwanini alifichwa kama anaujauzito. Walienndelea na vikao kadhaa vya kifamilia ili kusuluhisha migogoro yao na lile jambo lisitokee tena. Kuna siku yule Dada alinitafuta kunijulia hali, niliongea nae mambo mengi sana kisha nikamuomba kama hatojali nionane nae.
Nakumbuka ilikuwa weekend aliomba ruhusa kwamba anaenda kwao (Ni maeneo ya Temeke), pia aliomba mumewe amsindikize, na kweli Mume wake waliongozana nae mpaka huko ukweni. Mie nilikuwa tayari nishaplan mishen yangu ya kuonana nae bila kuacha tracing points.
Baada ya kufika walikaa kidogo, Jamaa akaondoka ( Mama wa yule Dada alikuwa bado na kinyongo so jamaa kukaa muda mrefu pale ilikuwa ni ngumu), yule Dada alinitafuta na kuniambia tayari yupo kwao na Mume wake kashaondoka, nimtajie location tukutane.
Nilimwambia atulie kwanza ntamjulisha nilipo ila utaratibu ni ule ule aje kama alivyo asibebe yale niliyomkataza. Kweli na mie nilikuwa nipo sehemu tulivu na Pc yangu nikaingia katika mfumo, nikaona Jamaa yupo kinondoni anaitafuta Morocco nikajua moja kwa moja anaenda kwa Mke wake yule mwingine. basi nilizidi kuwa huru.. kutokana na maelekezo niliyompa yule Dada hakuchukua muda mrefu nae alifika exactly nilipomwambia afike, nilimfata na kuondoka nae lile eneo na kusogea eneo jingine.
Nilimuuliza nyumbani kaagaje? Aliniambia kuwa ameshamweleza Mama yake kila kitu kuhusu Mimi na kipi kinaendelea, maana Mama mtu alimbana aseme ukweli chanzo cha ugomvi pia kuhusu swala la Ujauzito kwanini hata yeye Mama mtu alifichwa? hivyo iliweka mashaka na maswali mengi ambayo ilipelekea kumbana aseme ukweli. Basi mie sikuwa na neno maana najua vifua vya Wanawake kwenye kutunza mambo mazito ni shida sana.
Tulispend muda mwingi kuongea mambo tofauti tofauti, muda huo nawaza naanzaje kumweleza yale niliyoyapanga kumweleza, nilimzuia kutumia alcohol ili awe na akili timamu tukiwa tunaongea, alinishangaa kwanini hiyo siku nimekuwa serious sana. nilimuuliza maswali mengi ila kubwa ni kuhusu Mume wake. Je ana Mke mwingine? aliniangalia na kuniona kama chizi vile yaani kivipi nauliza swali kama lile wakati yeye anavyohisi ni kwamba yupo mwenyewe tu. Nilimuuliza tena kama labda anahisi ana Wanawake au Mwanamke mwingine? akaniambia hilo swwala kwa Mume wake halipo, Mume wake ni mwaminifu sana. Alinirudishia swali kwanini nauliza hivyo? Mie sikuongea sana kwa kuwa nina Mkeka wangu nishauandaa nilimpa PC ajionee yeye Mwenyewe. Alikodoa macho palee nikaona anatetemeka tu mwili, mie muda huo nipo busy naangalia TV.
Nakumbuka yule Dada alikuwa kama kapata stroke... au kama mtu aliyepigwa shoti jinsi anavyotulia.. eeh. Nilimuita kama mara tatu hivi mpaka nikaamua kumtingisha ndipo alianza kulia sasa kama kuna msiba. Muda huo nilikuwa nimechukua room hotelini so haikuwa sehemu ya wazi. Nilimbembeleza sana.. hakunielewa akawa anasema lazima afe yeye au afe mume wake. Mie nilimbembeleza sana.. kuna muda ikabidi nimuache tu alie akichoka tukae tuongee. (Hapa ndio plan yangu nilitaka niingize).
Kweli, baada ya muda alitulia na kuniangalia tu, nilimuuliza kama yupo tayari niongee nae kitu cha msingi na nini cha kufanya kwa wkati huo. Aliniitikia kwa kichwa tu.
PLAN yangu ni hii:
Kwa kuwa Jamaa ameniharibia sana mambo yangu na Amani ya maisha yangu, vile vile alitaka kunidhuru bila kosa lolote lile hapo awali basi na mimi ni muda wangu wa kulipa kisasi, pia ni muda wa kumaliza hili swala mimi nibaki na Amani na yeye abaki na Amani (Kama ataenda sawa na yale nayoyataka).
1- Bank Details ninazo: hizi niliplan kumhamishia hela zote yule Dada kama itawezekana.
2- Nilipanga kumtumia yule Jamaa encrypted file (with the same passowrd alizokuwa anatumia ku decrypt zile picha) lenye ujumbe wangu kumwambia kila kitu alichokuwa anafanya nimekiona na najua na ushahidi ninao, aamue kusuka au kunyoa. Aache kunifatilia au nimuanike hadharani.
3- Akae akijua Mke wake tayari anajua kila kitu kuhusu yule Mke wake na watoto wake ambao hakutaka wajulikane, pamoja na wanawake wengine anaolala nao na kuwapangia nyumba maeneo tofauti tofauti.
Kwanini Hela zote nimuwekee yule Dada?
Binafsi sikutaka kabisa kujihusisha na fedha za yule Jamaa, pia nilikuwa na uhakika kabisa ile Ndoa ingekufa tu, hizo fedha zingemsaidia huyu Dada kuendelea na Maisha yake mapya huko mbeleni.
Nilihamishaje Fedha?
Katika ulimwengu wa mtandao kuna njia nyingi za kuhamisha fedha, ingawa ni hatari na ni rahisi sana kukamatwa au kubainika pia ni ngumu kuhamisha kiasi kikubwa cha fedha kwa wakati mmoja, mbinu niliyotumia ni kununua bank cards kwenye black market, nakumbuka nilinunua yenye currency ya USD only. nilinunua cards (accounts) mbili. kisha nikaingia kwenye bank ya jamaa na kuset automation ya transfer ya pesa. yes kuna Bank zina offer money transfer automation.
hii ni nini? Mfano una kampuni ina vibarua 20 kila siku inatakiwa uwe unawalipa kwa siku au kwa saa, hii ni usumbufu kuingia na kuwa unalipa mtu mmoja mmoja, so kwa kutumia feature ya Money transfer automation ni kwamba unafeed taarifa za account husika then unaset time frame, system inakuwa inatuma fedha kwa kiwango ulichoset kwenda kwenye account uliyoweka na kwa muda ulioelekeza, uzuri accounts zake zote zilikuwa zina convert currency juu kwa juu through VISA platform.
Niliweka kiwango fulani (Sitakitaja), hela zikawa zinaingia kwenye zile fake Bank accounts kwa muda wa siku mbili mfululizo.
Kwanini hajagundua mapema?
Ukiwa unatumia Monetary apps mfano hizi Banking apps unaweza kuingia kwenye mpangilio wa app na kuipunguzia baadhi ya fetures, mfano unaweza kuondoa notification feature.. yes, mtu/mhusika anakuwa hapati taarifa za uwizi au transactions zinazokuwa zinaendelea, mbili hizi apps haziruhusu kutumika katika simu mbili.. ni kwenye simu moja tu ambayo umeregister ndio itafungua (Ikiwa ni active session). kuna njia ya kuingia kwenye root folder la OS ya Simu husika na kufanya IMEI Dead recorn technique, jambo ambalo IMEI inapachikwa fake kwa muda so app ya Bank haitofungua session maana itataamua/kubaini kuwa hiyo Simu ni nyingine na sio ile simu iliyokuwa registered hapo mwanzo (System fooling).
Pia kuna njia nyingine nyingi kuandika sitamaliza leo, baasi baada ya kufanya hayo yote na kiwango nilichotarget kikiwa kimefanikiwa, nilizitakatisha kwa kuziingiza kwenye bitcoin account then nikawithdraw kwenye account nyingine ambayo nayo ni fake na mwisho kabisa nikaziingiza kwa yule Dada nae sikutumia account yake binafsi alitumia account ya Biashara ya familia yao, nilifanya hivyo ili kuondoa tracing points zote na hakuna ushahidi wowote hapo kati, alinishukuru sana sana, na akawa anasisitiza lazima aachane na yule Jamaa. Mie sikuwa na maoni zaidi ya kumwambia ataamua yeye atakavyotaka ila mie na yeye ndio tushamalizana aendelee na Maisha yake mapya na asifikirie kwamba tunaweza kuwa kama zamani, pia kuonana ni majaaliwa ya Mwenyezi Mungu maana sitataka kabisa kuwepo kwenye maisha yake.
Huku upande wa pili baada ya kutuma ule ujumbe kwa Jamaa hakunijibu siku hiyo hiyo, alikaa wiki nzima na kuniomba nionane nae face to face, Sikukubali kirahisi ila alinisihi sana nionane nae tuzungumze tuyamalize, nilimwelekeza nini anatakiwa kufanya na ni wapi nionane nae, nakumbuka ilibidi nisafiri Morogoro kuna sehemu nilipatarget ndio safe kwangu hata akidhuru basi na yeye hana maisha. tulionana na kuongea mambo mengi ila kuna mambo tuliwekeana makubaliano ambayo sitayaweka wazi. na Ishu yetu iliishia hivyo jamaa yeye anaendelea na mishe zake na mimi naendelea na harakati zangu imepita miaka miwili sasa.
Mwisho.
Wakiume au wakike huyo mwenzie?mwenzie alikuja kumchukua.wakawa wawili.
😅 kawaida..Nimefatilia mwanzo mpaka hapa. Wewe Gentlemen_ ni balaa.
Worry out....Story nzuri sana nilikuwa sijaona tag nimechelewa
[emoji3] mm nilitumiwa kauli moja tuna mume wa mtuPart 2 aisee ni kisa kirefu kidogo..
Ila huyo Manzi baada ya kuwasiliana siku mbili tatu niligundua kuwa ni Mke wa Mtu na ametoka kufunga ndoa recently na aliyemuoa sio yule aliekuwa nae pale.
Yaan story ni ndefu ila ile Ndoa sina hakika kama ipo au La.. ila mie ndio nikawa Suspect namba moja, nilibadiri kuanzia namba yangu ya simu, Mpaka Makazi niliyokuwa naishi.
Nashangaa kwann hamtuzingatiiWana tabu sana hawa viumbe ni wa kuonewa huruma
Hamtakiwi kuzingatiwa 😀Nashangaa kwann hamtuzingatii
Hahaha, safi sana Kamanda.Hakuna mazingira magumu niliyopitia kama ya kuchukua namba ya mtoto mkali mbele ya mama yake mzazi, siku tatu mfululizo pisi mtoto kaumbika inaongozana na mama yake kila siku kuja hapa ninapofanyia kazi kupata huduma, fanya janja janja zoze zikagomba mwamba
Mwamba nilitumia ujanja wote kupata namba ukashindikana japo nahisi kama mama mtoto alikua asha sanukia mishe yangu akazidi kumbana binti yake kweli, ila mwisho wa siku ilibidi nijilipue mbele ya mama yake kuomba namba ya mtoto.
Ilikua hivi wakati wamekamilisha kupata huduma wanatoka nikazunguka kijanja chapu ili niwatokezee kwa mbele na nilifanikiwa hilo. Nikawasimamisha gafla na wakashtuka kama wahalifu , mwamba nika wapa salamu upya na pole na hapo hapo nikamshika binti mkono mbele ya mama yake kwa ujasiri mtoto anataka kuchomoa mkono nikakaza .
Nilifunguka ya moyoni pasi na kupepesa macho , kaza sura mtu nipo serious sana tofauti na alivyo niona awali mama alielewa somo akacheka ikabidi mama asogee pembeni ajifanye anatembea tembea mimi na ongozana na binti yake mithili ya kutoka nje,
binti alikosa cha kuongea alikua kama kapigwa shoti ya umeme maana hakujua ajibu nini na mama yupo around, akaniambia tuu tutaongea basi mimi nikamwambia nipe namba yako tutaongea baadae maana namchelewesha mama yako na sijui lini tutakutana tena kwa kweli namba nilipewa ase
Baada ya kupata chap nikasogea kwa maza mapema ila mama yake alichoniambia ni sentensi hii "wewe kijana unapata wapi ujasiri wa haya yote" mimi nikamjibu kwa kumuuliza kwani baba yake na mwanao alikupataje pataje ? mama mtu akakosa cha kuongea ila alikua anamuangalia binti yake kwa ukali sana lakini hakuwa na namna . Mimi ninachoshukuru tuu mama mtu alikua ana busara sana siyo wa mama hawa wa uswahilini
Japo ndiyo hivyo binti yake nilikuja date nae na kumla mzigo kadiri nilivyo jitakia na mpaka sasa ni moja ya mademu walio katika kumbukumbu zangu za hatari na bado nikimtaka ananiletea ila ananishangaza haniombi hela kabisa
Requirements za kusoma ninatakiwa niwe na sifa zipi?Yeah course zipo ni kujipanga tu hakuna kinachoshindikana
Most of things nimejifunza mwenyewe. Chuon huwezi fundishwa how to buy or sell something on darkweb.Requirements za kusoma ninatakiwa niwe na sifa zipi?
Tunasubiri..Nitaleta andiko namna nilivyonyakua namba ya mrembo mmoja milage zero namba E mbele ya mama ake mzazi
🤣 una moyo.. sanaMi naombaga email mambo ya namba ni uzamani sana,ila usije ukaomba email kwa demu wa mbagala,anaweza akakuuliza ndio chakula gani hicho?