Mbio za Mwenge: Wakimbiza Mwenge watumie vigezo vya kitaalam kukagua miradi

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
IMG-20220406-WA0028.jpg

Katika miaka ya karibuni tumeshuhudia mambo ya ajabu katika ukimbizaji mwenge wa uhuru.

Wakimbizaji mwenge siku hizi wamegeuka kuwa TASK FORCE ya ukaguzi wa miradi.
Sina uhakika kama wakimbiza mwenge ni wahandisi au wataalam wa kukagua miradi na usimamizi wake.

Kama picha hapo juu eti mkaguzi anakagua kwa sululu kupima ugumu wa barabara.
Hili lilofanyika huko Njombe.
Hakuna anayejua vigezo vya ukaguzi huo kitaalam.

Naamini hawa vijana wakimbiza mwenge hawana utaalam wowote, zaidi ya uzalendo mkubwa kwa nchi yao.
Wao si maafisa wa TAKUKURU inayotembea.

Waratibu wa mbio wawape wakimbiza mwenge ujumbe wa kuleta mshikamano, amani ya nchi nakwa ujumla kuleta matumsini kwa wananchi.

Hayo ndiyo yalikuwa majukumu ya kwanza toka enzi za Mwalimu.
 
Yes kazingua katika njia aliyotumia ila kaconfirm hypothesis yake ya kuhisi barabara ni mbovu
 
Yupo mmoja mwaka juzi sijui ni huyu,sikumbuki ila alikuja mtaa ninaoishi huku Mbezi kuzindua kisima cha maji ya Dawasa nikashangaa anaagiza aletewe tindo na nyundo zilipoletwa akagonga gonga kisima mara akapanda jukwaani na kusema hakifai.

Mpaka napoandika hapa hakijatumika kipo kama alivyokiacha sasa mtu unajiuliza ni kwamba kilikuwa kinavuja au nini maana hakuyasema haya.
 

Katika miaka ya karibuni tumeshuhudia mambo ya ajabu katika ukimbizaji mwenge wa uhuru.

Wakimbizaji mwenge siku hizi wamegeuka kuwa TASK FORCE ya ukaguzi wa miradi.
Sina uhakika kama wakimbiza mwenge ni wahandisi au wataalam wa kukagua miradi na usimamizi wake.

Kama picha hapo juu eti mkaguzi anakagua ksa sululu kupima ugumu wa barabara.
Hili lilofanyika huko Njombe.
Hakuna anayejua vigezo vya ukaguzi huo kitaalam.

Naamini hawa vijana wakimbiza mwenge hawana utaalam wowote zaidi ya uzalendo mkubwa kwa nchi yao.
Wao si maafisa wa TAKUKURU inayotembea.

Waratibu wa mbio wawape wakimbiza mwenge ujumbe wa kuleta mshikamano, amani ya nchi nakwa ujumla kuleta matumsini kwa wananchi.

Hayo ndiyo yalikuwa majukumu ya kwanza toka enzi za Mwalimu.
Huo mwenge wakauweke kwenye Museum ya Taifa. Sijawahi kuona umuhimu wake zaidi ya matumizi ya pesa ovyo, uzinzi na udanganyifu kwa miradi ambayo mwenge has NOTHING to do with
 
Yupo mmoja mwaka juzi sijui ni huyu,sikumbuki ila alikuja mtaa ninaoishi huku Mbezi kuzindua kisima cha maji ya Dawasa nikashangaa anaagiza aletewe tindo na nyundo zilipoletwa akagonga gonga kisima mara akapanda jukwaani na kusema hakifai.

Mpaka napoandika hapa hakijatumika kipo kama alivyokiacha sasa mtu unajiuliza ni kwamba kilikuwa kinavuja au nini maana hakuyasema haya.
Wanakiuka maagizo yao ambayo ni kuzungusha mwenge kuhamasisha mshikamano wa kitaifa.
 
Yani ndo tunapoteza mabilioni Kila mwaka ili kuzungusha mwenge wa kukagua miradi Kwa Hali hii?
 
Back
Top Bottom