Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Usijali nitafanya hvyo mkuunaomba ukipika siku 1 nione picha ya jinsi kinavyoonekana tu kwanza...
pika mkuu kama una vitendea kazi vyote mkuu pika,kama hupikinmekwelewa sana mkuu. japo haya mayai ya kisasa yana madawa sana asee mm siyapendi. nkimaliza kusoma hii thread nategemea nitaanza kupenda kupika mana spend kupika asee.!!
fungua macho unapoenda kula mahali tena fungua macho zaidi unapochota mboga Ipo siku utaona kitu na itakua ndio mwisho wako wakula huko.hv karibun nahis ntaanza kupika mana kila cafe nnayohamia naona wanapika hovyo hovyo mno asee. afu unakuta veges waanakuwekea kakijiko kamoja dadeq
Mkuu usiombe ukutane na anayejua kupika maini,yatakuwa your new fav side dish tena km jioni upate na ndizi mzuzu fried au chips na fresh juice.....aah usiku unalala tusijayala maini nadhani huu mwaka mzima,sijui kwann sijawahi sikia hamu ya maini.
ni nini kumbe?
nijibu kama mtanzania tafadhali...
Kwahiyo huyo kitambi anakiona kwenye TV[emoji23][emoji23]pika mkuu kama una vitendea kazi vyote mkuu pika,kama hupiki
nakuhakikishia afya uliyonayo si yako,pika hebu halafu utaona.
Hebu sema ulikula Nini?fungua macho unapoenda kula mahali tena fungua macho zaidi unapochota mboga Ipo siku utaona kitu na itakua ndio mwisho wako wakula huko.
Yaani we acha, niligoma sikulipa.maknge ya mbuzi umekutana na shingo ya kuku, [emoji23] [emoji23]
Hahaha eti zoezi kali,Vyote hivyo nakorofisha pia hupenda nyama ya kukaanga kwa ugali pembeni kuna kachumbari pia prawns wa kukaanga lakini unaacha sosi kidogo hawa ni kwa wali. Sasa hivi niko kwenye zoezi kali sana la kujifunza kupika pilau. [emoji39][emoji39][emoji39][emoji39] Mie pia sipendi kula nje nafanya hivyo mara moja moja sana.
Just hahaha... Maana hii michezo yenu hamuambiliki pamoja na stress zote mnazopata hukoHaha,
Sasa mkianza kwenda sokoni tutawezaje kubana hela ya mchezo??
ni muda sana nilikua nayala kila asubuhi kwenye cafe naletewa na chapati mbili daah yalikua mazuri sana ila baada ya kuondoka ule mkoa sikuwahi pata fundi wakujua yapika kama vile,nili jarbu sehemu tofaut ila bado nikawa nakuta yanapkwa hovyooo basi ukawa mwisho na hadi na leo siya miss hata.Mkuu usiombe ukutane na anayejua kupika maini,yatakuwa your new fav side dish tena km jioni upate na ndizi mzuzu fried au chips na fresh juice.....aah usiku unalala tu
ningekua nakujua ningekuonyesha kitu flani hivi ambacho ndio ingekua mwisho wako wa kula hotelini,naamini siku 1 utakijua na utaanza tu kula nyumbani.
kuna watu wamejivika uzungu wakati wanajua fika tupo Tanzania tena huku tandale ndani ndani.
nakulaga sana tena kwa maelezo hayo hayo uliyotoa pembeni na glass yangu ya mtindi aaah safi kbsaHii ya yai nilikuwa sana nikiwa mwanafunzi. Ukikaanga vitunguu, hoho na nyanya acha viive kidogo. Unavunjia mayai mawili au matatu na kuyaacha kwanza. Yakiiva una Ona kabisa cheupe na njano wala havionekani kama uchafu.
Mkuu wewe ni JINSIA gani kwanza?Mimi ni moja ya wale wajuba wasiopenda kula mitaani iwe hotel,cafe,bar,pub,nk sehemu yeyote wanayotoa huduma ya chakula sio mpenzi wa kula sehemu hizo na hii n kwasababu sipendi pikiwa chakula nisichojua kimeandaliwaje,kimepikwa ktk hali gani,nk nk (sababu ni nyingi).
Mimi ni moja ya watu ambao huchelewa sana kurudi nyumbani kutokana na kazi zangu lakini hii hainifanyi niache kupika kwasababu moja ya vitu nivipendavyo chini ya jua basi kupika ni mojawapo ya vitu hivyo.
Unajua kuna watu humu tunawasiliana sana huwa nikirudi home naweza mwambia ngoja nipike kidogo basi wanaishia kucheka na kuniona muongo sazingine wananikubalia ila hawaniamini kbsa kama napika.
Leo nataja mboga zangu pendwa ninazo penda zipika ninapokua nimerudi home,hizi ni baadhi tu ya zile za chap chap ambazo ndani ya dk.10-20 nishaivisha mzigo upo mezani tyr kuelekea tumboni.
1. Mboga ya nyanya
Hii mboga naiita hivi kutokana nyanya ndio kitu pekee kilichotawala hii mboga.
Mahitaji yangu ni:
Huo mchanganyiko naanza kuupika kama mboga zingine naanza kitunguu maji ilaa sisubri mpk ktunguu kiwe brown nakoroga in 1min natia tangawizi,nakoroga naleta karoti zangu zile zakukata kata + hoho (naweka pamoja) nafunikia kama dk kadhaa nakuja naweka nyanya + karoti zile zakukwangua naweka pamoja nakoroga then nafunika baada ya muda kidogo nakuja namalizia kile kitunguu swaum changu na viungo vya pilau masala+ ile plipli yangu kisha nakoroga mboga naifunikia, in 5min nikifunua nikipga mwko kona mbili tatu linatoka sotojo moja tamu sana. Chumvi mimi huwa nawekaga kule mwanzo kabisa wakati wakukaanga vitunguu.
- Nyanya
- Hoho
- Kitunguu maji
- Kitunguu swaum (hiki hakikosekan kwenye friji huwa kipo standby maana hamna mboga napka ikose hii kitu hakuna)
- Tangawizi (niliyoparua) hiii pia ipo standby kwa friji haikosekani maana naitumia ktk kila kitu ninachopka chini ya jua
- Karot (nakwangua kdg na nyingine nakata kata)
- Viungo vya pilau (vilivyosagwa)
- Pilipili mbichi
Hii mboga nakulaga nayo ugali mkubwa hata mtto mdogo anaweza asivuke. (ni tamu sana na ni simple sana)
2. Mboga ya Mayai
Hii mboga ya mayai nadhani n mboga ninayoila sana chini ya jua kuliko mboga zingine nadhani n kwasababu ya utamu wake na addiction yangu na mayai kwakweli hata kama n kitambi nahisi hii mboga ndio chanzo cha kitambi.
Mahitaji
Ni yale yale na vile vile kama hapo juu kwenye mboga ya nyaya ila ninapopika mboga ya mayai huwa siweki masala za pilau so ktk mahtaji ondoa pilau masala ila vingine vyote viache kama vilivyo.
Jinsi yakuipika hiii kuna style zangu mbili ambazo napenda
style 1
Nikishaandaa mboga yangu kama nilivyoandaa mboga ya nyanya pale juuu ikiwa jikoni navunjia mayai yangu idadi ninayojiskia kisha nakoroga mpk yale mayai yaive mchuzi wa nyanya nao ukauke.Mboga tyr.
style 2
Napika mboga yangu kama mboga ya nyanya kule juu ila ikifka muda wa kuweka mayai,nakaanga pembeni mayai yangu yenyewe kama yenyewe yakiwa tyr nayaweka kwenye sahani nayakata vipende vidogo vidogo kisha vile vipande vyote namwagia kwenye ile mboga yangu,inakua kama nakula nyama mzeee kumbe n vipisi vya mayai,daah tamu sana na ugali.
3. Dagaa
Bana mimi ni moja ya wale raia ukiwalisha dagaa kila siku ndani ya wiki/mwezi/mwaka mzma hawachoki wala kukinai kila siku hii mboga n kama mpya kwangu kutokana na mapenzi yangu kwa dagaa nmejikuta jikon dagaa hawakauki ila sasa dagaa wengi walio tyr n wale wa mwanza wale wanaokua tyr wamekaangwa.
Mahitaji
Wakati wakupka kama kawaida naanza na kitunguu changu maji,sisubr kiwe brown naweka karot + hoho nakoroga then nakuja naweka dagaa zangu + ile karot ya kukwangua kwa pamoja na pili pili yangu nakoroga mpk viungo vyangu karot na hoho nione vinakarbia iva kisha mwsho namalizia na ile nyanya yangu 1,nyanya hii nmeiweka mwsho mana haihelewi kuiva nikipga mwko mizunguko miwili mitatu mzgo unatoka unameremeta kbsa. Mboga tyr kuliwa na chakula cha siku hyo.
- Nyanya 1
- kitunguu maji
- karoti (zakukata kata + za kukwangua)
- hoho
- kitunguu swaum
- tangawizi
- pilipili
4. Kachumbari
Mahitaji
- Nyanya mbichi 1
- Kitunguu maji
- Karoti
- Hoho 1
- Tango
- Parachichi 1
- Limao
- Pilipili
maandalizi n simple kama yeyote anavyoweza andaa basi ikikamilika namix safi kabsa kitu tyr kuliwa na chakula cha siku husika.
5. Mtindi
Hiii kwangu husimama kama mboga na mara zingine husimama kama chakula kbsa maana kuna siku nakunywa nalala yani friji ikose kila kitu ila sio pakti ya mtindi.
Hizi ni zile za chap chap ambazo at any time naweza ziandaa mtu akala chakula akahisi kala 5 star hotel kwasababu sio masihara msosi ninaopenda kuula huwa najua upika kwa ustadi ule unaokidhi vigezo vyote kuliwa na raia mwenye njaa yake mjini.
[QUOTE="Freema Agyeman, post: 36903590, member: 38427"
Dagaa, mtindi na mayai si mboga.