Mbona orodha ya matajiri Tanzania, Kenya, Uganda wengi ni Waarabu na Wahindi na si waafrika weusi?

Nyie endeleeni na siasa tu
Halafu kuombeana ajira serikalini ili muombe Rushwa na kudhulumu watu

Wakati mnakimbiza mwenge na kuimba oo ooh Tanu na Kanu wao walikuwa wanaleta mafuta ya taa na kuwauzia
Hawakuingia siasa kwa sababu ya discrimination ila wakajikita kwenye biashara na kuweza kuwafanya muwe wahitaji wao hata ukiishiwa kasabuni unaenda kumuomba

Tatizo la mswahili hana mipango ya kesho yeye ni kula Bata tu
Akikamata mkaa akapewa elfu 30 anaona kashinda lottery
 
Wapinzani uchwara kama wewe ndo ninaowaongelea. Mnatanguliza vyama kabla ya nchi. Ila tatizo wapinzani wa Tanzania wengi wao elimu duni. Lema, Mbowe, Sugu wanaweza kushauri kitu gani cha kitaalamu? Hasahasa Lema atakimbilia kutabiria watu vifo.
 
Wapinzani uchwara kama wewe ndo ninaowaongelea. Mnatanguliza vyama kabla ya nchi. Ila tatizo wapinzani wa Tanzania wengi wao elimu duni. Lema, Mbowe, Sugu wanaweza kushauri kitu gani cha kitaalamu? Hasahasa Lema atakimbilia kutabiria watu vifo.
Ondoka madarakani ndio uone kama Nchi itaweza kuongozwa au lah....sasa madaraka yote umeshikiria wewe, utajuaje kama wengine wanaweza kuongoza au lah? Kiti cha madaraka umeshikiria wewe tangu tupate Uhuru, alafu unakashifu Vyama ambavyo hamtaki kivipa madaraka... Tukizungumzia umaskini wa nchi, lawama lazima ziangukie CCM, kwa sababu nyie ndio mmeshikilia madaraka tangu tupate uhuru, CCM ingekuwa ni mtu basi isingekuwa tofauti na Museveni
 
mkoloni alimuandaa nani wewe? Hao akina Bakhresa walioanza kuwa wauza viatu vya kushona? Kwa nini hatutaki kutambua juhudi za watu kujikomboa lazima tuambatanishe na ukabila fulani?

Mbona wawe hao hao waarabu na wahindi. Umezungumzia kwamba alianza na kuuza viatu vya kushona, ni watanzania weusi wangapi pia walianza nae hiyo biashara ila sasa hawapo?

Shida ni serikali, ukiwa muwekezaji mweusi unapigwa sana vita, ila ukiwa na ngozi nyeupe unaonekana ndio unastahili
 
Sasa si bora kuendelea na CCM angalau tumeona kasoro zao na walipopatia kuliko kuachia nchi kwa watu ambao mwaka mzima ni malalamiko tu huku hawatoi suluhisho lolote. Mara nyingi mpinzani akifanya kosa majibu yake ni "mbona CCM wamefanya"? Kuna makada wangapi waandamizi wa upinzani wanaoongea mambo kitaalamu ukimtoa Lipumba na mara chache Zitto?
 
Hii nchi haiko chini ya autocracy (ufalme), hii nchi ni ya kidemokrasia kuruhusu mfumo wa vyama vingi kutawala... Hayo mambo ya Single party system tuliachana nayo mwaka 1992.

Tanzania ina Raia zaidi ya Millioni 60, kwenye hao raia wote unataka kusema viongozi wanaofaha wanatoka CCM tu?

Mitaani kuna viongozi wengi wazuri kuliko hao walioko CCM, na hawakupata fursa CCM kwa sababu muda mwingine huko CCM mnawekana madarakani kwa kujuana. Sasa hawa viongozi walioko mitaani wameamua kujiunga na vyama pinzani angalau waingie serikalini waifikishe nchi kwenye nchi ya ahadi lakini nao mmewaua ndoto zao.

Haya bunge lote limejaa wanaCCM ila mikataba inapitishwa bila kusomwa, mbunge anapiga kura ya kupitisha mkataba bila hata kujua kilichoandikwa... Alafu bado unataka tuendelee kuiamini CCM.
 
CCM inaenda kuanguka miaka ijayo kwa sababu vizazi vilivyozaliwa enzi za ujamaa vinaenda vinakufa. Vinakuja vizazi vya mfumo wa vyama vingi kuanzia miaka ya 1990.

Usije kudhani CCM itadumu madarakani milele, miaka ijayo huko mpaka 2050 CCM itaanguka tu
 
mkoloni alimuandaa nani wewe? Hao akina Bakhresa walioanza kuwa wauza viatu vya kushona? Kwa nini hatutaki kutambua juhudi za watu kujikomboa lazima tuambatanishe na ukabila fulani?
Race ya bakhresa umeiona,ana uswahili kwani [emoji1]

Ova
 
Wewe umefafanua vyema sana. Elimu ni muhimu. Kina Hushpupi pamoja na uhalifu wao ila walikuwa wamebobea kwenye elimu ya IT na Banking. Elimu, elimu, elimu.
 
Huu uzi ni mkubwa sana kwa uwezo wako wa kufikiri. Nakushauri utumie tu emoji kutoa maoni yako badala ya kuandika vitu vilivyokaa kisiasa.
 
Hao jamaa wanamipango,wachapakazi,
Wanajuwa kuendeleza Mali ya urithi
Ngozi nyeusi kazi kubaniana,kukomoana kufanyiana figisu tu

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…