Mbona sasa hivi matangazo ya kampuni za BETTING yameshamiri sana?

Mbona sasa hivi matangazo ya kampuni za BETTING yameshamiri sana?

Bingwa wa kamari za casino za mtandaoni nakuja kutolea ufafanuzi jinsi Watanzania wanavyoliwa na makamari ya kubet mpira na namba.
Njoeni kwenye casino mtafurahi
 
Radio hawana cha kuzungumza sahvi
Zaidi ya mipira,mambo ya wasanii,umbea,kamari
Mfumo ndiyo unataka hivyo

Ova
 
Bora hizo redio za kwenu zinatsngaza Mambo ya fweza. Sasa kuna station fulan maeneo yetu huku kila baada ya dk 10 ni matangazo ya mganga wa jadi toka sumbawanga
Na kuna zingine ni kuwasifia mitume , manabii na makuhani tu.
Huku wakitangaza nguvu za uwezo wa vifaa vya kiroho kama maji, sticker na mafuta
 
Najua tena Nakiri kuwa Uti Mgongo wa Media yoyote ile ni Matangazo na yakiwa mengi zaidi ndiyo Afya kwa Ustawi wa Kimapato kwa Media husika na Mishahara mikubwa na ya uhakika kwa Wafanyakazi (Watumishi) wake.

Ila hili la Kipindi cha Michezo cha Sports Headquarters cha EFM ambacho huwa kinaanza Saa 3 Kamili Asubuhi hadi Saa 6 Kamili Mchana kimetawaliwa na Matangazo mengi kuliko Contents za Michezo.

Kwa mfano Kinachowakera Wasikilizaji wengi ni pale Kipindi hiki cha Michezo kinaachoanza Saa 3 Kamili kuanza Kulundikwa na Matangazo ya Bandika Bandua na Taarifa za Habari kuanza ama Saa 3 na dakika 25 au na dakika 30 kitu ambacho Kinawakwaza Wasikilizaji (Audiences) wengi na kujikuta Wakihamia Kusikiliza Redio zingine kama Clouds FM, Uhai FM, Wasafi FM na hata Magic FM.

Tafadhali sana Boss Dizzo (Dickson Mwaimu) lichukue na lifanyie hili Kazi kwani linawakera Wasikilizaji wenu na sasa Wengi wao wameanza Kuwahama na msipoangalia na kubadilika mnaweza kujikuta mkawa Mnatangaza hapo Studioni mkidhani mnasikilizwa na Wengi kumbe mkawa mnasikilizwa na Wanafamilia wenu pamoja na Mahawara zenu ila Wenye Akili wameshawahama Kitambo tu.
 
Mnatuchosha na issue za mipira nyie vijana, washajua mnajazana kwenye kipindi muda huo ili kutumiza agenda za vijana wa sasa kubeti na kubishana mipira, hivyo wanaotengeneza hela wanatumia huo muda pia kulipia matangazo yao na kila mtu anataka litangazwe huo muda ili wapige hela zaidi.
 
Bila matangazo hakuna redio
Nalijua hilo ila waangalie jinsi ya kuyachezesha kulingana na Content vinginevyo itaishia kuwafanikisha Kimapato tu ila upande wa Wasikilizaji wakawahama na baadae hata hayo Matangazo yenyewe wenye nayo wanaweza Kuyatoa na kupeleka Kwingineko kwani watagundua kuwa mmekimbiwa na Wanaowalenga ambao ni Wasikilizaji.
 
Nalijua hilo ila waangalie jinsi ya kuyachezesha kulingana na Content vinginevyo itaishia kuwafanikisha Kimapato tu ila upande wa Wasikilizaji wakawahama na baadae hata hayo Matangazo yenyewe wenye nayo wanaweza Kuyatoa na kupeleka Kwingineko kwani watagundua kuwa mmekimbiwa na Wanaowalenga ambao ni Wasikilizaji.
Mbona leo unaongea kwa nidhamu sana? Nini kimekusibu hadi kuwa na nidhamu ya ghafla?
 
Back
Top Bottom