Mbona wanawake ndio wanaongoza kwa kushauri wanaume kuoa?

Mbona wanawake ndio wanaongoza kwa kushauri wanaume kuoa?

Naendelea kukusanya data kila siku.
Ukikaa na wanaume huwezi ukasikia wakimshauri mwanaume mwenzake kuoa mara kwa mara lakini kinyume chake

wanawake wamekuwa washauri wakuu wa vijana waliofikia umri wa kuoa kwamba oa oa ♫︎♫︎♫︎♫︎ kama wimbo sasa sijui kwa nn wao ndio washauri wakuu siku hizi.

Utaskia wanasema oa kijana umri unaenda.
Oa maisha ni hayahaya.
Oa utakuja kuitwa babu na watoto wako.

Oa utakuja kuzaa watoto wasiokuwa kuwa na akili.
Oa utakuja kusomesha uzeeni
Oa watukuja kukugongea mke wako.
Oa utakufa uache watoto wadogo.
Oa uendeleze kizazi eti kitapotea.
Utaishije mwenyewe huo ni uchoyo.
Oa ukifa upate wa kukulilia

Mbona wanakuja kwa kasi sana.
Ukijipenda mwenyewe watu wanaonaje sijui.

Jitathmini mwenyewe kwanza ewe kijana.
Hahahh, kuna ndugu zangu walikuwa wanamsakama mdogo wangu unaoa lini, kila kikao au shughuli wanamuuliza.
Siku moja akawatolea uvivu, hivi nikioa mtafaidika nini?
Toka siku hiyo hawakumuuliza tena. Kipindi hicho alikuwa na vikazi vya kuungaunga na hata kodi ya nyumba ilikuwa inasumbua kulipa.
Wabongo ni shida sana. Kuna ndugu yangu eti mtoto wa sijui elfu 2000 wamemupzesha na hana kazi. Sasa hivi mama yake kastaafu analea mtoto, mkwe , mjukuuu, analalamika maisha magumu.
Nawaangalia tu wapambane na hali zao.
 
Unapozungumzia Mahusiano /Ndoa familia haya mambo kwa mwanamke yanachukua 70% kama sio 80%

Mwanamke ndoa inamjenga ,inampa utambulisho (identity) na pia inampa prestige hasa anapokuwa na watoto ambao wanamuita mama .

Mwanamke kukushauri kuoa au kupata mtoto anakuwa yupo sahihi kabisa .

Neno "mke wa MTU " lina uzito mkubwa kuliko "mme wa MTU "

So ikiwa utapata kutafakari hayo mambo unaweza kuelewa kwa kina.
mbona kama falsafa ......fafanua tena kidoogo japo anayefaidi ni mwanamke na mwanaume hana maana.
 
Kwanini wanawake wanaunga zaidi mkono ndoa ukilinganisha na wanaume

1. Ndoa inalinda zaidi masilahi ya mwanamke. Wajibu wa mwanaume unatambulika kisheria na anashurutishwa kuutimiza tofauti na wajibu wa mwanamke ambapo ni hiyari ya mwanamke kutimiza, vile vile ndoa inapovunjika mwanamke analipwa fidia ya muda aliotumia katika ndoa lakini mwanaume halipwi fidia ya muda wake kwenye ndoa iyo iyo.

2. Ndoa ni ajira ya kudumu kwa mwanamke. Endapo mwanamke maisha yakimpiga knock out basi ndoa inaweza kuwa kimbilio lake.

3. Ubora wa mwanamke haudumu kwa muda mrefu. Mwanamke anakua kwenye kilele chake cha ubora kuanzia anapovunja ungo mpaka late 20s, anapoingia 30s ubora wake kuanzia uzuri mpaka uwezo wa kuzaa unaingia kwenye declining stage, kwaiyo ni lazima akukuluke amalizane na mambo yote hapo kwenye 20s.

4. Njia ya mkato kufanikiwa kimaisha. Kwa sasa wanawake walio wengi duniani kote wamegeuza talaka, child support na mirathi ya mume kuwa miradi ya kibiashara. Mwanamke akiitimua ndoa kimkakati inaweza kumpa utajiri.
Ndoa ni ajira ya kudumu kwa mwanamke. Endapo mwanamke maisha yakimpiga knock out basi ndoa inaweza kuwa kimbilio lake. 100% 𝐰𝐞𝐧𝐠𝐢 𝐰𝐚𝐤𝐢𝐨𝐧𝐚 𝐰𝐚𝐦𝐞𝐬𝐡𝐢𝐧𝐝𝐰𝐚 𝐤𝐮𝐩𝐚𝐭𝐚 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐜𝐡𝐨𝐡𝐢𝐭𝐚𝐣𝐢 𝐡𝐮𝐭𝐚𝐟𝐮𝐭𝐚 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐮𝐦𝐞 𝐰𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚𝐧𝐲𝐚𝐧𝐲𝐚𝐬𝐚.
 
Unapozungumzia Mahusiano /Ndoa familia haya mambo kwa mwanamke yanachukua 70% kama sio 80%

Mwanamke ndoa inamjenga ,inampa utambulisho (identity) na pia inampa prestige hasa anapokuwa na watoto ambao wanamuita mama .

Mwanamke kukushauri kuoa au kupata mtoto anakuwa yupo sahihi kabisa .

Neno "mke wa MTU " lina uzito mkubwa kuliko "mme wa MTU "

So ikiwa utapata kutafakari hayo mambo unaweza kuelewa kwa kina.
naamini na kuhisi tunaitaji zaidi wanawake ambao ndoa kwao is not about identity au wenye kufikiria kuwa nikiwa 'mke wa mtu' ndiyo nakuwa na heshima kwenye jamii;

kwa mawazo ayo ndiyo inapelekea wengi kuona ndoa kama jau, just imagine unaona mwanamke ambaye anaingia kwenye ndoa kwasababu tu anataka ndoa as identity au kuitwa mke wa mtu;

sikatazi watu kuoa ila usioe mtu ambaye kwake ndoa ni kama kivuli cha identity yake au anatamani tu kuitwa mke WA MTU.....
 
Unaheshimika bwana ukiwa umeoa, unaacha kuonekana muhuni. Unaonekana unajua wajibu. Huulizi kwanini kuna nafasi huwezi kupata kama hujaoa?
hapa ndiyo panapo tuumiza yaani ni kama tunafanya vitu kwa kuhofia watu watanionaje;

Oa lakini ndoa isiwe kitu cha kufanya kisa tu ooh! ntaonekana muhuni, nisipo oa ntaonekana sijui wajibu wangu;
 
Unapozungumzia Mahusiano /Ndoa familia haya mambo kwa mwanamke yanachukua 70% kama sio 80%

Mwanamke ndoa inamjenga ,inampa utambulisho (identity) na pia inampa prestige hasa anapokuwa na watoto ambao wanamuita mama .

Mwanamke kukushauri kuoa au kupata mtoto anakuwa yupo sahihi kabisa .

Neno "mke wa MTU " lina uzito mkubwa kuliko "mme wa MTU "

So ikiwa utapata kutafakari hayo mambo unaweza kuelewa kwa kina.
Wewe jamaa unajua sana.
 
Ukiondoa sababu za kiimani( kwa waamini).....mkataba wa ndoa una manufaa makubwa kwa mwanamke kuliko kwa mwanamume........ mwanamke akishaingia kwenye ndoa anakuwa amesha tatua robo tatu ya matatizo yake maishani mwake......... mwanamke mwenye ufahamu lazima alilie kwa kuwa ndani yake kuna manufaa mengi......
 
hapa ndiyo panapo tuumiza yaani ni kama tunafanya vitu kwa kuhofia watu watanionaje;

Oa lakini ndoa isiwe kitu cha kufanya kisa tu ooh! ntaonekana muhuni, nisipo oa ntaonekana sijui wajibu wangu;
Sio kwamba unaonekanaje, wapo watu ambao hawajaoa na haina shida

Ni kwamba tu ukiipatia ndoa, faida yake ni maradufu. Watu hapa hawasemi, ila bila wake zao wasingekuwa walipo
 
Watu hapa hawasemi, ila bila wake zao wasingekuwa walipo
1000300113.jpg
 
Back
Top Bottom