Mbowe aliiweka Chadema rehani kwa Samia. Sisi tulimuuliza kwani kuna shida gani mzee? Mbona uwezo tunao huku ukituweka rehani?

Mbowe aliiweka Chadema rehani kwa Samia. Sisi tulimuuliza kwani kuna shida gani mzee? Mbona uwezo tunao huku ukituweka rehani?

Ndio maana wapambe na chawa wake wanahaha
Kuna 12b wametengewa wakiweza kumuondoa Lissu kwenye siasa kabisa,yaani asiwe mwenyekiti na asipewe nafasi ya kugombea urais. Hiyo 12b imewatoa ufahamu wengi sana ndiyo maana threads za kumponda Lissu hazikauki kila baada ya dakika tano zinazalishwa .
 
Muarobaini wa matatizo katika vyama vya siasa ni Kuruhusu Mgombea huru
 
Toka 2022 ndio watu wanajitokeza leo kuanika "dhambi" za Mbowe? Hayo mapendekezo yalitoka kwa nani? Kama ni kutoka kwa CCM, alifanya kosa gani kuwashirikisha wenzake? Hayo yalikuwa ni mapendekezo ambayo Kamati Kuu ilikuwa na mamlaka ya kuyakataa na nadhani ndivyo ilivyokuwa. Sidhani kama Mbowe angekubali kupewa majimbo 20 maana kwa experience yake ni lazima alijua kuwa kuna uwezekano mkubwa wa CCM kumgeuka kwa ama kutoruhusu CDM washinde kama walivyo ahidi ( mfano ni NCCR Mageuzi) ama watatoa nje makubaliano hayo ili wakimalize kabisa chama chake. Mbowe sio mjinga kiasi hicho.

Mimi ninavyojua ni kuwa Lissu alitangaza nia ya kugombea urais kama chama chake kitampa idhini. Sijamsikia Mbowe akisema lolote kuhusu hilo. Kama angekuwa hataki angeweza kusema kuwa ametangaza nia mapema mno. Na mpaka hivi karibuni Lissu alikuwa anasisitiza kuwa yeye nia yake ni kugombea umakamu Mwenyekiti na urais tu. Kama alifanya hivyo huku akijua kuhusu usaliti mkubwa wa Mbowe basi tatizo litakuwa lake. Wenje amezungumzia tuhuma zilizotolewa dhidi ya Mbowe za kuhongwa magari mawili ambayo kiukweli aliyanunua katika mnada. Mpaka sasa hivi hatujaelezwa kama ni kweli tuhuma zilitolewa na kama zilikuwa za kweli.

Ninavyojua mimi ni kuwa strategists wengi wa vyama vya siasa huwa wanaangalia ni sehemu gani ndiko wana uhakika zaidi wa kushinda, na huko ndiko wanaweka nguvu kubwa. K.m. sio rahisi kwa Chadema kushinda Pemba na Mafia kwa hiyo itakuwa busara zaidi kuwekeza zaidi kwenye majimbo ya Mbeya, Mara n.k.

Hivi karibuni pamejitokeza tuhuma za ajabu ajabu kutoka kwa watu wanaodai wako jikoni. Kuna wanaodai walizuiwa na watu wa Mbowe kugawa kompyuta na kadhalika. Humu ndani wamejaa watu ambao wanaamini wakimchafua Mbowe ndio mtu wao atashinda na chama chao kitaingia kwenye era mpya ya mafanikio.

Nashauri wanyamaze. Kama wana ushahidi wa tuhuma hizo wazikabidhi kwa Kamati Kuu. Kama hawana imani nayo basi wamfanyie kampeni safi mgombea wao ili ashinde bila kukivuruga chama zaidi. Akishinda, wataweza kuzifuatilia na kuzichukulia hatua stahiki. Haya wanayofanya ni kwa faida ya wapinzani wao na sio chama chao.

Amandla...
Hakika wewe umeongea. Anachokifanya Lisu na wafuasi wake ni kuiua Chadema na wala si kampeni kwa nia ya uchaguzi uliosafi. Hata Lisu akishinda uchaguzi huu, hakika Chadema haiwezi kuwa moja tena kutokana na majeraha wanayosababisha. Lisu namfananisha na Mabere Marando wa enzi za NCCR. Ameamua kupasua Chama kwa maslahi binafsi au Ego yake tu.
 
Watu hamjui tu ila hili sekeseke la Chadema na Samia tulianza nalo mwaka 2022 mwishoni. Ilikuwa ghafla sana mwenyekiti wetu alibadili "jia" angani.

Aliyosema Lissu leo ni ukweli mtupu. Ndani ya Chadema kulikuwa na vuguvugu sii la kitoto. Mnyika ni shahidi.

Mwenyekiti alikuja na mapendekezo kwamba kusiwe na mgombea urais mwenye nguvu ama asiwepo kabisa mwaka 2025. Pia akaja mpaka na orodha ya majimbo ambayo Chadema ingeachiwa mwaka 2025. Kama kuna mtu atabisha basi tutayaweka hadharani. Miongoni mwa hayo majimbo watu wake nanga zinapaa kweli kweli kwa sasa maana wana faida wataipata huko mbeleni. Sisi tuliuliza, kwanini tuingie kwenye makubaliano hayo? Mbona nguvu tunayo?

Kiukweli ni jambo baya sana kumsema kiongozi mwenye Legacy kama Mbowe lakini hapa mwishoni alituuza, alituweka rehani. Sisi wengine tulihoji kulikoni? Mbowe anafaidika na nini? Mbona uwezo wa kupata hata majimbo zaidi ya 100 tunao mwaka 2025? Leo tuingie kwenye maridhiano ya kudanganywa na majimbo chini ya 20 ili tu mtu avuke? Ili nani afaidike?

Yapo mengi kweli tutayasema wazi wazi siku za mbeleni ila Mbowe kwa hatua aliyokuwa amefikia si wa kumung'unyiwa tena maneno! Aliharibu pakubwa!
Huo uwezo mbona hatujauona kwenye uchavuzi wa serikali za mitaa?
 
Watu hamjui tu ila hili sekeseke la Chadema na Samia tulianza nalo mwaka 2022 mwishoni. Ilikuwa ghafla sana mwenyekiti wetu alibadili "jia" angani.

Aliyosema Lissu leo ni ukweli mtupu. Ndani ya Chadema kulikuwa na vuguvugu sii la kitoto. Mnyika ni shahidi.

Mwenyekiti alikuja na mapendekezo kwamba kusiwe na mgombea urais mwenye nguvu ama asiwepo kabisa mwaka 2025. Pia akaja mpaka na orodha ya majimbo ambayo Chadema ingeachiwa mwaka 2025. Kama kuna mtu atabisha basi tutayaweka hadharani. Miongoni mwa hayo majimbo watu wake nanga zinapaa kweli kweli kwa sasa maana wana faida wataipata huko mbeleni. Sisi tuliuliza, kwanini tuingie kwenye makubaliano hayo? Mbona nguvu tunayo?

Kiukweli ni jambo baya sana kumsema kiongozi mwenye Legacy kama Mbowe lakini hapa mwishoni alituuza, alituweka rehani. Sisi wengine tulihoji kulikoni? Mbowe anafaidika na nini? Mbona uwezo wa kupata hata majimbo zaidi ya 100 tunao mwaka 2025? Leo tuingie kwenye maridhiano ya kudanganywa na majimbo chini ya 20 ili tu mtu avuke? Ili nani afaidike?

Yapo mengi kweli tutayasema wazi wazi siku za mbeleni ila Mbowe kwa hatua aliyokuwa amefikia si wa kumung'unyiwa tena maneno! Aliharibu pakubwa!
GSam, hakika wewe ni mtu niliyekuheshimu sana hapa jukwaani kwa hoja zako Murua. Ila kwa hili naona kama unapotoka vile. Mbowe asichukuliwe kama Mungu bali binadamu ambaye anakosea na kuweza kukosolewa kupitia machineries za chama. Nionacho hapa ni utovu wa nidhamu kwa wote wanaomfanyia kampeni Lisu wakiongozwa na yeye mwenyewe. Wanachokifanya hakina tofauti na Mabere Marando wa NCCR miaka ile. Nadhani wewe ulikuwa kijana mdogo sana kuweza kushuhudia ile minyukano. Kwa mantiki hiyo usitegemee Chadema iliyomoja chini ya Uenyekiti wa Lisu. Lisu ni mtu egoistic sana kiasi kwamba yuko tayari kuanika mambo ya ndani ya Chama kwa maslahi yake binafsi. Namuona kama mtu aliyeamua kugawana fito za nyumba na si vinginevyo. Na huo ndio utakuwa mwisho wa Chadema, belieave me or not.
 
Lissu akiwa mwenyekiti wala rushwa watamuogopa ,wakimwita gizani kuteta naye kumrubuni,asubuhi peupe anaongea yote kinagaubaga. LISSU OYEEEE...
 
Watu hamjui tu ila hili sekeseke la Chadema na Samia tulianza nalo mwaka 2022 mwishoni. Ilikuwa ghafla sana mwenyekiti wetu alibadili "jia" angani.

Aliyosema Lissu leo ni ukweli mtupu. Ndani ya Chadema kulikuwa na vuguvugu sii la kitoto. Mnyika ni shahidi.

Mwenyekiti alikuja na mapendekezo kwamba kusiwe na mgombea urais mwenye nguvu ama asiwepo kabisa mwaka 2025. Pia akaja mpaka na orodha ya majimbo ambayo Chadema ingeachiwa mwaka 2025. Kama kuna mtu atabisha basi tutayaweka hadharani. Miongoni mwa hayo majimbo watu wake nanga zinapaa kweli kweli kwa sasa maana wana faida wataipata huko mbeleni. Sisi tuliuliza, kwanini tuingie kwenye makubaliano hayo? Mbona nguvu tunayo?

Kiukweli ni jambo baya sana kumsema kiongozi mwenye Legacy kama Mbowe lakini hapa mwishoni alituuza, alituweka rehani. Sisi wengine tulihoji kulikoni? Mbowe anafaidika na nini? Mbona uwezo wa kupata hata majimbo zaidi ya 100 tunao mwaka 2025? Leo tuingie kwenye maridhiano ya kudanganywa na majimbo chini ya 20 ili tu mtu avuke? Ili nani afaidike?

Yapo mengi kweli tutayasema wazi wazi siku za mbeleni ila Mbowe kwa hatua aliyokuwa amefikia si wa kumung'unyiwa tena maneno! Aliharibu pakubwa!
Inasikitisha sana
 
Ndugu yangu napenda kukupa Taarifa Kwamba, Kesi ya Ugaidi ya Mbowe ilikuwa na ushaidi mwingi sana. Ndiyo Sababu Mbowe anamshukuru sana Samia Kwa Msamaha wake!
Kuna siku Mama Samia alisema maneno kuhisi hiyo case watu wanalalamika kaonewa ooh ni siasa akasema subilini muone mahakama si zipo so evidence against him kwenye case ya ugaidi was seem/ deemed strong kiasi Mbowe angekutwa na hatia so analipa fadhila
 
GSam, hakika wewe ni mtu niliyekuheshimu sana hapa jukwaani kwa hoja zako Murua. Ila kwa hili naona kama unapotoka vile. Mbowe asichukuliwe kama Mungu bali binadamu ambaye anakosea na kuweza kukosolewa kupitia machineries za chama. Nionacho hapa ni utovu wa nidhamu kwa wote wanaomfanyia kampeni Lisu wakiongozwa na yeye mwenyewe. Wanachokifanya hakina tofauti na Mabere Marando wa NCCR miaka ile. Nadhani wewe ulikuwa kijana mdogo sana kuweza kushuhudia ile minyukano. Kwa mantiki hiyo usitegemee Chadema iliyomoja chini ya Uenyekiti wa Lisu. Lisu ni mtu egoistic sana kiasi kwamba yuko tayari kuanika mambo ya ndani ya Chama kwa maslahi yake binafsi. Namuona kama mtu aliyeamua kugawana fito za nyumba na si vinginevyo. Na huo ndio utakuwa mwisho wa Chadema, belieave me or not.
Mbowe kweli alikengeushwa na niliyoandika aliyafanya. Mbowe huyu sie yule tuliyemuishi
 
Back
Top Bottom