DOKEZO Mbowe anakwenda kupewa nafasi nyeti ili kuyalinda maridhiano

DOKEZO Mbowe anakwenda kupewa nafasi nyeti ili kuyalinda maridhiano

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kama katiba ya CCM imekubali mpinzani kuwa makamu wa raisi (maalim seifu)
Je itakataaje mpinzani kuwa naibu waziri?
Hoja yako inafikirisha. Maana walibadilisha katiba yao ya visiwa lakini hawakubadili ya Chama, Katiba ya Chama haiwezi kuwa zaidi ya ile ya nchi.
You have a point.
 
Hili tulishalidokeza siku nyingi; labda tu ni kwa vile haikuanzishwa kama mada.

Dalili zote zinaonyesha kwamba siasa za Kenya ndizo zinazokuja kujaribiwa Tanzania.
Ni kama Tanzania siku hizi inaiga kila kitu kinachofanyika Kenya; iwe ukulima wa parachichi, nasi tunakimbilia kuiga; kuzungumza kiingereza, nasi tunataka tuwe kama wao. Wakisema wao wanawatambua 'diaspora' wao kwa kiwango fulani, nasi tunatafuta kuhimiza watu wetu watoke kwenda nje;, kana kwamba hapa kwetu hakuna fursavtele ambazo vijana wetu hawa wanaweza kuzitumia kujenga taifa lao kwa ufanisi.

Tumekuwa watu wa kuiga tu kila kitu, hatuna ubunifu wowote tunaoweza kujivunia...; la hasha; nisisahau Kiswahili chetu na taasisi yetu iliyofanya kazi nzuri sana BAKITA.

Nje ya hapo, ninaomba kukumbushwa eneo jingine tunaloweza kujivunia katika kulifanya vizuri.

Lakini naomba usinitajie udumu wa CCM kwenye madaraka, kama mfano.
Kama unamaanisha kuwa mpinzani kuteuliwa na raisi tumeiga Kenya basi unajidanganya sana unless uwe na lako jambo aidha wewe ni Mkenya ambae unatumia kimvuli cha siasa za Tanzania kuonesha kuwa nchi yenu ni bora nk.
Swala la serikali ya Tanzania kushirikiana na wapinzani lipo miaka na miaka toka enzi za kina maalim seifu kushirikiana na serikali ya Zanzibar, Kikwete alimteuwa Mbatia ambae ni mpinzani mwaka 2010, Magufuli hivyo hivyo 2015 to 2020. Na sasa Samia. Tanzania haijawahi kujifunza wala kuiga saisa toka nchi yoyote ya EA na maziwa makuu, isipokuwa kuna nchi za maziwa makuu ambazo zinajifunza siasa kutoka Tanzania.

Mbona haujasema kwamba Kenya imejifunza siasa kutoka Tanzania kwani kabla ya hapo Kenya ilikuwa inaongozwa kidikteta na mzee Arap Moi huku Tanzania ikiendeshwa kwa mfumo wa kidemokrasia wa kubadilishana vijiti kila baada ya miaka 10 raisi anatoka anaingia mungine. Lakini kwa Kenya haikuwa hivyo hadi miaka ya 2000 ndo wakaanza utaratibu kama wa Tanzania, na wao kubadilishana vijiti kila baada ya miaka 10 kwa kufuata mfumo wa Tanzania ambao ulikuwa umeshazoeleka huku Tanzania kitambo?
Burundi, Congo nk zikafuata mfumo huo ambao kabla haukuwepo katika nchi zao. Mbona haukusema nazo zimeiga mfumo wa Tanzania?
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] hili neno linakua kwa kasi sana,eti na yeye japo amiminiwe asali [emoji23][emoji23][emoji23][emoji114][emoji114][emoji114]
Amna mwamba tuna imani nae 😂😂😂
 
Oh kumbe unaamini kuwa ikiundwa serikali ya kitaifa ambayo Mbowe yupo ndani yake kutakuwa na upigaji.

Kwa maana nyingine Mbowe nae atakuwa mpigaji kupitia kimvuli cha umoja huo, sawa umeeleweka.
You surely are deeply obsessed with Mbowe. What is he to you, btw?

I ain’t made reference to no individual ‘cause it’s immaterial.
 
Umejenga hoja vizur ila hiyo aya hapo mwisho umeharibu kabisa
Sijaharibu; ni fact ambayo siyo ngumu sana kuikubali, ila tulio wengi huwa tunakwepa kuikubali. Bado hatujaandaa chama kingine kinachoweza kushika dola kwa usahihi. Tunavyo vyama vingi tu vinavyoweza kushika dola ila si kwa usahihi. Tukilikubali hilo, ndiyo pale maandalizi yetu yatakapoanzia
 
Sijaharibu; ni fact ambayo siyo ngumu sana kuikubali, ila tulio wengi huwa tunakwepa kuikubali. Bado hatujaandaa chama kingine kinachoweza kushika dola kwa usahihi. Tunavyo vyama vingi tu vinavyoweza kushika dola ila si kwa usahihi. Tukilikubali hilo, ndiyo pale maandalizi yetu yatakapoanzia
Huyo alieku quote anajua sana. Sema amejaribu kukwepesha ukweli ili kutafuta uungwaji mkono wa chawa wenzake.
 
Ndo maana mie mwenzenu haya mambo ya siasa siyatoleagi macho kivile,, mpinzani wa kweli bongo hayupo, narudia tena hayupo, wote wanatafuta vyeo(ulaji) kwa ajili ya wao na familia zao, rejea kwa Edward lowasa, tambwe hiza, dokta mashinji, etc.
Ccm wenyewe wanaong'ang'ania madaraka hadi kuua wananchi na kuhujumu uchaguzi wao ndio hawataki ulaji.
 
Bora akapumzike maana wa tanzania bado hawajawa tayari kwa mabadiliko
Bado wametawaliwa na woga na unafiki
Kujitolea kuwapigania watu ambao hawajielewi utaiadhirishaa Familia yako na wanaokutegemea
Utakufa wabaki wanakukebei
 
Bora akapumzike maana wa tanzania bado hawajawa tayari kwa mabadiliko
Bado wametawaliwa na woga na unafiki
Kujitolea kuwapigania watu ambao hawajielewi utaiadhirishaa Familia yako na wanaokutegemea
Utakufa wabaki wanakukebei
Kama jinsi Magufuli alivyowapigania watanzania dhidi ya wanyonyaji wa nchi yetu. Matokeo yake wanyonyaji wakawatumia wachumia tumbo wa nchi yetu wenyewe kumkebehi na kumdhihaki.

Kama alivyosema kwamba na sacrifice maisha yangu kwa ajili ya Tanzania. Kweli ka sacrificed maisha yake na sasa anadhihakiwa.
 
Back
Top Bottom