DOKEZO Mbowe anakwenda kupewa nafasi nyeti ili kuyalinda maridhiano

DOKEZO Mbowe anakwenda kupewa nafasi nyeti ili kuyalinda maridhiano

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Habari zenu wana JF wenzangu, natumai kila mtu ana afya tele.

Kwa dokezo lililonifikia kutoka kwa mtu ambae siwezi kumtaja, ni kwamba mama anamuandalia kamanda Mbowe nafasi nyeti na muhimu ndani ya serikali yake ili kujenga serikali yenye sura na mtazamo wa kitaifa.

Ikumbukwe kwamba raisi Samia aliwahi kunukuliwa akitamka mwenyewe kwamba serikali yake anayoiunda angependa kuona anashirikiana na wanasiasa wa vyama vingine vya siasa, ili kutengeneza serikali ya kitaifa ambayo haiegemei upande wowote wa chama.

Na katika hili raisi ameanza kuonesha njia kwa kujiweka mbali na siasa za majitaka, ambazo zimekuwa zikiwafaidisha wapuuzi wachache waliopo ndani na nje ya chama chake.

Mungu ilinde Tanzania yetu
Mungu mlinde raisi wetu
Mungu ilinde amani yetu
na kila aliepo ndani ya nchi yetu
Ameen 🤲🤲🤲
Hili ni jema,hongera Rais Samia.
 
ATAKAPOINGIA SEREKALINI NA VUGUVUGU LA UPINZANI LITAKUWA KWISHNEY.
Mbona Maalim Seif alishiriki katika serikali mbili tofauti za kitaifa na bado aliendelea kuwa mwiba mkali kwa watawala hadi siku ya kifo chake?

Unafikiri bila alhaj Jecha kufanya yake leo hii chama gani kingekuwa madarakani huko Zanzibar.

Ukiona mpinzani kalainika kwa sababu ya kushirikishwa kwenye serikali ya kitaifa jua huyo ni mchumia tumbo, na swala la serikali kalitumia kama kichochoro kutimiza malengo yake.
Peter Ngurunziza alishiriki katika serikali ya kitaifa huko Burundi, uimara wake na misimamo yake aliyoionesha hata pale alipokuwa katika serikali hiyo ya kitaifa vilimuwezesha kuchaguliwa kuwa raisi wa Burundi kwa mara ya kwanza mwaka 2006.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, natumai kila mtu ana afya tele.

Kwa dokezo lililonifikia kutoka kwa mtu ambae siwezi kumtaja, ni kwamba mama anamuandalia kamanda Mbowe nafasi nyeti na muhimu ndani ya serikali yake ili kujenga serikali yenye sura na mtazamo wa kitaifa.

Ikumbukwe kwamba raisi Samia aliwahi kunukuliwa akitamka mwenyewe kwamba serikali yake anayoiunda angependa kuona anashirikiana na wanasiasa wa vyama vingine vya siasa, ili kutengeneza serikali ya kitaifa ambayo haiegemei upande wowote wa chama.

Na katika hili raisi ameanza kuonesha njia kwa kujiweka mbali na siasa za majitaka, ambazo zimekuwa zikiwafaidisha wapuuzi wachache waliopo ndani na nje ya chama chake.

Mungu ilinde Tanzania yetu
Mungu mlinde raisi wetu
Mungu ilinde amani yetu
na kila aliepo ndani ya nchi yetu
Ameen [emoji2969][emoji2969][emoji2969]
Wewe jifanye tu unazo za ndani, watakuja wakubane korodani hizo unyooshe maelezo
 
Propaganda hizi hazita saidia nchi yetu kwani bado tuna matatizo mengi Sana.
Yatakiwa tujikite katika kujenga hoja ambazo zitasidia taifa letu lisonge mbele
 
Akipewa uwaziri tayari ameungana na serikali.
Hata kuwa na uwezo kuikosoa serikali ambayo yeye ni sehemu ya hiyo serikali.

Ubunge hauna mafungamano na serikali atakuwa huru kutoa maoni na kukosoa.
Iliwahi kufanyika enzi za JK kwa kumpa Mbatia na alifanya vuzuri bungeni sana tu hasa upande wa elimu alileta changamoto
Ubunge wa kupewa na Rais? Mbatia na kelele zake aliishia kuwa “lame duck” huko bungeni. Si JK, si Spika, si wabunge wa CCM; si serikali walikuwa wakimpuuza sana.

Ona kina Mdee. Hata wafurukute vipi, nobody gives a hoot. Hoja zile zile wangekuwa wanazitoa chini ya mwamvuli wa chadema bunge lingekuwa linachemka muda wote. Badala yake wanakumbushwa kumshukuru JPM na sasa SSH kwa kuwa kwao bungeni!
 
Mwaka 2015 nikiwa na ID nyingine kongwe niliwahi kuandika kuhusu Lowasa anapanga kukimbilia chadema baada ya kutemwa ccm. Wapo walionishambulia, walionipinga na walioandika kama wewe hivi. Vigezo vyao vilikuwa kwamba Lowasa ni fisadi kwahiyo isingekuwa rahisi kukubaliwa kujiunga na watu wasafi (chadema ya wakati huo) wengine walisema chadema kamwe hawezi kushirikiana na mafisadi papa kama vile Lowasa na wengineo, eti ni mara kumi chadema inaweza kushirikiana na mchawi lakini sio fisadi Lowasa.

Kifupi maneno yalikuwa mengi sana kwenye uzi ule, ila baada ya siku kidogo za usoni akahamia na cha kuchekesha zaidi akapewa nafasi ya kugombea uraisi. Nilivyofufua uzi nikakuta wengi wameshakimbia ID zao kutokana na aibu ya maneno yao waliyoandika kabla hajahamia chadema, wengine wakaanza kuandika visingizio mbali mbali ambavyo havikuwa hata na mashiko.

So kwahiyo hata wewe ulieandika hivi sikushangai, muda ukifika wa Mbowe kuteuliwa, wewe utapotea kama walivyopotea wale wa 2015. Hii ndio siasa ya bongo.
Unaamini suala la maridhiano ya CCM/CHADEMA 2022 ni copyright ya Lowassa kupokekewa CHADEMA 2015?
 
Lengo la kuteuliwa kwake sio kwa sababu ya njaa yake, bali ni kwa sababu ya kuwa na serikali yenye sura ya kitaifa bila kujali chama, rangi, dini, kabila nk.
Hiyo itakuwa serikali ya “compromise”. Haina manufaa kwa wananchi. Agenda na mikakati ya CCM ni tofauti na ya CHADEMA. Itakuwa ni njama za viongozi wa CCM na CHADEMA DHIDI yetu Watanzania.. A conspiracy of the politicians against the interests of the people.

Wananchi tunahitaji uhuru wetu wa kupima na kuchagua viongozi wenye maono, itikadi, sera, mikakati na mipango bora kabisa ya kutuwezesha kujiletea maendeleo na maisha bora kabisa nchini. SIO serikali compromised yenye “sura ya kitaifa” kwa ajili ya wapigaji! Hiyo “sura ya kitaifa” ya kisiasa/kivyama ni “fallacy” - batili!
 
SIO serikali compromised yenye “sura ya kitaifa” kwa ajili ya wapigaji!
Oh kumbe unaamini kuwa ikiundwa serikali ya kitaifa ambayo Mbowe yupo ndani yake kutakuwa na upigaji.

Kwa maana nyingine Mbowe nae atakuwa mpigaji kupitia kimvuli cha umoja huo, sawa umeeleweka.
 
Mbowe hana mkakati wa kugombea urais yeye kama yeye; ana mkakati wa kutoa Rais kutoka kwenye chama chake, yeye akiwa pembeni. Alishasema kuwa 2025 hatasimamisha mgombea, maana yake ni kwamba atajikita zaidi katika kutafuta wabunge. CCM wasipojiandaa vizuri 2025, idadi ya wabunge kati yao na CHADEMA itakuwa 50 by 50; na bado kuna ACT wazalendo nayo imeshakuja juu.
Njia wanayoweza kutumia CCM kumdhoofisha Mbowe, ni kuhakikisha kuwa wananzisha chama kingine kwa kivuli cha upinzani ambacho hata ikitokea mambo yakawa magumu 2030, wanahamia huko kisirisiri. CCM wao ndiyo wanatakiwa kuandaa chama ambacho watakuja kuwa tayari kukiachia madaraka. Mpaka muda huu, bado hatujawa na chama pinzani chenye uwezo wa kushika dola kwa usahihi kama wao
Hapa sina cha kuongeza. Nikimaanisha kuwa nakubaliana na mawazo yako mkuu.
 
Propaganda hizi hazita saidia nchi yetu kwani bado tuna matatizo mengi Sana.
Yatakiwa tujikite katika kujenga hoja ambazo zitasidia taifa letu lisonge mbele
Wewe ndo ungeleta sasa hizo hoja unazozitaka ili zijadiliwe, sio lazima wana JF wote zaidi ya laki tuliopo humu tuandike kitu kimoja kinachohusu hayo matatizo yako.

JF ni jukwaa huru ambalo kila mtu ana uhuru wa kuandika kile anachoamini na anachokipenda ilimradi mtu huyo asivunje sheria za nchi na za jukwaa hili.
 
Unaamini suala la maridhiano ya CCM/CHADEMA 2022 ni copyright ya Lowassa kupokekewa CHADEMA 2015?
Lengo langu ni kukuonesha kwamba usimuamini mwanasiasa kwa 100% , ni afadhali umuamini Mungu wako na wewe mwenyew. Unaweza kusema namuamini Mbowe hawezi kufanya hivi, mwisho wa siku akaja kufanya kilekile ambacho wewe umepinga kwa nguvu zako zote kuwa yeye hawezi kufanya.

Katika siasa lolote linaweza kutokea. Ndomaana nikakutolea mfano wa mwaka 2015 Mbowe alipokuwa anashangaa kwamba inakuaje vibaka wadogo wadogo wanachomwa moto, huku mwizi mkubwa na fisadi papa Lowasa akiendelea kupeta mtaani. Mwisho wa siku Mbowe huyu huyu alieshangaa vibaka kuchomwa moto huku Lowasa akidunda ndo akawa anapanda jukwaani kutaka watu tumchague Lowasa awe raisi wetu. Can you imagine that?

Ngoja nikuulize swali.. hivi mkuu kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, uliwahi kufikiri kwamba mtu aina ya Mbowe au Lisu wangeweza kupanda jukwaani kuwataka watanzania wamchague Lowasa kuwa raisi wa Tanzania?
 
Back
Top Bottom