Mbowe ashikiwa bango kutafuna milioni 800 za ujenzi wa ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA

Mbowe ashikiwa bango kutafuna milioni 800 za ujenzi wa ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA

Sasa ukweli utakuwa mara ngapi? magazeti yenu yasiyo na credibility yameandika sana. Mlianza na mla ruzuku wanachama ambao ndio wenye chama wakawapuuza, mkaja kamuua Chacha Wangwe mkapuuzwa na wote mahakama hadi familia ya marehemu, mmekuja na kalmia kwenye chanzo cha maji hadi mkafyeka shamba lake huku mnapiga selfie ili mpande vyeo na ikajulikana sio chanzo cha maji.
Hamkuishia hapo mmebomoa ukumbi wenye hadhi East and central Bills bado hajatetereka na chama kimesema kinamuamini leo mnasema kala 800m za kujenga jingo la ofisi. Hivi Mbowe angekuwa kazaliwa ukoo wa kimasikini kama huyo munayejaribu kumpendeza ingekuwaje? Huu mufanyao ni uduanzi wa kiwango cha reli ya SGR
Mbona unachanganya mada? Nilidhani tulikuwa tunachangia mada inayohusu tuhuma kuwa mwenyekiti CDM anajilipa fedha za chama kwa malipo ambayo hayathibitiki kimaandishi.
Tuendelee na mada yetu ila ukitaka mamba ya SGR fungua nyuzi yake na wachangiaji watafanya hivyo.
 
Dubai huwezi kununua nyumba kama wewe si mzawa.
Mnataka kumtoa kiongozi wetu kwenye mwelekeo wa kukijenga chama.
Ukweli kununua nyumba nje ya nchi siyo dhambi na kuna wengi tu wamefanya hivyo ila hoja hapa ni kwamba bwana mzee anajimilikisha maduhuli ya chama kwa matumizi binafsi.
 
View attachment 886186

Gazeti la Fahari Yetu limeandika tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, likimhusisha na matumizi ya milioni 800 za ujenzi wa jengo la ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Gazeti hilo limedai kuwa, Mbowe alikiuka Azimio la Kikao cha Kamati Kuu ya Chama na kuamua kutumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi. Inaelezwa kuwa:
  • Mbowe alinunua nyumba Dubai kwa fedha za Chama.
  • Michango ya watu binafsi kwa Chama kama akina Mzee Sobodo haijulikani zilichukuliwa lini na kwa mfumo gani na hatimaye kutumikaje.
  • Fedha zilizopatikana kupitia "Fund Raising Events" mbalimbali kama za Dar na Mwanza hazijawahi kuonekana.
  • Malalamiko kwa Mbowe kujilipa fedha kwa mnadai ya kukikopesha milioni Chama milioni 700.
  • Malalamiko dhidi ya Mbowe kukiuzia Chama magari chakavu kwa zaidi ya milioni 600 ambapo kabla ya kuyauza kwa Chama, alikuwa akiyakodisha kwa Chama.
  • Malalamiko kwa Mbowe kununua LandCruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama na kisha kukiuzia Chama.
  • Ripoti ya CAG ya 2016/2017 imeonyesha namna fedha za CHADEMA zinavyotafunwa na wajanja wachache.
Kulingana na Gazeti la Fahari, kila anapojitokeza Kiongozi yeyote ndani ya CHADEMA kuhoji juu ya matumizi ya fedha za Chama, wanajitokeza wapambe wake wa kumtetea kwa kutumia hoja za nguvu badala ya nguvu ya hoja. Hivyo kwa mtaji huo wa kujichotea fedha bila kuhojiwa ama kuulizwa chochote, Mbowe hawezi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa Chama.

View attachment 886175
hongera Mbowe, mm nawashangaa sana wanaokusema nadhani hawajui kuwa CHADEMA ni chama cha Baba Mkwe wako na ni Saccos yako, baba endelea kuzitafuna ila angalia maana ndani ya chama chako wamechoka na huo ulafi wako, jiangalie baba zama hizi sio zileeeeee
 
Ila Mbowe Sijui Aliwafanya Nn Ccm?
Labda hajawahi kumilki hata kadi ya CCM ndiyo maana. Na kama aliwahi kuwa na kadi ya CCM basi nadhani alikuwa anaichukulia kama tiketi ya kwenye daladala.
 
h
zile kamera kwenye tukio la kutaka kumtoa uhai kamanda LISSU mlizipeleka wapi
kaka tunataka mwenyekiti atueleze ukweli kwani hiz ni tuhuma nzito kwa kiongozi tunaemwamini na aneyejiita mpigania haki za Wtz
 
k
Gazeti hilo, Jamvi la habari na Tazama, wao huwa hawana habari zaidi ya aina hizo. Hata gazeti la Uhuru, huwa haliandiki habari za aina hiyo!

Wakati mwingine tuwe tunaelimishana wapendwa, kazi za vyombo vyombo vya habari , ni kuchunguza kuelimisha,kuburudisha na kuiambia jamii nini kinafanyika ndani ya jamiii. Hongera sana waandishi wetu
 
nyu

kweli kuongoza nyumbu raha jamani
Nyumbu mama yako, siyo? kama mwanadamu anazaa nyumbu , basi na mama yako ni nyumbu.. LIKE BEGETS LIKE! usikasirike simple logic dictates my writing!..
If A= B and
B=C, then, logically
A=C

Mchana mwema!
 
Ukweli kununua nyumba nje ya nchi siyo dhambi na kuna wengi tu wamefanya hivyo ila hoja hapa ni kwamba bwana mzee anajimilikisha maduhuli ya chama kwa matumizi binafsi.
Hivi wewe unaelewa kuwa mfumo wa fedha ndani ya vyama ni ule uliokubalika na CAG? acha hekaya zako Abunuasi, sasa hivi zinazo trend ni za #Kalumekenge na #Essopo
 
Hebu ingia humu ndani jamvini usome kutoelewana kati ya mheshimiwa chacha wangwe na uongozi mzima wa CDM[maana walimtenga na mwenyewe aliwahi kusema hivyo.] Hata hivyo waswahili husema 'KIPENDACHO ROHO, DAWA'
Kumbe una vielelezo? Peleka haraka polisi mummalize Huyo anaeikosesha raha CCM nzima.
 
Huyu jamaa tangu achukue mzigo kwa Lowassa hajawahi kaa sawa
There is no free lunch
Billions zimeliwa kwa gharama ya kifo cha chadema
Wenzie wanajua hilo ndio maana wanasepa mmoja mmoja
Hilo la rushwa nalo peleka polisi, takukuru, ili achukuliwe hatua. Hakuna haja ya kuendelea kujaza jf au kutungatunga tuhuma Kama Makonda.
 
Jamaa ni mpigaji mzuri,halafu sijui kwanini kama hana maslah binafsi ndani ya chama kwanini asiachie wengine nao wakiongoze chama especially wakati huu chama kikiwa kwenye crisis
Peleka ushahidi uliyonao polisi ili akamatwe ashitakiwe, aondoke afungwe. Muwe na raha. Hapo vipi??
 
Hii ndiyo raha ya kuongoza nyumbu wanachokijua ni kushangilia tu.

Piga pesa mbowe piga pesa
 
Hili Gazeti ni kwa nini linapenda kutumia neno "inadaiwa" kama habari zake ni za kweli? Ni kwa nini wasiseme kwamba wao kazi yao ni kuandika habari za kufikirika!?
Unategemea nini kutoka kwa Musiba mwenye fungus ya ubongo?
 
View attachment 886186

Gazeti la Fahari Yetu limeandika tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, likimhusisha na matumizi ya milioni 800 za ujenzi wa jengo la ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Gazeti hilo limedai kuwa, Mbowe alikiuka Azimio la Kikao cha Kamati Kuu ya Chama na kuamua kutumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi. Inaelezwa kuwa:
  • Mbowe alinunua nyumba Dubai kwa fedha za Chama.
  • Michango ya watu binafsi kwa Chama kama akina Mzee Sobodo haijulikani zilichukuliwa lini na kwa mfumo gani na hatimaye kutumikaje.
  • Fedha zilizopatikana kupitia "Fund Raising Events" mbalimbali kama za Dar na Mwanza hazijawahi kuonekana.
  • Malalamiko kwa Mbowe kujilipa fedha kwa mnadai ya kukikopesha milioni Chama milioni 700.
  • Malalamiko dhidi ya Mbowe kukiuzia Chama magari chakavu kwa zaidi ya milioni 600 ambapo kabla ya kuyauza kwa Chama, alikuwa akiyakodisha kwa Chama.
  • Malalamiko kwa Mbowe kununua LandCruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama na kisha kukiuzia Chama.
  • Ripoti ya CAG ya 2016/2017 imeonyesha namna fedha za CHADEMA zinavyotafunwa na wajanja wachache.
Kulingana na Gazeti la Fahari, kila anapojitokeza Kiongozi yeyote ndani ya CHADEMA kuhoji juu ya matumizi ya fedha za Chama, wanajitokeza wapambe wake wa kumtetea kwa kutumia hoja za nguvu badala ya nguvu ya hoja. Hivyo kwa mtaji huo wa kujichotea fedha bila kuhojiwa ama kuulizwa chochote, Mbowe hawezi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa Chama.

View attachment 886175
Kunukuu gazeti la kipumbavu ni upumbavu nao!
 
Back
Top Bottom