Pre GE2025 Mbowe: Makubaliano na Jeshi la Polisi yamefikiwa kuwa maandamano yataendelea kama yalivyopangwa

Pre GE2025 Mbowe: Makubaliano na Jeshi la Polisi yamefikiwa kuwa maandamano yataendelea kama yalivyopangwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapo kuna mamluki watatumwa makusudi na kufanya uhalifu ili ionekane makatazo ya kufanya maandamano yote hapo nyuma yalikuwa sahihi
Yes,
Ndio akili za wenye madaraka in third world countries ukiwakosoa unazimwa kama ANOLOGY KWENDA DIGITALLY
 
Kama maandamano yatafanyika bila kuzuiliwa nitampongeza sana mama.
Haya maandamano CCM huwa wanayapaisha wenyewe.

Hivi kwa mfano wapinzani wakitaka kufanya maandamano yao ya amani, na serikali ikasema itawapa askari wa kuwaongoza barabarani mwanzo mpaka mwisho, wapinzani wakafanya maandamano yao wakamaliza, kutatokea nini cha ajabu cha kuitishia CCM hivyo?

Kipi ambacho wapinzani watasema kwenye maandamano haya ambacho hawajasema au hawawezi kusema kwenye mitandao na mikutano yao?

Naona kama jitihada za kuyazuia ndiyo zinayapa press zaidi na kuyapaisha kiumuhimu haya maandamano.

Enzi za Kikwete, kuna siku Maxence Mello alishikwa na Polisi, kumbe Polisi walikuwa hata hawajatumwa, walikuwa wanajipendekeza tu.

Tukajioanga kinataifa kumulika udhalimu ule. Tukawaarifu "Committee for Protection of Journalism" New York City. Wakalishikia bango suala hilo kimataifa.

Kikwete akaambiwa kuna vijana wameshikwa na Polisi, Tanzania imeanza kuandikwa kwamba inaminya uhuru wa habari kwenye vyombo vya habari kimataifa.

Kikwete akasema waachieni mara moja, mimi hao vijana hawanisumbui na wala sijaagiza wakamatwe, hizi habari kwamba mmewakamata na Tanzania inaminya uhuru wa habari ndiyo zinanisumbua, msiipake matooe nchi yangu.

Max akaachiwa.

Yani, kwa Kikwete, ile zimazima ya Polisi ilikiwa imetengeneza tatizo kubwa kuliko kuachia mambo yaende tu.
 
Hata hivyo maandamano hayo hayakuwa kwenda kwake bali ofisi za UN kumshtakia yeye na serikali yake kuwa hasikilizi wenye mamlaka ya nchi ambao ni wananchi.
Wasaidizi wake walishayakemea na kuyalaani. Unawezaje kuamini kuwa sponsor ana utu iwapo wasaidizi wake wanakata funua mbele yake na hajali?
 
Haya maandamano CCM huwa wanayapaisha wenyewe.

Hivi kwa mfano wapinzani wakitaka kufanya maandamano yao ya amani, na serikali ikasema itawapa askari wa kuwaongoza barabarani mwanzo mpaka mwisho, wapinzani wakafanya maandamano yao wakamaliza, kutatokea nini cha ajabu cha kuitishia CCM hivyo?

Kipi ambacho wapinzani watasema kwenye maandamano haya ambacho hawajasema au hawawezi kusema kwenye mitandao na mikutano yao?

Naona kama jitihada za kuyazuia ndiyo zinayapa press zaidi na kuyapaisha kiumuhimu haya maandamano.
Lakini naona sasa hivi hali ni tofauti, wakubwa wote wako kimya.
Ngoja tuone.
 

Ameandika Mbowe katika ukurasa wake wa mtandao wa X;

"Team yetu ya Chama ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, Bara Mhe Benson Kigaila imekuwa na kikao na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum, Dar Es Salaam ACP Jumanne Muliro na timu yake kuhusiana na Maandamano ya Amani yanayopangwa na kuratibiwa na CHADEMA siku ya Jumatano, 24 Januari 2024.

"Makubaliano yamefikiwa kuwa maandamano yaendelee kama yalivyopangwa.

"Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa busara hii. Karibuni Watanzania wote, tuandamane kwa Amani."
Chalamila anazo hizi taarifa ?
 
Lakini naona sasa hivi hali ni tofauti, wakubwa wote wako kimya.
Ngoja tuone.
Rais kusema anataka 4Rs halafu kuachia maandamano ya amani kuzimwa atakuwa ana ji contradict.

Awaachie tu tujue tuna Iron Lady anayeweza kuhimili political criticism.

As long as maandamano ni ya amani, na fujo ni za maneno ya kisiasa tu, awaachie tu.

Ukubwa gunia la chawa. Huwezi kuongoza watu zaidi ya milioni sitini ukategemea wote wakupende.
 

Ameandika Mbowe katika ukurasa wake wa mtandao wa X;

"Team yetu ya Chama ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, Bara Mhe Benson Kigaila imekuwa na kikao na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum, Dar Es Salaam ACP Jumanne Muliro na timu yake kuhusiana na Maandamano ya Amani yanayopangwa na kuratibiwa na CHADEMA siku ya Jumatano, 24 Januari 2024.

"Makubaliano yamefikiwa kuwa maandamano yaendelee kama yalivyopangwa.

"Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa busara hii. Karibuni Watanzania wote, tuandamane kwa Amani."
Halafu tusikie wale wafanya usafi wa Chalamila wakileta zao
 
Kama maandamano yatafanyika bila kuzuiliwa nitampongeza sana mama.
Kwa hili mama ame score mno katika nyanja za Demokrasia na zile 4R nimeonekana kilichobaki ni kuondoa miswada baada ya serikali kutathmni sauti ya watanzania kupitia maandamano hayo.
 

Ameandika Mbowe katika ukurasa wake wa mtandao wa X;

"Team yetu ya Chama ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, Bara Mhe Benson Kigaila imekuwa na kikao na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum, Dar Es Salaam ACP Jumanne Muliro na timu yake kuhusiana na Maandamano ya Amani yanayopangwa na kuratibiwa na CHADEMA siku ya Jumatano, 24 Januari 2024.

"Makubaliano yamefikiwa kuwa maandamano yaendelee kama yalivyopangwa.

"Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa busara hii. Karibuni Watanzania wote, tuandamane kwa Amani."
Kwa hili nawapongeza polisi sababu sioni tatizo watu wakiandamana
 
Kwa kauli ya Dr. Joseph Kizito Mhagama hapa chini inaonesha bado anataka ukiritimba wa kutoa maoni kupitia Bunge ndiyo njia pekee sahihi.

Hii inaonesha kuwa bado mhimili huu wa dola bado unaishi kwa kujibainisha wabunge pekee ndiyo wanahaki ya kuzungumzia mustakhabali wa taifa letu


22 January 2024
Dodoma, Tanzania

MWENYEKITI KAMATI ya BUNGE AJIBU HOJA za CHADEMA -AMSHANGAA MBOWE - MNYIKA -LISSU "WANAJUA -WAZOEFU"....

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge hajakubali njia ya Maandamano kutoa maoni


View: https://m.youtube.com/watch?v=0ws8xgGKvhw

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Utawala, Katiba na Sheria, Dr. Joseph Kizito Mhagama leo Januari 22, 2024 amezungumza na vyombo vya habari ambapo ameeleza mchakato wa kupokea maoni ya wadau mbalimbali ya mswada wa sheria tatu zilizowasilishwa na Serikali mbele ya kamati hiyo ambapo sheria moja inayohusu uchaguzi ilifata wadau wengi vwaliojitokeza vikiwepo vyama vya siasa, asasi za kiraia na Taasisi zingine za dini

Mwenyekiti huyo akitoa ufafanuzi amesema ameshangazwa na kauli ya viongozi wa chadema kuwaambia watanzania na wafuasi wao kuwataka kuingia barabarani kufanya maandamano Kwa madai kuwa kamati hiyo imetupilia mbali hoja zao....
 

Ameandika Mbowe katika ukurasa wake wa mtandao wa X;

"Team yetu ya Chama ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, Bara Mhe Benson Kigaila imekuwa na kikao na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum, Dar Es Salaam ACP Jumanne Muliro na timu yake kuhusiana na Maandamano ya Amani yanayopangwa na kuratibiwa na CHADEMA siku ya Jumatano, 24 Januari 2024.

"Makubaliano yamefikiwa kuwa maandamano yaendelee kama yalivyopangwa.

"Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa busara hii. Karibuni Watanzania wote, tuandamane kwa Amani."
Asante sana kwa taarifa hii, tutashiriki kikamilifu.
Natoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia, baada ya kuusoma ushauri huu Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu
Atakuwa amekubaliana na ushauri huu. Hivyo sasa wito wangu huu Kufuatia Umuhimu wa Maandamano ya UKUTA: Nimehamasika, Nitashiriki, Tujitokeze kwa Wingi! Ila...!
Uendelee,

Haya shime, tujitokeze kwa wingi kushiriki maandamano muhimu sana haya.

P
 
Back
Top Bottom