Mbowe na genge lako, mnamtisha Amiri Jeshi Mkuu akitumia madaraka yake muanze tena kulalamika?

Mbowe na genge lako, mnamtisha Amiri Jeshi Mkuu akitumia madaraka yake muanze tena kulalamika?

Eti hatutokubali yaani wao ndiyo wanaona ndiyo wapinzani peke yao, wakati mwingine unaona sawa tul yue muhuni wa Hai alichokuwa anawafanyia.
Uwendawazimu dalili mojawapo ni kama unavyoropoka. Huna uwezo wa kujenga hoja?
 
Uwendawazimu dalili mojawapo ni kama unavyoropoka. Huna uwezo wa kujenga hoja?
Nani kakuambia nahitaji uwezo wa kujenga hoja uwezo huo anayo mfalme Mbowe, anasema eti hatupo tayari kumpa muda rais.
 
Mkuu hata Mimi naitaka Sana hiyo katiba lakini mtu hajamaliza hata siku Mia watu wakaanza kuhamasishana na kulazimisha mambo, yaani nikama wanatumia.

Mfumo dume Kwa mama Samia wanatumia.neno 'ASIPO, ASIPO' nini maana yake? Hilo siliafiki ana mengi ya kurekebisha likiwemo la katiba lakini Kwa mipangilio sio kulazimisha watakavyo wao
Asipo zao hazifanyi maamuzi ya kitaifa zisikusumbue yaani.
 
AFADHALI WAISLAMU TURUDI JF TUANZE MTETEA MWENZETU TENA. Ulikuwa umepotea toka ameingia Magufuli.


Wanaukumbi,

Hakuna Mtanzania mwenye akili timamu asiyetambua umuhimu wa Katiba Mpya; tunapishana sehemu ndogo sana ‘timing’ na vipaumbele vya kitaifa kwa sasa viwe ni 1. Katiba Mpya au kupambana na 2. Janga la Corona na 3. Kuinua Uchumi na hali za wananchi masikini?

Sisi Watanzania tumechagua muhimu 2 na 3.

Mbowe na wafuasi wako mnachekesha sana hivi mnataka rais wetu afuate mnachotaka nyie kwa maslahi yenu?

Rais akitumia madaraka yake kama katiba unavyomtaka mtaanza tena kulia kuwa Tanzania hamna demokrasia.

Nakushauri Mbowe, zile pesa mlizorudishiwa na mahakama jengeni ofisi kwanza ondokeni Ufipa mlilpopanga vyumba viwili hamna Mtanzania anaweza kuwaamini wewe na kundi lako.
 
Uongozi sio hisani, watu wa taifa hili wanalipa kodi kuwalisha na kuwavisha viongozi, uwajibikaji kwa watu hao ni lazima na muhimu.
Mbona hukuona hayo kipindi cha Mwendazake?!
Wacheni unafiki Mwendazake aliwakatia tuu kwamba KATIBA Mpya kwake no! Mkaufyata mama anasema mumpe mda mwamjia juu
 
Wewe nawe! CCM ni wa hovyo sana mara nyingi! Eti Maghufuli kafariki ndo umepata uwezo wa kuongea tena humu. Una maslahi binafsi yaliyojikita kwenye chama pengine na familia kuliko uzalendo wa Taifa
Ritz na THE BIG SHOW kwa kweli ni watu wa ajabu sana, watiifu kweli kweli!

Miaka kumi ya Kiwete walitamba humu hadi watu wakashindwa hata kukohoa.

Wakati wa dhalimu mwendazake wakawa kimya kama wamemwagiwa maji baridi!

Kaingia mama loo afadhali hata nzi huchukua taimu kupumzika huko kwenye dampo!!

Yaani jamvi walivyolihatamia...kula hapa hapa, kulala hapa hapa ohoooooo!

Ona sasa wanachofanya, eti wanamtaka mama afuate nyayo za jiwe.

Kwa mbali namuona na FaizaFoxy naye akijipanga kuingia vitani!

Kumtetea mama hata akisigina Katiba ya nchi sawa tu!
 
Nchi ni shwari imebadilika kuna uhuru wa kudai katiba kama tulivo pewa haki kwenye katiba ya sasa
Ingekua enzi za Jiwe wacha kuingia barabarani hata huu mkutano usingekuwepo.
Watu walishakimbilia Dubai , Belgium ,Canada,Kenya
Ingekua Jiwe yupo huu mkutano upo karibu na Segerea !
Upo sahihi. Kichaa akiingia na panga nyumbani mwako, wapo watakaokimbia nje ya nyumba, wapo watakaotafuta sehemu ya kujibanza ndani ya nyumba.

Nchi ilikuwa chini ya utawala wa shetani. Mama Samia, hata akosee vipi, hakuna muujiza utakaompeleka kufanana na dikteta aliyepita.

Dikteta alikuwa dhalimu kushinda kiongozi yeyote ambaye Taifa limewahi kuwa naye.

Mungu amjalie hekima Rais Samia, aongoze kwa haki, na wala asichukue ushauri wa baadhi ya mawakala wa shetani, masalia ya marehemu.
 
Toa hoja kama mtu mwenye akili yimamu. Hili ni jukwaa la walio na afya njema ya akili.
Hili jukwaa langu na zaidi ya miaka 15 humu tuanzie hapa.
Unakubaliana na Mbowe kumwambia rais hatupo tayari kukupa muda?
 
Punde si punde wataingia mabarabarani na wataanza vurugu za ajabu.

Wataanzisha mikutano isiyo na kibali kisa tu wamebip na kuona we dhaifu..
Bahati mbaya huelewi hata maana ya maendeleo.
 
Ritz na THE BIG SHOW kwa kweli ni watu wa ajabu sana, watiifu kweli kweli!
Miaka kumi ya Kiwete walitamba humu hadi watu wakashindwa hata kukohoa...
Rais Samia amekuwa tofauti na mtangulizi wake na kuna mabadiliko ameyafanya ndani siku 100 ikiwemo kumuondoa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai, Ole Sabaya aliyekuwa akilalamikiwa. Kumuondoa DPP, kuachia wafungwa ie. Masheikh Uamsho, tumeanza kuona mwanga wa Haki na Sheria.

Wewe ulivyikuwa na roho ya husda hautaki watu wampe pongezi.

Unataka kila mmoja akubaliane na Mbowe kila anachoongea.
 
Hilo la kuingia barabarani halitokaa litokee,just wait and see! Mama kawa fair sana lakini wao wanaanza kuleta dharau..Magu alikua sahihi sana ma.maaee..
Nampongeza sana Rais Samia kwa yale aliyoyafanya mpaka sasa.

Lakini suala la kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano, hapana. Kwa sababu anaenda kinyume na katiba.

Kusema katiba mpya isubiri kwa muda usiojulikana, hapana. Alistahili kueleza wazi kuwa ni lini anafikiria kufufua mchakato wa kupatikana katiba mpya. Katiba mpya ni muhimu sana. Utawala dhalimu wa Magufuli umetufunza hilo.

Kumfananisha Rais Samia au hata kumtaka afuate utawala dhalimu wa marehemu Magufuli ni kumdhalilisha. Utawala wa marehemu ulikuwa ni utawala wa kishetani ambao kila aliye wa Mungu hastahili kuuiga. Nina hakika, Rais Samia, hapa na pale, anaweza kukosea, lakini kamwe hatafanana na yule dikteta.
 
Mama Samia ndio kwanza anamaliza miezi 3 tangu apate urais
Ndani ya kipindi hicho tumeona mabadiliko mengi yanayohusu haki na uhuru ambayo watu wengi wapinzani na wananchi wa kawaida waliyalalamikia

Kutaja tu machache

Kuna kesi za kubambiza zaidi ya 147 zimefutwa

Vyama vya upinzani vimezunguka nchi nzima vikifanya mikutano ya ndani bila rabsha zozote kabisa

Vyombo vya habari vilianza kurudi, na hata kuandika kwa uhuru

Kuondolewa kwa watu kama Sabaya, ambaye yupo mahabusu kwa sasa na wengine kama akina Biswalo Mganga, DC Odunga. Chalamila n.k

Kuondolewa kwa utaratibu wa kukusanya kodi kwa mtutu wa bunduki

Wapinzani kushinda kesi zao ama rufaa za kesi ambazo walihukumiwa kipindi cha Magufuli

Kuachiwa kwa mashehe wa uamsho

Hata suala la katiba mpya alitoa lugha ya matumaini kidogo kuwa ni suala muhimu ila apewe muda, (tujilinganisha na Magufuli ambaye ali rule out kabisa)

Haya ni machache niliyoweza kukumbuka kwa haraka

Sasa kwa haya amewakwaza watu wengi ndani ya CCM ambao wanatja angefuata umagufuli

nilitarajia upinzani ungempa muda kidogo aendelee kurekebisha zaidi mengi,

Kwa hizi provocation walizoanza nazo Wapinzani ndani ya kipindi hiki kifupi, kutishia maandamano nchi nzima na mikutano ya kudai katiba, nadhani wale hardliners wa Magufulism watakuwa wamepata cha kumwambia, Samia kuwa, tulikuambia njia pekee ya ku deal na hawa watu ni Magufuli's way
 
Angalia vitu wanavyodai ndio utajua wapo kwa maslahi yao binafsi hiv nikuulize lini umewahi kuona Tundu lisu kajitolea kupambana kisheria kwa maslahi ya umma mfano kujitolea kisheria against mwananchi anayodai ardhi yake kuporwa na mengine kama hayo.
Tatizo hujielimishi. Waulize wenye ufahamu watakuambia TL amewasaidia wangapi kwenyeasuala ya kutafuta mahakamani, tena bila malipo. Na hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya wengine kuchangishana na kwenda kumwona hospitalini Nairobi.
 
Move calculated, Samia hataki kukutana na wapinzani kawawekea mtego, ili aone heshima zao ziko wapi, wapinzani watarudi sero tena, nawashauri ili pesa wasiitumie.
 
Amemuona mtangulizi wake alipewa ushauri wa kijinga kufanya alivyo fanya. Sasa atampata nani wa kuwa Sabaya?
 
Back
Top Bottom