Pre GE2025 Mbowe: Nikiona chama changu kinaenda kuzamishwa, Kamanda naingia mzigoni

Pre GE2025 Mbowe: Nikiona chama changu kinaenda kuzamishwa, Kamanda naingia mzigoni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mwenyekiti anaye maliza muda wake, Freeman Mbowe amesema ya kwamba iwapo ataona chama chake Cha CHADEMA kinataka kuzamishwa basi ataingia mzigoni. Kwa maana nyingine atagombea uenyekiti wa CHADEMA. Je nani anataka kugombea uenyekiti akizamishe chama.

Kwa kauli hii ya Mbowe Ina maana atagombea uenyekiti. Nadhani Mbowe anafikiri yeye tu ndio mwenye uwezo wa kuisimamisha CHADEMA. Wengine wataizamisha
aache hayo maneno isije ikawa kama utopwinyo kutaka kucheza na malaika sasa yanawakuta, chadema inavichwa vya maana kwanza kawachelewesha miaka yote hiyo chadema ingekuwa mbali kisiasa na kushika dola, astaafu kwa heshima
 
uzuri ni kwamba wote wanafanya kampeni ila kura ndio zitakazo amua nani awe mwenyekiti wa chama mbowe yupo sahihi Lisu yupo sahihi.
 
Nilikuwa natamani sana CCM kitoke madarakani na nilikuwa nadhani CHADEMA wana nia ya dhati ya kuitoa lakini kwa tanayoendelea kwenye chama nafikiri hata jina la chama libadilike. Huwezi ukatuaminisha ni chama cha demokrasia wakati akijitokeza mtu mwingine kugombea anaonekana ni haini ndani ya chama.

Nilitamani sana mwenyekiti Mbowe aachie watu wengine wakiongoze chama maana Mbowe kazoeleka mno tunahitaji watu wengine ambao sio ma puppet ambapo kwa kweli Lissu hata kama utamuua lakini sidhani kama anaweza kuitumikia Ccm.

Dhana ya chama cha wachagga nadhani inaenda kudhihirika rasmi na kufanyiwa figisu kwa Lissu kutapunguza sana wanachama na wapenzi wa Chadema.
Well said,na hili linakwenda kukizamusha kabsa hiki chama,hususan ktk uchaguzi ujao
 
Akiona chama chake kinazamishwa kamanda anaingia mzigoni, hiyo kauli inaashiria atagombea tena
 
aache hayo maneno isije ikawa kama utopwinyo kutaka kucheza na malaika sasa yanawakuta, chadema inavichwa vya maana kwanza kawachelewesha miaka yote hiyo chadema ingekuwa mbali kisiasa na kushika dola, astaafu kwa heshima
kasema ataingia mzigoni
 
Mwenyekiti anaye maliza muda wake, Freeman Mbowe amesema ya kwamba iwapo ataona chama chake Cha CHADEMA kinataka kuzamishwa basi ataingia mzigoni. Kwa maana nyingine atagombea uenyekiti wa CHADEMA. Je nani anataka kugombea uenyekiti akizamishe chama.

Kwa kauli hii ya Mbowe Ina maana atagombea uenyekiti. Nadhani Mbowe anafikiri yeye tu ndio mwenye uwezo wa kuisimamisha CHADEMA. Wengine wataizamisha
Kama chama kikizama yeye atakuwa mtu kwa kwanza kulaumiwa, so awe makini kuona ni nani anaweza kuwa mwenyekiti atakayekisogeza chama mbele.

Hata Mwalimu Nyerere aliingilia kati 1995 alipoona wahuni wanataka kuukwaa Urais wa nchi pale Dodoma - so Mbowe yupo sahihi.
 
Mwenyekiti anaye maliza muda wake, Freeman Mbowe amesema ya kwamba iwapo ataona chama chake Cha CHADEMA kinataka kuzamishwa basi ataingia mzigoni. Kwa maana nyingine atagombea uenyekiti wa CHADEMA. Je nani anataka kugombea uenyekiti akizamishe chama.

Kwa kauli hii ya Mbowe Ina maana atagombea uenyekiti. Nadhani Mbowe anafikiri yeye tu ndio mwenye uwezo wa kuisimamisha CHADEMA. Wengine wataizamisha
Anafanya chama kama chake binafsi,apishe wengine waongoze…Hivi watu dizaini hii ndio kweli tuje tuwape nchi yetu?
Juzi naona maiigizo tu eti watu wameenda nyumbani kwake kuomba agombee,hv watu wanaokuja bila taarifa unawaandalia kabisa hema na viti?
 
Chadema ibadilishwe jina, iitwe Mbowe Saccos
inawezekana ikawa hivyo. Ujerumani kuna mtu kaanzisha chama cha siasa kinaitwa jina lake. Labda tumuongezee majina achague. Mbowe alliance party, congress party of mbowe, mbowe democratic party of tanzania, majina ni mengi ni bora ajimilikishe chama tu ijulikane ni mali yake
 
Hili kwa sasa liko wazi, CDM itabaki sana sana Uchagani, na Mboyee akishinda tutegemee by 2035 CDM ikiwa Hoi na CCM ikijiimarisha zaidi.

I second this!
inasikitisha kwa kweli. Act wazalendo wajiandae kupata wabunge wawili watatu pahala pa chadema, chadema ndio basi tena kama mbowe ataendelea kuwa mwenyekiti
 
Chadema walipokuwa machachari kutetea wananchi maccm yalikuwa yanajibu mapigo yanasema chadema ni chama cha mbowe. chadema ni chama cha wachaga mpaka yakawa yanaiita chagadema.Nilikuwa naona kama maccm yamekosa hoja, kumbe yalikuwa na hoja. Hizi rasha rasha za uchaguzi wa ndani wa Chadema zimenipa nafasi ya kuijua chadema.


Endapo Mbowe ataendelea kuwa mwenyekiti , wananchi hawatakuwa na imani na chadema na chadema itapotea .

Chadema inajipambanua kama chama cha mtu binafsi na kwa mbali naona pia chadema inajipambanua kama chama cha kikabila kama maccm yanavyosema.
 
Ama kweli CHADEMA ni chama cha Mbowe na CCM ni Chama cha Wananchi!
ametoa kauli mbaya sana hivi ingetokea mwana ccm mstaafu atamke kuwa akiona chama chake kinazama ataingia mzigoni ataeleweka vipi? Huo ni uhaini
 
Back
Top Bottom