Mbowe: Nimewasikiliza Rais Magufuli na Spika Job Ndugai. Nimesikitika, tunatafakari! Nitazungumza tena na Taifa wakati wowote

Kwani ni kosa mtu especially kiongozi wa Upinzani kuongea na Waandishi wa Habari ?

Au hilo neno Taifa ndiyo lenye kuleta nongwa?

Mbona tangu kuanzishwa kwa vyama vingi imekuwa ikifanyika hivyo?

Je Katiba inasemaje kuhusu Uhuru wa watu kukusanyika na kujadili jambo au mambo ?




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo bosi wenu Chakubanga anavyowadanganya
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu wajinga sana nchi hii. Ngoja niwaulize nyie mnaounga mkono mbowe watu wasiende bungeni. Kumbukeni kuna madaktari, mama ntilie, rais, mawaziri, wahasibu, tra, bandari, msd, vyuo, madereva, vituo vya mafuta, wote ni binadam hawa wote wakiacha majukumu yao na kuja kukaa kwa kuogopa corona mnafikiri maisha yatakuwa aje. Mbowe kafeli pia na kwa hili kama anavyofeli kwenye move zake zote zilizopita. Saiz cdm inafukuta kwa joto wabunge wanataka kurudi bungeni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahahaha
Ati Mbowe anazungumza na Taifa!
Kumbe na wewe ni kibibi cha hovyo! Kwani kati ya Jiwe na Mbowe nani mwenye weledi? acha mtu kutegemea jeshi, vifaru risasi. Waweke kwenye mzani wa uraiani in terms of upstairs!
 
Ila jamaa sio mtu mzuri. Anasema corona haitishi wakati yeye amekimbia.
Ukisikia usaliti ndiyo huo. Unayaona maisha yako ni ya thamani kubwa, ya wenzako hayana thamani, hata yakitoweka ni sawa. Na bado kuna wendazaimu wanaona ni sawa, na wanashabikia.

Kwa nini usiwashauri watu wachukue tahadhri kubwa kama unavyofanya wewe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijaelewa hapo.Anaongea na Taifa yeye kama nani?
 
Kumbe na wewe ni kibibi cha hovyo! Kwani kati ya Jiwe na Mbowe nani mwenye weledi? acha mtu kutegemea jeshi, vifaru risasi. Waweke kwenye mzani wa uraiani in terms of upstairs!


Mbowe alipata daraja la mwisho kabisa kwenye Elimu ya TZ yaani division 0, hivyo Mbowe ana low IQ kwa mujibu wa matokeo yake, ni ajabu mmefanya kuwa Kiongozi wenu, Mbowe hana uwezo wa kutuma maombi ya kazi popote na kujibiwa kwani IQ haitoshi, ameweza tu kuwa Kiongozi wa chadema shauri ya Upendeleo kwamba kaoa Mtoto wa Mtei ambaye ni Mwanzilishi wa chadema, hivyo kawekwa hapo kwa nguvu lakini siyo kwa merit, ...
 
Safi sana kamanda. Kuna mtu kajichimbia chato anachezea uhai wa watz lazima aambiwe ukweli sasa sio kesho......
Hii ni serikali ya KISHETANI
 
Mbowe kweli anazeeka vibaya,

Kwa siku za hivi karibuni amekua akitoa hotuba utafikiri ni mtu mwenye instruments za kumuwezesha kutekeleza anachokisema, yaani kwa ufupi amejipa mamlaka ambayo hana.
 
Kuzungumza na taifa?? Interesting...Yaani Mhe. Mbowe eti anadai atazungumza na taifa?? Mmmh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…