Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,404
- 6,969
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe ametangaza kujiuzulu kufanya siasa endapo Chama cha Mapinduzi (CCM) kitashinda angalau kiti kimoja tu cha jimbo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro wenye majimbo tisa (9) ya uchaguzi.
Mbowe ametangaza ahadi hiyo Julai 05.2024 wakati akizungumza na wakazi wa Maore, wilayani Same, mkoa wa Kilimanjaro kwenye muendelezo wa mikutano ya hadhara ya chama hicho inayolenga kufikia mikoa yote ya kanda ya Kaskazini ikiwa ni muendelezo wa 'oparesheni +255 Katiba mpya' ambapo amesema msingi wa kuweka ahadi hiyo ni kutokana na ukweli kwamba mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya Kaskazini kwa ujumla wake CHADEMA imekuwa nguzo imara mara zote.
Ametolea mfano uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo CHADEMA chini ya mwavuli wa UKAWA (Umoja wa Katiba ya Wananchi) uliohusisha vyama vingine vitatu (3) wakati huo vya CUF, NCCR Mageuzi na NLD, vyama vya upinzani vilishinda majimbo saba (7) kati ya tisa (9) ya mkoa wa Kilimanjaro.
Ametaja majimbo yaliyochukuliwa na upinzania kuwa ni pamoja na Same Mashariki, Rombo, Vunjo, Moshi vijijini, Moshi mjini, Hai na Siha, huku CCM ikiambulia majimbo ya Mwanga na Same pekee, hivyo kutoa wito kwa wakazi wa Same na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla wake kujipanga sawasawa ili kurejesha heshima hiyo kwa kuhakikisha wanashinda sehemu zote kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu (2024) na uchaguzi mkuu mwakani (2025)
Kuhusu mkoa wa Arusha, Mbowe ameeleza kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 CHADEMA iliibuka kidedea kwenye majimbo sita (6) kati ya saba (7) yaliyoko mkoani humo, ambapo CCM iliambulia jimbo moja (1) pekee ambalo ni la Ngorongoro, jambo ambalo amedai kuwa haoni dalili ya CCM kushinda tena kwenye jimbo hilo kwa kuwa wakazi wa Ngorongoro wameahidi kuipigia kura CHADEMA kutokana na kile alichodai kuwa shukrani ya chama tawala (CCM) na serikali yake baada ya kuchaguliwa ni kuwahamisha watu wa jamii ya Masai kutoka kwenye eneo lao la asili na kuwapeleka Msomera, wilayani Handeni, mkoani TangaAidha, kwa upande wa mkoa wa Tanga.
Mbowe amebainisha kuwa mkoa huo umekuwa ngome ya CCM kwa miaka mingi kwani katika majimbo 12 ya uchaguzi yaliyopo mkoani humo CCM ilikuwa inashinda majimbo yote, hata hivyo amedai kuwa kufuatia mikutano 72 aliyoifanya hivi karibuni kwenye mkoa huo tathmini ya CHADEMA inaonyesha kuwa majimbo pekee ambayo CCM inaweza kushinda ni matano (5) tu huku CHADEMA ikiwa na uhakika wa 'kunyakua' majimbo yote yaliyosalia ambayo ni saba (7).
Mbowe ametoa wito kwa wakazi wa Same, mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya Kaskazini kwa ujumla wake kuhakikisha wanashinda chaguzi zote zijazo, yaani kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji baadaye mwaka huu (2024) na uchaguzi mkuu mwakani (2025) kuanzia kwenye viti vya Madiwani ili waweze kuunda Halmashauri, Wabunge na hatimaye nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kile alichodai kuwa chama hicho kinaenda kuunda serikali baada ya uchaguzi mkuu wa mwakani (2025).
Mbowe ametangaza ahadi hiyo Julai 05.2024 wakati akizungumza na wakazi wa Maore, wilayani Same, mkoa wa Kilimanjaro kwenye muendelezo wa mikutano ya hadhara ya chama hicho inayolenga kufikia mikoa yote ya kanda ya Kaskazini ikiwa ni muendelezo wa 'oparesheni +255 Katiba mpya' ambapo amesema msingi wa kuweka ahadi hiyo ni kutokana na ukweli kwamba mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya Kaskazini kwa ujumla wake CHADEMA imekuwa nguzo imara mara zote.
Ametolea mfano uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo CHADEMA chini ya mwavuli wa UKAWA (Umoja wa Katiba ya Wananchi) uliohusisha vyama vingine vitatu (3) wakati huo vya CUF, NCCR Mageuzi na NLD, vyama vya upinzani vilishinda majimbo saba (7) kati ya tisa (9) ya mkoa wa Kilimanjaro.
Ametaja majimbo yaliyochukuliwa na upinzania kuwa ni pamoja na Same Mashariki, Rombo, Vunjo, Moshi vijijini, Moshi mjini, Hai na Siha, huku CCM ikiambulia majimbo ya Mwanga na Same pekee, hivyo kutoa wito kwa wakazi wa Same na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla wake kujipanga sawasawa ili kurejesha heshima hiyo kwa kuhakikisha wanashinda sehemu zote kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu (2024) na uchaguzi mkuu mwakani (2025)
Kuhusu mkoa wa Arusha, Mbowe ameeleza kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 CHADEMA iliibuka kidedea kwenye majimbo sita (6) kati ya saba (7) yaliyoko mkoani humo, ambapo CCM iliambulia jimbo moja (1) pekee ambalo ni la Ngorongoro, jambo ambalo amedai kuwa haoni dalili ya CCM kushinda tena kwenye jimbo hilo kwa kuwa wakazi wa Ngorongoro wameahidi kuipigia kura CHADEMA kutokana na kile alichodai kuwa shukrani ya chama tawala (CCM) na serikali yake baada ya kuchaguliwa ni kuwahamisha watu wa jamii ya Masai kutoka kwenye eneo lao la asili na kuwapeleka Msomera, wilayani Handeni, mkoani TangaAidha, kwa upande wa mkoa wa Tanga.
Mbowe amebainisha kuwa mkoa huo umekuwa ngome ya CCM kwa miaka mingi kwani katika majimbo 12 ya uchaguzi yaliyopo mkoani humo CCM ilikuwa inashinda majimbo yote, hata hivyo amedai kuwa kufuatia mikutano 72 aliyoifanya hivi karibuni kwenye mkoa huo tathmini ya CHADEMA inaonyesha kuwa majimbo pekee ambayo CCM inaweza kushinda ni matano (5) tu huku CHADEMA ikiwa na uhakika wa 'kunyakua' majimbo yote yaliyosalia ambayo ni saba (7).
Mbowe ametoa wito kwa wakazi wa Same, mkoa wa Kilimanjaro na kanda ya Kaskazini kwa ujumla wake kuhakikisha wanashinda chaguzi zote zijazo, yaani kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji baadaye mwaka huu (2024) na uchaguzi mkuu mwakani (2025) kuanzia kwenye viti vya Madiwani ili waweze kuunda Halmashauri, Wabunge na hatimaye nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kile alichodai kuwa chama hicho kinaenda kuunda serikali baada ya uchaguzi mkuu wa mwakani (2025).