Pre GE2025 Mbowe siyo mwanademokrasia, kwanini amesusa kuwakabidhi ofisi Lissu na Heche?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Annunaki

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2021
Posts
2,042
Reaction score
3,674
Katika hali ya kushangaza, Mbowe hajatokea kabisa leo Katika tukio la kitaifa la kumkabidhi ofisi Lissu.

Kwa hali ilivyo ni kama uongozi uliopita umekomba kila shumuni kutoka kwenye akaunti ya chama kabla ya kubwaga manyanga.

Mbowe siyo mwanademokrasia kabisa, mnaomsifu mnampaka mafuta kwa mgongo wa chupa tu.

Uongozi mpya unatakiwa kuwa makini sana wale wote wanaopanga kuhujumu na kukwamisha chama waondolewe kwenye chama haraka sana kabla hawajapata muda wa kukivuruga chama.

Umma una matumaini makubwa sana na uongozi wa Lissu kuelekea kuiondoa CCM madarakani 2025.

Soma, Pia: Tundu Lissu, John Heche na viongozi wengine wapokelewa Ofisi za CHADEMA Makao Makuu. Wasisitizia No Reform, No Election
 
Kwa hiyo wakaamua kujikabidhi si ndio? 😁😁
 
Kwa kweli kwa matusi yale hata mimi nisingeenda. Maana Mbowe aliambiwa mpaka watu wanaotekwa yeye ndio anawauza kama alivyouza chama kwa Mama Abdul. So sad!
Hiyo siyo demokrasia anayo ihubiri.
Mbowe ni mtu mwenye kisilani, kwa ukomovu wake wa demokrasia mnaomsifia nao alitakiwa amkabidhi ofisi Lissu.
 
Kwani kazi ya katibu mkuu ni nini?
 
ukisema kuiondoa ccm madarakani unaharibu, watapenda mgogoro uendelee
 
Ufafanuzi huu kashautoa KM - Mnyika muda mchache ukiopita.
 
Lusungo Fundi Mchundo Retired Quinine Ngongo mwambieni Mbowe akabidhi Ofisi na mali za chama kwa Mwenyekiti mpya.
 
Lissu akaze sana, lakini atakutana na hujuma nyingi kutokea ndani ya chama chake.
Chama kile ni 'kichafu' na hata ambayo wanayakosoa kutoka mbogamboga yapo ndani mwao.
Mtu mwadilifu kama Lissu hatakiwi kwa kuwa wanaona mishe zao za giza zitakwama.

Watu walishazoea kuzua taharuki ili serikali iwaite, wa-negotiate, kisha wapate mpunga!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…