Mbowe: Tozo ya benki, wafanyakazi wanakatwa kodi mara mbili, wanaotoza kodi wanaenda kununulia V8 ya milioni 450 au milioni 500

Mbowe ameshazungumza kuonesha msimamo wake, ajabu nyie bado mnaamini hisia zenu, hebu acheni kuishi kama mnatembea barabarani huku mnaota ndoto mchana wa jua kali, amkeni!.
Muda wote alikuwa wapi mpaka anaongea sasa hivi au kaona kule kwenye bank kumemgusa mimi ndio maana siwaamini Wanasiasa wote wapo kimaslahi tofauti yao ni Moja mmoja yupo madarakani mwingine anasaka madaraka kwa kutumia matatizo ya wananchi
 
Kama ni hivyo angeweza pia kuamua kukaa kimya tu badala ya kuhadaa watu ambao tayari wana shida na wanaumia, siyo vizuri kumkejeli mtu ambaye anataabika tayari!
Wewe unayewaza ujinga ndiye unayewaza hivyo ila wenye busara wanajua kaongea mambo ya msingi.
 
Iitaridhisha kuona upinzani wa Mbowe upo imara ikiwa atailazimisha serikali kuruhusu mikutano ya kisiasa ambayo si ya kujificha mahala.

Pili, itaridhisha serikali ikikiruhusu chama cha Umoja kuendelea na shughuli zake za kisiasa na wanachama wake kuendelea kusambaza ujumbe ulobeba malengo na dhamira ya chama hicho.

Tatu, serikali kupitia TCRA iwaruhusu wale wanojitoa kuwaelimisha watanzania juu ya haki zao na mfano mmoja ni Humphrey Poleople arudishiwe tovuti na mtandao wake wa Shule ya Uongozi.

Nne, Tundu Lissu, Zitto Kabwe na wapinzani wengine wote wajiunge pamoja wakitoa kauli za kweli za upinzani na sio kukaa kimya baada ya Lissu kupoozwa au Zitto Kabwe kujipooza mwenyewe kwa kauli yake ya kijinga kwamba "watu wanomuenzi hayati JPM wakazikwe nae kule Chato".

Tano, serikali iruhusu mchakato wa katiba mpya uendelee kwa kuwapa nafasi wananchi wapige kura ya maoni. Wananchi wakiamua tubadili katiba inakuwa kheri la wakikataa hiyo pia yawa ni uamuzi wa wengi na itasemwa kuwa tumejaribu.

Serikali ionekane yakubali kupingwa au kukosolewa kwa staha bila kuchukua hatua kali za kuwaadhibu raia wake kwani wanatumia haki yao ya kikatiba ya kutoa maoni.

Hiyo iendane na kumuachia yule kijana wa TRA aendelee na maisha yake bila kubugudhiwa kwani ametumia haki yake ya msingi ya kutoa maoni ambayo kiukweli haiwezi kuiangusha serikali au kuikebehi bali inaipa mwamko wa kufikiri zaidi juu ya hizi tozo za zaida.

Nchi ikiwa na watu wenye mawazo tofauti ndo huwa chachu ya kuleta maendeleo kwani kiujanja serikali inakuwa yatumia mawazo ya wapinzani kutekeleza mipango yake.

Ni dhahiri serikali imeshindwa kukusanya kodi na fedha zinokusanywa kama ushuru katika mikoa yote ya Tanzania zinaibwa. Kwa mfano Waziri mkuu Kassim Majaliwa alipokwenda kwenye moja ya halmashauri nchini alikuta kuna mchezo wa kuonyesha mapato ya milioni 2 hadi 3 lakini kumbe kuna zaidi ya fedha milioni hadi 4 na nusu hio kuonyesha kwamba badoi upogaji upo na wafumbiwa macho.

Serikali iketi tena na washauri wake wa uchumi kutathmini hizi tozo zisizo na maana ambazo zinaumiza wananchi.

Kisha serikali ikazanie kukusanya kodi kwa kila afanyae biashara halali nchini na iwe ni sheria kwamba ukikutwa unakwepa kodi basi kuna adhabu ya malipo zaidi.

Hata TRA wakikuta mtu hajalipa kodi ni wajibu wao kuketi na mtu huyo ili wapange namna ya kulipa "arrears" hizo kwa awamu hadi amalize lakini lengo likiwa lilelile kuhakikisha kila mtanzania mwenye shughuli za kuingiza fedha alipa kodi.

Mbona masuala haya ni rahisi sana kuonekana kwenye macho ya watanzania?, miaka mitano ilopita Tanzania iliweza kufikia uchumi wa kati ya kusifiwa hata na hao IMF na Benki tya Dunia, leo hii imekuwaje tena serikali imebadili gia angani na kuharibu kila chema kilichobuniwa na kiongozi aliepita?

Hakika sasa Mbowe kaibuka na ametoa neno na aungwe mkono na hii iwe twasema kwa kiingereza "Moment of truth" au wakati wa kufanya kweli.
 
Siku hizi kuweka fedha bank imekuwa si kimbilio tena. Pesa ikikaa muda bila kufanyiwa transaction yoyote unakuta imekatwa bila sababu ya msingi na maelezo yasiyojitosheleza, imekuwa sawa na kuweka salio kwenye simu(voda) na uliache bila kujiunga! Wanakukata kwa lazima! Ili utafute ya kujazia
 
Maneno MAZITO....Kiongozi anaongea TAIFA zima LINAMSIKILIZA....
 
Kuonyesha Chadema tunapinga matumizi ya ma V8 serikalini, tulimbembeleza Mbowe asikubali kupokea gari hili kwani lingefifisha kelele zetu hakutusikia. Leo kalirudisha ndio akumbuka kumbe alikuwa anatembelea gari litokanalo na kodi za wananchi.
 

..hoja yako inafikirisha.

..naunga mkono katiba mpya.

..lakini pia lazima tuchague Raisi na wabunge kwa namna ambayo itawezesha mfumo na katiba kufanya kazi.

..tuige mfano wa Wamarekani. Wao wakichagua Raisi toka Democrat, basi bungeni huchagua Republican wengi zaidi.

..Ni lazima tujenge utamaduni wa kuwawajibisha na kuwabadilisha viongozi wanaopigiwa kura.
 
Anaongea nini huyo nae, atulie hakuna wa kumsikiliza.
Angekuwa ni mtumishi wa umma ndiyo kasema hivi! mngemfukuza kazi, mngemkamata na kumfungulia mashtaka ya utovu wa nidhamu, na bla bla nyingine!

Ila kwa huyu jamaa; mtafyata tu mikia yenu. Maana mkijiroga tu kumkamata, mnajua fika shughuli ya akina Kibatala na wenzake.
 
Siamini tena CHADEMA kuanzia pale mulipomuuzia lowassa chama chenu, hadi kuwapoteza zitto na slaa, siasa za tz ni za ovyo sana. usimwamini mwanasiasa. amini nakuambia
 
Uchaguzi wa Kenya hauna mizengwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…