Mbowe usimwachie Lissu chama kwa utovu huu wa nidhamu, afadhali kifie mikononi mwako maana kilitokana na mikono yako na wananchi wenye nidhamu

Mbowe usimwachie Lissu chama kwa utovu huu wa nidhamu, afadhali kifie mikononi mwako maana kilitokana na mikono yako na wananchi wenye nidhamu

Hizo lugha za kuficha ficha ndio zimekifikisha ccm kuwa chama kinachoongozwa kwa nidhamu za woga na unafiki. Kama neno muongo sio neno sahihi, liko kwenye kamusi ya kiswahili ili litumike wapi na kwa nani?
Neno muongo ni neno sahihi ila lina bad connotation, kumuita mtu muongo inaonekana ni habitual layer, ukisema hakuwa sahihi unamaanisha ni mkweli ila hapo ndio amekosea.

Ni kama demu wako kuchepuka mara moja tuu, huwezi kumwita malaya, utamuita amekosa auaminifu, kumwita malaya maana yake ni tabia na kjiuza!.
P
 
Mbowe toka aseme CCM oyeeee nilijua Tu mambo yameshaharibika , nikajua Yuko chadema lakini anawaza Sana ccm yake
 
Kwa mwendo huu wa Lisu, atakiuza chama kwa Msigwa. Usiachie chama , lilwalo na liwe. Aanzishe chake na Heche wake!

Na kwa kuropoka kwake, kutokuwa na kaba ya ulimi dola itakifuta. Samia atakifuta kwa sababu ambazo kila mmoja atazikubali na si kukionea.
Kitila aliondoka, Zito aliondoka, Dr. Slaa akaondoka, Msigwa akaondoka, Seleman Bungala akaondoka na wengine wengi. Hao wote hawana nidhamu? Kwamba Mbowe tu ndio sahihi?
 
Kwa mwendo huu wa Lisu, atakiuza chama kwa Msigwa. Usiachie chama , lilwalo na liwe. Aanzishe chake na Heche wake!

Na kwa kuropoka kwake, kutokuwa na kaba ya ulimi dola itakifuta. Samia atakifuta kwa sababu ambazo kila mmoja atazikubali na si kukionea.
Madogo kama kina David Silinde wa Momba, Yule wa Shinyanga, Ally Bananga wa Arusha, tumbili wa PPP wote wako wrong ila Mbowe yuko sahihi! Maajabu!
 
Hicho ndio tunachompendea Lissu, amenyoka hana konakona. Kama wewe ni muongo atakuita muongo bila kujali cheo chako.
Hii tabia ya Lissu kuwa ropo ropo ni a very bad liability kwa kiongozi!. Anahitaji civility!. Hebu msikie hapa, anawaita wenzake wajinga!. Msikie Tundu Lissu Hapa, Anauliza Kama Wenzake Wana Akili Kweli! Maridhiano Ayaita Ujinga. Je, Lissu Bado ni Asset or Sasa ni A Liability?
View: https://youtu.be/Qa59DIQs2yI
Anajua huyo anayeitwa mjinga ni nani?.
Ila huu uropo ropo wa Lissu, japo ni a bad liability kwa kiongozi, ndio asset ya kuibamiza CCM na kuiingiza Chadema ikulu kwa kura za GenZii. Japo Lowassa Alikuwa a Liability CCM, Akawa Asset Chadema. Lissu is a Very Bad Liability, but is The Only Asset Chadema Has Kuwangiza Ikulu!. Je... ?

Wakati huu wa uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura, ukiendelea, huu ndio ungekuwa wa amsha amsha GenZii wajiandikishe kwa wingi kwenye daftari, lakini Chadema viongozi wako busy kutukanana na kupigana vijembe, muda wa uchaguzi ukifika, mikutano yao inajaa nyomi za watu, GenZii, lakini siku ya kupiga kura, hawaonekani!, kumbe hawakujiandikisha!.

P
 
Kwa mwendo huu wa Lisu, atakiuza chama kwa Msigwa. Usiachie chama , lilwalo na liwe. Aanzishe chake na Heche wake!

Na kwa kuropoka kwake, kutokuwa na kaba ya ulimi dola itakifuta. Samia atakifuta kwa sababu ambazo kila mmoja atazikubali na si kukionea.
mbowe anatakiwa kuongea uwongo
Lema amegoma kabisa alichokifanya mbowe hapo
 
Kwani mbowe ndiye anaaamua chama amuachie nani au wanachama ndio watachagua nani wanamtaka siku ya uchaguzi? Mbona hii kauli yako inataka kuchorea mstari madai ya kwamba chana ni cha mtu na sio wanachama? Au umekosea.
Mbowe huyo kachanganyikiwa
 
Nilipooma uwezo umeshuka wa kuchambua pale uliposema afadhali kifie mikononi mwako, hebu tuambie dhamira ya post yako ni nini?

Kwamba Lissu hafai kugombea uenyekiti wa CHADEMA? Na kama hafai kuna wanachama wa CHADEMA ambao wanayo nafasi ya kuchagua mwenyekiti wao kwa nini usiwape nafasi wachague wanayeona anafaa?

Kwa nini kife? Tena kifie kwa Mbowe? kwa nini kisfie kwa Lissu? Mada fikirishi ukifikiria sana kuna hoja za kibandibangi hapa.
 
Lissu Yuko smart Sana,
How? amefanya nini tangible politically tangu aingie kwenye siasa? Kuropoka? huyo ni msaliti as put by Magufuli. Anamsaliti Mbowe! Sina neno na Mbowe kuachia madaraka, my concern ni the way Lisu anavyotafuta madaraka kwa kumdharau/kumkose adabu Mbowe! haikubaliki!
 
Kwa mwendo huu wa Lisu, atakiuza chama kwa Msigwa. Usiachie chama , lilwalo na liwe. Aanzishe chake na Heche wake!

Na kwa kuropoka kwake, kutokuwa na kaba ya ulimi dola itakifuta. Samia atakifuta kwa sababu ambazo kila mmoja atazikubali na si kukionea.
Kilitoka mikononi mwake?.
Umelewa wewe.
 
Kabisa ni rasmi naona chama kinataka kutekwa na wanaharakati uchwara.

Hakuna kuachia Chama kama wanataka wakaunde Chao , period
Ukiona machawa wa mama Abdul na CCM wanamuogopa mtu jua wameshindwa kummiliki, hivi nyie chawa wa mama mapenzi na CHADEMA yameanza lini?
 
Kwani mbowe ndiye anaaamua chama amuachie nani au wanachama ndio watachagua nani wanamtaka siku ya uchaguzi? Mbona hii kauli yako inataka kuchorea mstari madai ya kwamba chana ni cha mtu na sio wanachama? Au umekosea.
Sijakose! Nimelitafakari kabla ya kuliandika. Inafika mahali kukinusuru chama ambacho wewe una dhamana kama mwenyekiti...LAST DEFENCE LINE...you take charge in whaterver way to make things move! The way Lisu anavyotafuta Uenyekiti, siwezi kukubali!

To be honest, very honest so to say, Ningelikuwa mimi Mbowe, ningelicheza JECHA!
 
Namuunga mkono mbowe, akiachia chama ndo mwisho wa chadema.

Lisu hawezi kuelewana na wenzie ktk siasa, kama anaweza kutukana viongozi wakuu wa nchi akiwa hana mamlaka ya juu ktk upinzani akiwa mwenyekiti atazua tafrani na mamlaka hazitamvumilia.
Namsihi mama atumie instruments zake zite ku mu eliminate lisu toka kwenye siasa abaki mropokaji mtaani
Utakuwa una matatizo kichwani:
Kwanza hiki chama ni cha Mbowe hadi akitoka kitakufa?
Pili hebu tuonyesheni tusi lolote lile ambalo Lissu amewahi kumtukana kiongozi yeyote? Mwizi wa kura akimwita mwizi ni tusi?
Mtoa na mpokea rushwa ukimwita mla rushwa ni tusi?
Mtekaji na muuaji ukimwita wewe mtekaji tena wauaji ni tusi?

Tatizo lenu chawa mmeishozoea kuwaimbia mapambio viongozi wa CCM hata wanapokosea kwa Lissu hana. Kwa kukosa akili unapendekeza mama amueliminate Lissu kwenye siasa, kwa kutumia sheria gani?

Waache CHADEMA wachague viongozi wanaoona wanaweza kuipeleka mbele CHADEMA alipokwamia Mbowe. Hizi bangi zenu pelekeni lumumba
 
Neno muongo ni neno sahihi ila lina bad connotation, kumuita mtu muongo inaonekana ni habitual layer, ukisema hakuwa sahihi unamaanisha ni mkweli ila hapo ndio amekosea.

Ni kama demu wako kuchepuka mara moja tuu, huwezi kumwita malaya, utamuita amekosa auaminifu, kumwita malaya maana yake ni tabia na kjiuza!.
P
Mkuu nyie mnaopaka rangi maneno ndiomaana mnamuona Lisu mbaya. Yeye nyeusi ni nyeusi hana konakona za kucheza na maneno.
 
Hii tabia ya Lissu kuwa ropo ropo ni a very bad liability kwa kiongozi!. Anahitaji civility!. Hebu msikie hapa, anawaita wenzake wajinga!. Msikie Tundu Lissu Hapa, Anauliza Kama Wenzake Wana Akili Kweli! Maridhiano Ayaita Ujinga. Je, Lissu Bado ni Asset or Sasa ni A Liability?
View: https://youtu.be/Qa59DIQs2yI
Anajua huyo anayeitwa mjinga ni nani?.
Ila huu uropo ropo wa Lissu, japo ni a bad liability kwa kiongozi, ndio asset ya kuibamiza CCM na kuiingiza Chadema ikulu kwa kura za GenZii. Japo Lowassa Alikuwa a Liability CCM, Akawa Asset Chadema. Lissu is a Very Bad Liability, but is The Only Asset Chadema Has Kuwangiza Ikulu!. Je... ?

Wakati huu wa uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura, ukiendelea, huu ndio ungekuwa wa amsha amsha GenZii wajiandikishe kwa wingi kwenye daftari, lakini Chadema viongozi wako busy kutukanana na kupigana vijembe, muda wa uchaguzi ukifika, mikutano yao inajaa nyomi za watu, GenZii, lakini siku ya kupiga kura, hawaonekani!, kumbe hawakujiandikisha!.

P

Nyie wazee tulieni, CDM itapelekwa ikulu na sisi vijana wa 90 na 2000. Ndio tunahitaji mtu kama Lissu. Tangu Niko darasa la tatu Mbowe ni mwenyekiti mpaka nimemaliza chuo kikuu Mbowe ni mwenyekiti, na uzoefu wa miaka 7 kazini bado Mbowe ni mwenyekiti.Hapana imetosha sasa ampishe Lissu kwa vile hataki kwa hiari atalazimishwa kwenye sanduku la kura.
 
Kuongoza vyama vyamabadiliko sio rahisi kama unavyofikiri.Unadhani kungekua na huo ukomo kati ya wale waliowahi kugombea uko nyuma wangeshinda ina maana wangekua ndio wenyeviti unadhani hicho chama kingekua wapi kwa sasa?.Inawezekana ata nyie mnaopalilia hiyo agenda ya ukomo mna agenda yenu yakuja kupandikiza mtu wenu badae aje kukiny'ong'onyeze chama.Ccm bado ni chama chenye mipango mingi yakudhibiti wapinzani wake.kungekua na usawa wakisiasa hiyo ingekua agenda ila sio kwasasa kwasababu bado hakuna misingi sawa yakisiasa.tupunguze mihemko na uchawa tutazame uko mbele zaidi badala ya hapa karibu kwasababu ya mikumbo na upepo.Mengine tuache kura ziamue.
Kwa hiyo hata kama kuna mwingine mwenye uwezo wa kukipeleke mbele chama hatakiwi kwa hoja yako? Kosa la Lissu ni nini hapo?
Kwa nini uone kuwa kuchaguliwa kwa Lissu ni kuweka pandikizi? Kwa nini Mbowe asiwe pandikizi la CCM?

Wenye mihemko ni nyie msioamini kwenye mabadiliko, Mbowe amefika ukomo kwa maana kwenye maridhiano nini mafanikio kwenye mabadiliko ya mifumo ambayo CCM wanaitumia kwenye kuhujumu vyama vya upinzani?

Uchaguzi wa 2024 umeonyesha CCM ni watu wa aina gani na kuelekea uchaguzi wa 2025 muhimu kuwa na approach nyingine kudeal na CCM.

Kwani Edwin Mtei alifia akiwa kiongozi? Hakumuachia Bob Makani? Bob Makani hakumuachia Mbowe aendeleze walipoishia? kwa nini kwa Mbowe iwe tofauti mnakuja na hoja nyingi za kijinga kama vile zaidi ya Mbowe hakuna mwingine? Kwani Mbowe ndiye mwanzilishi wa CHADEMA?
Acheni uchawa
 
Mwizi wa kura akimwita mwizi ni tusi?
Mtoa na mpokea rushwa ukimwita mla rushwa ni tusi?
Mtekaji na muuaji ukimwita wewe mtekaji tena wauaji ni tusi?
EVIDENCE? EVIDENCE EVIDENCE siyo kuropoka tu!
 
Back
Top Bottom