Mbowe: Vijana wa chama changu wana mihemko, Hivi mnajua maana ya kuingia barabarani?

Mbowe: Vijana wa chama changu wana mihemko, Hivi mnajua maana ya kuingia barabarani?

happyxxx

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2020
Posts
604
Reaction score
1,970
IMG_20220604_212003.jpg


Kamanda Mbowe amekuwa na hulka tofauti sana tangu aanze safari za ikulu.

Anawapa makavu vijana wanaojifanya wana uchungu na chama chake.

Je, nini kimembadilisha?

Ni muda ndio utasema.
 
Mbowe sasa amekomaa. Anataka kufanya siasa na si uwanaharakati. Ukisoma mitandaoni vijana wa CHADEMA wengi ni wanafanya harakati badala ya siasa.

Si wavumilivu, wana mshambulia kila wanaye dhani yuko kinyume na mtazamo wao. Wanasusia fursa ambazo kama wangezitumia zingesaidia kutuvusha.

Hivi karibu nimejufunza kwamba, wanaharakati hawaitakii mema hii nchi. Hawapendi kuona siasa za kistaraabu. Wao wanapenda kuona kukiwa na mizozo na mitafuruku kila kukicha..nadhani ndo wanafaidika kwa namna moja ama nyingine. Wanaogopa kwamba mambo yakiwa vyema watakosa relevancy na hivyo matumbo yao kiwa hatarini.

Mbowe amepitia mengi, amejifunza mengi na amekomaa.
 
Back
Top Bottom