Mbunge Joseph Kasheku Msukuma ataka Magufuli apewe Mihula minne ya Miaka 20 ili kukamilisha miradi

Mbunge Joseph Kasheku Msukuma ataka Magufuli apewe Mihula minne ya Miaka 20 ili kukamilisha miradi

Akizungumza bungeni leo Mheshimiwa Msukuma kadai hakuna Rais aliyedhubutu Kama Magufuli tangu tupate uhuru....
"... mtu yeyote mwenye akili akimpa mtu mwenye akili mawazo ya kipumbavu huku akijua kuwa mtu huyo anajua kuwa mawazo aliyopewa ni ya kipumbavu lakini akayakubali basi mtu huyo aliempa mawazo hayo ya kipumbavu atamdharau sana ...."

Mwl. J.K. Nyerere
 
Akizungumza bungeni leo Mheshimiwa Msukuma kadai hakuna Rais aliyedhubutu Kama Magufuli tangu tupate uhuru...
Musukuma asitufanye sisi sote ni wa la Saba Kama yeye. Ni kitu gani cha ajabu ambacho Magufuli amefanya Mtanzania mwingine hawezi?? Angalia mambo ya Nyerere hapa;
Nyerere alijenga madaraja makubwa kama Kirumi, Selander, Wami, Mara na mengine mengi.
Nyerere alijenga viwanda vya kuchakata mazao ya Pamba, Kahawa, Pareto, Chai, Ngozi, Nyama, Maziwa, Viatu.
Nyerere alinunua Meli na vivuko (Panton) katika maeneo kadhaa nchini.

Nyerere alijenga viwanda vya kutengeneza Vifaa/Zana za kilimo, Mbolea, Madawa, Magurudumu n.k
Wakati wa Nyerere wanafunzi walisoma na kusafiri kwenye usafiri wa umma bure.
Nyerere alijenga Reli ya TAZARA

Pamoja na mambo mengine kede kede na kuwafanya Watanzania kuwa wamoja na upendo bila chuki za kikabila kisiasa au ukanda.

Lakini bado aliondoka madarakani kwa hiari yake mwenyewe (kung'atuka) na hakuogopa ama kuhofia kwamba akiondoka madarakani ni nani atafanya kama yeye!

Vimbwanga vya kutaka kuaminisha watanzania kwamba hakuna mwingine mwenye uwezo wa kufanya kama WEWE yanatokea wapi???
 
Mkuu hayo yote Jiwe alishayapanga ,,,subiri siku si nyingi yatazuka maandamano ya kupangwa ikionesha wanataka Rais aongezewe muda.
Hapo ndipo alipoboa. JPM kipenzi cha wengi akamilishe miaka yake 10 na 2025 akabidhi kijiti kwa mwingine. Hizi ngonjera za akina Msukuma ni za kupuuzwa
 
Akizungumza bungeni leo Mheshimiwa Msukuma kadai hakuna Rais aliyedhubutu Kama Magufuli tangu tupate uhuru...
Wameshaanza tayari na kwakuwa wapo wengi mjengoni utasikia tunafanyia marekebisho vifungu vya katiba
 
Tayari

Sasa Nape alikuwa anaongea nini?

Rais akiwakumbuka wafanyakazi tu ataungwa mkono wa ajabu Amalizie miradi
Siyo awakumbuke wafanyakazi pekee yao tu bali akumbuke sekta zote yaani wakulima,wafanya biashara na wale wasiyo na ajira wakumbukwe
 
Kani hiyo miradi ni ya Magufuli binafsi au ni ya serikali?

Magufuli akifa kesho hiyo miradi itasimama?
Bila Jiwe Tz haipo, siku akifa jiwe na Tanzania inakufa, sioni mfu mwingine wa kuiletea tz maendeleo zaidi ya mchato!!!
 
Mtupoli LITAKE LISITAKE...
Nchi imekua ya makumaku sana hii.
 
Kama ya late Nkurunzinza sio.
Mule mule. Nkurunzinza na watu wake walirudi kuisoma Katiba neno kwa neno na "wakagundua" kumbe anastahili term ya pili maana ile inayosemekana ilikuwa ya kwanza actually haikuwa ya kwanza😀
 
Angalia machache aliyofanya Mkapa hapa na akaondoka baada ya miaka 10.

Mbali na mianya ya Rushwa,Awamu ya Mzee Mkapa ilipatwa na changamoto za uendeshaji wa Siasa visiwani Zanzibar,na ndiyo maeneo ambayo Serikali yake ilikosolewa sana, Ila kuna mazuri alifanya na hatuwezi kusema hakufanya. Hebu ona baadhi ya machache aliyoyafanya.

1.Tanzania inajivunia kuwa na Uwanja mkubwa wa mpira Afrika Mashariki na Kati (Ulijengwa wakati wa Mkapa).

2. Chuo Kikuu Kikubwa Afrika Mashariki(Chuo Kikuu Cha Dodoma), ni matokeo ya Maamuzi ya Serikali ya Mzee Mkapa na kuja kukamilisha kwa vitendo na Serikali ya Jakaya Kikwete, kumbukumbu kabla ya UDOM watanzania wenye sifa za kusoma Chuo Kikuu walikuwa wanapigana Vikumbo UDSM na SUA kabla ya Ujio wa SAUT.

3.Mtandao wa Barabara za Lami nchi nzima zilianza kutengwa kwa speed kubwa wakati wa Mzee Mkapa, nadhani alilenga kuacha Alama ya kuwa kiongozi ambaye amejenga mtandao wa Lami nchi nzima.

4. Mzee Mkapa aliendeleza pale alipoanzisha Mzee Mwinyi kwa kubadili mfumo wa Uchumi kutoka Uchumi hodhi kwenda Uchumi wa Ubia kati ya Sekta binafsi na Serikali na ndiyo tukaanza kuona kasi kubwa ya uwekezaji katika kila sekta kutoka sekta binafsi, leo tuna Vyuo Vikuu zaidi ya 20 vinavyomilikiwa na sekta binafsi, kwa upande wa Sekta ya Afya zaidi ya asilimia 50 ya vituo vya Afya vinamilikiwa na sekta binafsi. Haya ni matokeo ya maono ya Mzee Mkapa.

5. Mzee Mkapa alianza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu binafsi, kabla ya uamuzi huo ilikuwa ili upate Mkopo ilikuwa lazima usome kati ya UDSM, Muhimbili au SUA hii ilisababisha vijana wengi wenye sifa ya kusoma Chuo Kikuu wakakosa fursa hiyo,leo tujiulize Mkapa asingeamua Haya wangapi wangekosa fursa hii ya kusoma mpaka Chuo Kikuu?Hizi degree zilizotapakaa mpaka Vijijini ni matokeo ya Uongozi wa Mzee Mkapa.

6.Ni wakati wa Mzee Mkapa ndiyo Ajira za Serikali zilirejea rasmi,mwaka 1997,ndiyo Serikali ilirejesha kwa kasi Ajira Serikalini Baada ya kusitishwa kwa muda kwa kile kilichoitwa Kubana matumizi,kabla yake ilikuwa Ni kawaida mtu kumaliza Chuo na kukaa hata miaka 5 bila Ajira kwa sababu kasi ya Serikali kuajiri ilifubaishwa kwa kisingizio cha kubana matumizi.

8.Mzee Mkapa alipokea nchi ikiwa na mzigo wa madeni,binafsi sikuwahi kumsikia akimsema mtangulizi wake kwa kukopa huko,Mzee Mkapa alijua kwa mazingira yeyote Serikali ya Mzee Mwinyi ilikuwa lazima ikope Maana ilichokikuta hazina ilihitaji busara na akili kubwa kuiongoza nchi na ndiyo Maana Mzee Mwinyi alikopa sana,Mzee Mkapa kwa kutambua kazi kubwa aliyofanya Mzee Mwinyi,aliyalipa madeni mpaka kufikia chini ya Trilion 8,alilipa kimya kimya huku akijua Ni wajibu wake.

9.Bunge hili la Kisasa lililopo Dodoma,lilijengwa na Serikali ya Mzee Mkapa.

10.Hata kwenye michezo kila Awamu kulikuwa na mafanikio,Awamu ya kwanza ilishuhudia Tanzania ikicheza kwa Mara ya kwanza fainali za Mataifa Huru barani Afrika,Awamu ya Pili Simba ilicheza faunal za michuano ya kumbe la shirikisho la kabumbu barani Afrika,Awamu ya Tatu Yanga ikafuzu kucheza hatua ya makundi ya kombe la Klabu Bingwa Afrika,awamu ya nne Simba ikacheza hatua hiyo ya makundi ya Klabu bingwa,Awamu ya tano Taifa Stars imecheza fainal za mataifa Afrika huku Simba ikifika hatua za makundi.
11. Alianzisha Taasisi madhubuti za kisasa Kama TRA, TANROADS, TFDA,

Kila kipindi kina mafanikio yake ambayo Ni vyema tukayatambua. Huyu Magufuli naye afanye yake aondoke wala asitudanganye kwamba yeye ana VISION kuliko Watanzania wengine.
 
Akizungumza bungeni leo Mheshimiwa Msukuma kadai hakuna Rais aliyedhubutu Kama Magufuli tangu tupate uhuru...
Kauli kama hizi zingeanza kutolewa mwishoni mwa 2024 angalau watu wenye busara wangeziona zina mantiki kidogo ndani yake. Lakini kwa kuwa zilianza kutolewa toka 2017 na hatimaye kuwa ""re-echoed" 2020 na wakina Juma Nkamia na Keisy, huku mara zote meza ya Spika ikionyesha kuzipa uzito.

Hii pengine ndiyo sababu iliyokuwa imejificha ya kufanya mabadiliko ya sheria ili kumpa kinga ya kutoshtakiwa Spika wa Bunge. Kuna kila dalili kuwa hili jambo linakwenda kutendeka muda ukifika. Ukiona wazee kama Ali Hassan Mwinyi na Butiku wakiliongelea hadharani, basi itambue kila kitu kimekwisha kupangwa.

Mzee wetu wa Lupaso pengine ndiyo maana alitangulia "with a bleeding heart".
 
Musukuma asitufanye sisi sote ni wa la Saba Kama yeye. Ni kitu gani cha ajabu ambacho Magufuli amefanya Mtanzania mwingine hawezi?? Angalia mambo ya Nyerere hapa....
Mbona hoja yake ya miradi isiyogusa wananchi tuachane nao Ufipa Wote mlishangilia na hamkumuita Darasa la Saba.Saizi ni kilaza Bwashee
 
Katiba yetu imetamka wazi kwamba ni awamu mbili achia ngazi wengine waingie..akiruhusiwa kuendelea kisa kafanya miradi mingi inatia mashaka kwa sababu hakuna rais ambae hakufanya jitihada zake ili kuweza kutoka hali moja kwenda nyingine, Pale walipofikia muda wao ukawa umeisha waliendeleza waliofuatia katika ngazi hio ya rais.Tz wakifanya makosa ya kubadili katiba ili magufuli aendelee kuwa madarakani,tutaenda kupoteza dira kama taifa.
 
Mtu aliyevuruga nchi kiasi hiki aongezwe muda ? Mgonjwa wa bipolar disorder ,user of cannabis sativa .
 
Kwani ni nani aliyemwambia inahitaji miaka 20 kukamilisha hiyo miradi.

Kwa nini isiwe 50, ama hii 10 aliyoipata.
 
Hapo ndipo alipoboa. JPM kipenzi cha wengi akamilishe miaka yake 10 na 2025 akabidhi kijiti kwa mwingine. Hizi ngonjera za akina Msukuma ni za kupuuzwa
Nchi haitafuti Mpishano wa Viongozi kwenda Ikulu. Bali tuna hitaji kiongozi kama Magufuli Mjomba.

Watu kama Hawa ni Adimu sana Mjomba. Tunapo mpata hatuna budi tumtumie Mjomba.

Magufuli 10 Tena 👐👐👐👐
 
Back
Top Bottom