Mbunge Mohamed Issa: Wanaotoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar wawe na Passport
Katiba ya Zanzibar haiwatambui wanaoishi bara kama wazanzibari. Wakiwa wapemba, waunguja au watanganyika. Wote hawa kwa sheria za SMZ hawana haki ya kumiliki ardhi, nyumba na hata chombo cha moto. Hata leseni ya udereva lazima uwe na kitambulisho cha mzanzibari.
 
Huyu Mbunge sijui ana umri gani! Wazanzibar walijaribu hilo miaka ya nyuma Wabunge wa Tanganyika wakasema nao waje kwa Passport. Wazanzibar waliondoa utaratibu ndani ya siku 7. Mwalimu Nyerere alisikia akaacha Bunge liwakaange...
Mimi mbona haujani tag? Huu siyo ndiyo Uzanzibar wenyewe mnaoupinga humu?
 
Mbunge wa Konde (ACT Wazalendo), Mohamed Said Issa ameitaka Serikali kurejesha upya utaratibu wa watu wote wanaoingia Zanzibar kuwa na hati ya kusafiria...
Imagine, mzanzibari anaongea haya bila kujua yafuatayo:

1. Yeye amevuka maji kuja kula perdiem bungeni, bila passport.

2. Wazanzibar wanamiliki ardhi na nyumba, mashamba n.k bara popote.

3. Wazanzibar wameajiriwa kwenye serikali kuu na hata kwenye private sector Bara.

4. Pato kubwa la wazanzibar wengi sana ni biashara wanazozifanya DSM au la, pesa wanazotumiwa na watoto wao wanaoishi DSM, Tanga na maeneo mengine ya bara. kuna wapemba hadi Arusha, hadi Mwanza popote nchini huwezi kukosa alau mpemba mmoja. ukienda Kigamboni, gongolamboto, tuseme maeneo mengi ya uswahilini DSM yamejaa maduka ya wapemba, wapika chips na mikahawa wazanzibar n.k.

halafu yeye leo hii anaona wabara wanaenda kule kuchukua ardhi, kuchukua kazi. hivi kuna wabara wanaendaga kutafuta ajira zanzibar kweli? nilikuwa sijui hili. pia, kwani samia anapokuja huku anakuwa na passport?
 
Watanganyika wanapaswa kumuunga mkono huyu mbunge kashaonyesha njia tumsapoti jamani Tanganyika yetu iwe huruuu!
 
Ukienda Kule mtandaoni X Watanganyika wamechachamaa na kumlaani mbunge wa ACT wazalendo kwa Hoja yake ya kibunge kwamba Watanganyika waingie Zanzibar kwa Passport kama zamani

Nauliza tu, Kosa lake ni lipi kwa mujibu wa sheria?

Najua Hapa JF ndio kuna akili Kubwa

Nawasilisha 😄
 
Hakuna kosa, tukubaliane tu - na sisi Wazanzibari tukija Bara - Tuingie kwa Passport Pia. Ili mzni u-balance. Na sisi pia Wazanzibari tusiruhusiwe kununua viwanja wala nyumba bara - ili pia mzani u-balance.
Unaelewa maana ya Muungano wa Serikali 2?

Tuanzie hapo
 
Wakati wengine wanajaribu kujenga madaraja wengine wanataka kujenga Fensi / Ukuta...,
 
Katiba ya Zanzibar haiwatambui wanaoishi bara kama wazanzibari. Wakiwa wapemba, waunguja au watanganyika. Wote hawa kwa sheria za SMZ hawana haki ya kumiliki ardhi, nyumba na hata chombo cha moto. Hata leseni ya udereva lazima uwe na kitambulisho cha mzanzibari.
Uzuri ni kwamba ukiishavuka maji kuja kuishi huku na akili zinafunguka,huwezi kuwa na akili ndogo kama huyo kunguni.
 
Back
Top Bottom