Mbunge Pauline Gekul akamatwa na Jeshi la Polisi akijaribu kutoroka nchini kuelekea nchini Kenya

Mbunge Pauline Gekul akamatwa na Jeshi la Polisi akijaribu kutoroka nchini kuelekea nchini Kenya

With a rotten system, Mwisho wa movie lazima ataachiwa huru tu. Manakumbuka Kigwangala aliwahi kutuhumiwa kumpiga mtu risasi ya mguu? Nini kiliendelea? Bashite na Sabaya wapo uraiani na kulikuwa na evidence za uhalifu hadi footage za CCTV camera. Msitarajie jipya hapo, baada ya Wiki moja hili sakata litasahaulika

..inategemea kama aliyofanya Gekul yana baraka za wakubwa zake au la?
 
Hata taarifa zake za unyanyasaji zilipofika hapa JF watu wengi walidai ni uzushi mpaka pale alipotenguliwa ndio wakaamini. Tusubirie muda utasema.
Hivi kweli kwa akili yako Gekul atoroke ili iweje? Atavikimbia vyombo vya dola? Atajificha kenya? Hivi kweli kulikuwa na arrest warant? Kwani alikuwa haruhusiwi kutoka nje ya nchi? Na ninani kamzuia?

Shida mnatuamia hisia zaidi mnasahau sound Mind!
 
Yani kashaingia kwenye line vizuri sana na vile chaguzi zipo karibu watamtoa kafara kuonyesha chama kinavyotenda haki ili kurudisha imani ya wananchi,, safi sana mwisho wa ubaya ni aibu
Huyo anatolewa kafala na hivi alitokea upinzani kwisha Habari!


Tena hao waliotokea upinzani ndio CCM hawakubaliki kabisa
 
Daah yaani hapa ndo kaharibu kabisa !! Nahisi hata huko ofisini wadosi watakua wanamcheka na kumshangaa !!
Wakati mwingine ukifanya makosa tulia subiri upepo upite na upambane nao hivyo hivyo 😂😂

Sasa alikua anatoroka kwenda wapi wakati anajijua yeye ni maarufu bado pia ana jimbo.
Hapa hata wadosi watajiweka pembeni kujifanya hawaoni huo msala atajivua mwenyewe inaonekana hata kubebeka habebeki kabisa

Na hata ukimbeba huu woga alionao hachelewi kwenye kampeni kusema anamshukuru Mama kwa kumchomoa kwenye msala 😂
Usaliti hauwaachi wasaliti salama bin salmin hata mara moja.
 
Tayari yuko mikononi mwa POLISI anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Manyara, pichani akiwa ofisi za RCO - Manyara.

Kamanda wa polisi Manyara, GEORGE KATABANZI amegoma kutoa maelezo ya ziada ya kwanini anashikiliwa, amesisitiza ni taratibu za upelelezi.

Taarifa nyingine ni kwamba katibu wa Pauline Gekul anayeitwa HUSSEIN S. ABRIMA na vijana wawili walioshiriki utesaji ule, wanashikiliwa polisi.

Taarifa tulizonazo ni kwamba jalada lililofunguliwa polisi ni malalamiko ya Pauline Gekul kutaka kuuwawa na siyo malalamiko ya Hashimu Philemon.

Afande George Katabanzi, tunataka kuona haki ya Hashimu inapatikana polisi. Watanzania tupo tayari kuchanga fedha akapimwe hospitali za kisasa.

Tunakwenda kumpima kupata ushahidi wa kitabibu wa kumuingizia chupa makalioni Hashimu. Mnachelewesha ili ku-buy time eeh? Tumeshtuka.

Tutafungua kesi mbili kama hamtaki kumshtaki Pauline GEKUL. Tutafungua kesi ya jinai, madai na kikatiba na tutaomba tafsiri ya mahakama kuu.

Tunao mawakili wa kutosha. Jopo linaongozwa Manyara na Wakili Thadei, Wakili Madeleka na mawakili wengine. Hatutaki kona-kona katika hili.

MMM, Martin Maranja Masesed
Shida yenu mnatumia hisia zaidi lazima mahakama ipewe uthibitisho kuwa kitendo husika kilifanyika au kulikuwa na jinai sio hisia! Mahakamani hakuna kuoneana huruma kule ni ushahidi na vipengele vya sheria!
 
With a rotten system, Mwisho wa movie lazima ataachiwa huru tu. Manakumbuka Kigwangala aliwahi kutuhumiwa kumpiga mtu risasi ya mguu? Nini kiliendelea? Bashite na Sabaya wapo uraiani na kulikuwa na evidence za uhalifu hadi footage za CCTV camera. Msitarajie jipya hapo, baada ya Wiki moja hili sakata litasahaulika
Peter madereka ameshafika site subiri uone !
 
Back
Top Bottom