Mch. Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama ameishinda vita hata kabla haijaanza. Muda utazungumza

Mch. Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama ameishinda vita hata kabla haijaanza. Muda utazungumza

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Mch. Eliona Kimaro ameonesha ukomavu wa kiroho na wa kiutumishi wa hali ya juu sana. Baada ya kupewa barua ya kutakiwa kuchukua likizo ya siku 60 (ambayo hakuiomba bila shaka maana alipanga kuendesha semina), inayomlazimu kusitisha semina aliyokuwa ameianza hapo kanisani kwake, na kutakiwa kuripoti makao makuu ya KKKT baada ya likizo ili apangiwe kituo kingine, itikio na kauli yake ni hii hapa:

Amesema:
"Mimi ni Mchungaji wa Lutheran ninayeheshimu kiapo changu cha kichungaji na kuishi katika kiapo changu cha kichungaji na maadili pia ya kichungaji kwa neema ya Mungu. Kwa sababu hiyo imenilazimu kutii amri na kwenda kwenye hiyo likizo ya siku 60 na baadae kuripoti kwenye ofisi ya Askofu kama nilivyoelekezwa" Asante.


Kwa kauli hiyo keshaishinda tayari vita inayomkabili hata kama haijaanza. Ushindi mkuu kwa mtu wa Mungu ni kukubali kujivika UNYENYEKEVU! Mch. Kimaro ana nguvu sana hapo kanisani kwake na kila mtu anajua hivyo.

Angeweza kabisa kudai apewe maelezo kwa nini afanyiwe hivyo kwa ghafla na bila shaka angeweza kuliomba baraza lake la wazee lisimame kidete pamoja naye kupinga maamuzi hayo, na nina uhakika sehemu kubwa ya washirika wangemuunga mkono na pangetokea vurugu!! Yeye hakufanya yote hayo!!

Sijasema kuwa Mch Kimaro hana makosa maana sijui undani wa jambo lenyewe, lakini kuna dalili kuwa anaweza kuwa amechezewa mchezo "usio mzuri". Siyo siri kuwa Kanisa la kkkt kijitonyama ni kanisa tajiri na kuna fedha hapo!! KIla mmoja anaitazama hiyo bila kujua kazi kubwa iliyofanyika kuandaa mazingira ya kiroho na kiuwezeshaji hadi kuona matunda hayo yaliyo dhahiri kwa kila mmoja. Kanisa linaloweza kuchanga sh milioni 300 kwa nusu saa siyo mchezo. Usiniambie kuwa ni kwa sababu kuna matajiri hapo la hapana, bali wale watu wameandaliwa vizuri kwa Neno la Mungu, wamelelewa vizuri na mchungaji wao kisha kuweza kutoa maziwa mengi. Kuna mtu anaona maziwa tu lakini kumbe hayo maziwa ni matokeo ya uchungaji bora!

Watu wana asili ya WIVU!! sitashangaa kama sakata zima limejengwa juu ya wivu!! Ilikuwa ni haki ya mch Kimaro kufaidi matunda ya huduma yake hapo kama mchungaji. Hakuna namna ambayo mchungaji hawezi kufaidi maziwa ya kundi analochunga. Sasa wengine hiyo inawauma!! Biblia inasema hivi:

"Ni askari gani aendaye vitani wakati wowote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Je ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi. 1Wakorintho 9:7?"

Ninafahamu katika mazingira haya kuna uwezekano mkubwa wa Mch. Kimaro kutuhumiwa "kula pesa za kanisa" ili kuhalalisha hatua zilizochukuliwa, lakini Mungu wa mbinguni anajua yote!! Kwa wengine kwa mchungaji kunywa katika maziwa ya kundi analochunga kama Biblia inavyoagiza huko wanadai ni "kula pesa za kanisa".

Lakini ukweli ni kwamba kazi ya mchungaji ni pamoja na kula pesa au sadaka za kanisa. Mchungaji akila maana yake Mungu amekula!! Huo ni ukweli tukubali tusikubali!

Yawezekana kuna mtu ana mpango wa kula matunda ya jasho la mwingine, Mungu anajua!

Namtia moyo mch Kimaro kuwa tayari keshaishinda vita kabla hata haijaanza na Mungu atakuwa pamoja naye popote atakapoenda!! Baraka za Kweli za Mungu huwa hazifuatwi bali huwa ZINAMFUATA MTU WA MUNGU!! Ni suala la muda tu watu watalishuhudia hili.

Mch. Kimaro nenda kapige kazi popote Na baraka za Mungu zitakufuata!!! Kama kuna tatizo la msingi napo usikose kulitengeneza kwanza na Mungu atakuwa pamoja nawe!!
 
Tafadhalj usije kuliama kanisa kisa kimaro. Hon endelea kutoa zaka na kumsapoti yule aliyeletwa swwal la kuwepo kwa kipato kikubwa hapo Hilo lisikuzumbue katu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Lakini pia watu huwa wanasahau ukweli kuwa mchungaji yeyote naye ni mtu tu, na anaweza kufanya kosa kama mtu mwingine!! Tatizo ni kwamba kama tayari watu walikuwa wanamsagia meno kwa wivu kutokana na mafanikio yake, ikitokea wakaona kosa lolote wanakandamizia hapo hapo kumbe walikuwa na lao jambo hata kabla, bali walikuwa wanatafuta tu sababu za kuegemea!! Ndiyo maana nimesema kuwa simaanishi mch hana makosa (japo anaweza kuwa hana makosa), ila kama kuna makosa basi watu wameyatumia ili kutekeleza matakwa ya wivu wao!! Msingi wa kikristo ni KUSAMEHEANA!
 
Umeshaiona clip inayomhusu, au umeamua kuja na porojo tu..
Umaarufu umempanda kichwani. Inabidi ajitafakari
*****************************

ASKOFU MWAMAKULA AZUNGUMZIA SUALA LA KUSIMAMISHWA KWA MCH. DKT. KIMARO

Taarifa za kupewa likizo na kusimamishwa kwa muda kwa Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Usharika wa Kijitonyama Mch. Dkt. Eliona Kimaro zimeanza kuenea katika mitandao ya kijamii na kuzua hisia nzito miongoni mwa waumini na wasio waumini wa KKKT. Kimaro ni miongoni mwa watu maarufu, hivyo suala hili haliwezi kuchukuliwa wepesi.

Hapa tumeweka tazamo wetu wa kitheologia ili kutoa mchango wetu katika hoja hii. Ni dhahiri kuwa misimamo binafsi ya Mch. Dkt. Kimaro imemtia katika misuguano mingi na uongozi wa KKKT kwa kipindi kirefu. Lakini, misimamo hiyo iliweza kuvumiliwa ndani ya KKKT na ndio maana alipewa kuongoza Usharika mkubwa katika Dayosisi ya Mashariki na Pwani.

Tumefuatilia kutoka kwa baadhi ya viongozi ndani ya Dayosisi ya Mashariki na kuelezwa kuwa matamshi ya Mch. Dkt. Kimaro aliyoyatoa hivi karibuni baada ya kutoka Marekani ndiyo yaliyopelekea uongozi wa Dayosisi kumuita na kumpa likizo ambayo imeibua hisia na mjadala mzito baada ya yeye Mch. Dkt. Kimaro kutoa hadharani jambo ambalo lilikuwa ni karipio la Kichungaji.

Kwa mujibu wa video iliyosambaa, Mch. Dkt. Kimaro amesikika akisema kuwa vijana wa Kikristo sio waaminifu bali vijana wa Kiislamu ndio waaminifu kuliko vijana wa Kikristo. Mch. Dkt. Kimaro amesikika pia akisema kuwa watu wote wanaosimama madhabahuni [Wainjilisti, Wachungaji na Maaskofu] ni matapeli na watu wote waliokaa kwenye viti [vya ibadani - Wazee wa Kanisa na waumini] ni matapeli pia. Mch. Dkt. Kimaro amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa takwimu [hajataja ni takwimu gani na taasisi iliyotoa takwimu hizo] zinaeleza hayo aliyosema.

Kitheologia tunapata tafsiri kuwa Mch. Dkt. Kimaro hana imani na maadili ya Kikristo, hana imani na mafundisho ya Kikristo na pia hana imani hata na watumishi wenzake wote wa Kikristo kutoka madhehebu yote nchini Tanzania. Tafsiri hapa ni kuwa Mch. Dkt. Kimaro anaonesha kuwa ana imani na maadili ya Kiislamu, mafundisho ya Kiislamu na hata Mashehe wa Kiislamu. Pia, Mch. Dkt. Kimaro anaonesha kuwa hana imani pia na hata vijana wake wa Kikristo ndani ya KKKT na nje ya KKKT ambao siku zote yeye mwenyewe amekuwa akiwafundisha katika ibada, mikesha, semina, morning glory, bali ana imani kubwa na vijana wa Kiislamu ndio maana akawaajiri hao katika miradi yake.

Mtumishi ye yote (Mwinjilisti, Mchungaji/Padre au Askofu) kutoka katika madhehebu yetu ya Katholiko (RC, Moravian, Lutheran, Anglikana na Orthodox) akitoa kauli kama hizo, ni lazima aitwe na uongozi wake, ahojiwe na hata ikibidi achunguzwe. Hicho ndicho kilichotokea kwake Mch. Dkt. Kimaro kuitwa na uongozi wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, kuhojiwa na kuchunguzwa. Kauli zake alizotoa zimepingana na imani, mafundisho na maadili ya Kikristo! Kauli ya Mch. Dkt. Kimaro hayakushambulia Ulutheri tu, bali kwa kujua au hata kutokujua, kauli yake ilishambuliwa Ukristo wote kwa ujumla katika nchi hii.

Kwa sababu hiyo, sisi Askofu tunatoa wito kwa waumini wote wa Kikristo nchini kuwa watulivu wakati KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani inashughulikia jambo la Mch. Dkt. Kimaro. Sisi tumelazimika kuandika baada ya kuona kuwa jambo hili limeanza kusambaa mitandaoni na kubeba hisia zaidi kuliko uhalisia na pengine kubeba upotofu mwingi zaidi kuliko ukweli.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki.
 
Jamaa aliliwa umaarufu na pesa hata akaanz kukata Tawa alilokalia.


Tukumbuke huyu n binadamu pia
 
Kwa sababu hiyo imenilazimu kutii amri na kwenda kwenye hiyo likizo ya siku 60
Hili neno IMENILAZIMU linaonesha hajatii chochote.

na ndiyo maana clip siyo ushahidi unaokubalika mahakamani!!
Mkuu, kisheria (The Electonic Transactions Act, 2015) clip ya audio au ya video inakubalika kabisa mahakamani kama itafuata taratibu za kuiwasilisha. Huo mtazamo kuwa hazikubaliki mahakamani, sijui ni kwa mujibu wa nini
 
Hotuba ya askofu malasusa iliashiria haya kwa kudai wachungaji wanajifanya wakubwa kuliko kanisa. Ipo shida kubwa kwenye diosisi ya madhariki na pwani na majimbo yake. Wapo watumishi wadogo kama parish worker ila wana nguvu hata kwa wachungaji kwa mahusiano yao na viongozi kwenye majimbo na diosisi. Kuajiriana kindugu na kutaka kupeana makanisa yenye kipato kunakera.
NAONA MUDA WA UAMSHO UMEFIKA.
IKIBIDI KUACHANA NA KANISA NI SASA !!
 
Umaarufu umempanda kichwani. Inabidi ajitafakari
*****************************

ASKOFU MWAMAKULA AZUNGUMZIA SUALA LA KUSIMAMISHWA KWA MCH. DKT. KIMARO

Taarifa za kupewa likizo na kusimamishwa kwa muda kwa Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Usharika wa Kijitonyama Mch. Dkt. Eliona Kimaro zimeanza kuenea katika mitandao ya kijamii na kuzua hisia nzito miongoni mwa waumini na wasio waumini wa KKKT. Kimaro ni miongoni mwa watu maarufu, hivyo suala hili haliwezi kuchukuliwa wepesi.

Hapa tumeweka tazamo wetu wa kitheologia ili kutoa mchango wetu katika hoja hii. Ni dhahiri kuwa misimamo binafsi ya Mch. Dkt. Kimaro imemtia katika misuguano mingi na uongozi wa KKKT kwa kipindi kirefu. Lakini, misimamo hiyo iliweza kuvumiliwa ndani ya KKKT na ndio maana alipewa kuongoza Usharika mkubwa katika Dayosisi ya Mashariki na Pwani.

Tumefuatilia kutoka kwa baadhi ya viongozi ndani ya Dayosisi ya Mashariki na kuelezwa kuwa matamshi ya Mch. Dkt. Kimaro aliyoyatoa hivi karibuni baada ya kutoka Marekani ndiyo yaliyopelekea uongozi wa Dayosisi kumuita na kumpa likizo ambayo imeibua hisia na mjadala mzito baada ya yeye Mch. Dkt. Kimaro kutoa hadharani jambo ambalo lilikuwa ni karipio la Kichungaji.

Kwa mujibu wa video iliyosambaa, Mch. Dkt. Kimaro amesikika akisema kuwa vijana wa Kikristo sio waaminifu bali vijana wa Kiislamu ndio waaminifu kuliko vijana wa Kikristo. Mch. Dkt. Kimaro amesikika pia akisema kuwa watu wote wanaosimama madhabahuni [Wainjilisti, Wachungaji na Maaskofu] ni matapeli na watu wote waliokaa kwenye viti [vya ibadani - Wazee wa Kanisa na waumini] ni matapeli pia. Mch. Dkt. Kimaro amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa takwimu [hajataja ni takwimu gani na taasisi iliyotoa takwimu hizo] zinaeleza hayo aliyosema.

Kitheologia tunapata tafsiri kuwa Mch. Dkt. Kimaro hana imani na maadili ya Kikristo, hana imani na mafundisho ya Kikristo na pia hana imani hata na watumishi wenzake wote wa Kikristo kutoka madhehebu yote nchini Tanzania. Tafsiri hapa ni kuwa Mch. Dkt. Kimaro anaonesha kuwa ana imani na maadili ya Kiislamu, mafundisho ya Kiislamu na hata Mashehe wa Kiislamu. Pia, Mch. Dkt. Kimaro anaonesha kuwa hana imani pia na hata vijana wake wa Kikristo ndani ya KKKT na nje ya KKKT ambao siku zote yeye mwenyewe amekuwa akiwafundisha katika ibada, mikesha, semina, morning glory, bali ana imani kubwa na vijana wa Kiislamu ndio maana akawaajiri hao katika miradi yake.

Mtumishi ye yote (Mwinjilisti, Mchungaji/Padre au Askofu) kutoka katika madhehebu yetu ya Katholiko (RC, Moravian, Lutheran, Anglikana na Orthodox) akitoa kauli kama hizo, ni lazima aitwe na uongozi wake, ahojiwe na hata ikibidi achunguzwe. Hicho ndicho kilichotokea kwake Mch. Dkt. Kimaro kuitwa na uongozi wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, kuhojiwa na kuchunguzwa. Kauli zake alizotoa zimepingana na imani, mafundisho na maadili ya Kikristo! Kauli ya Mch. Dkt. Kimaro hayakushambulia Ulutheri tu, bali kwa kujua au hata kutokujua, kauli yake ilishambuliwa Ukristo wote kwa ujumla katika nchi hii.

Kwa sababu hiyo, sisi Askofu tunatoa wito kwa waumini wote wa Kikristo nchini kuwa watulivu wakati KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani inashughulikia jambo la Mch. Dkt. Kimaro. Sisi tumelazimika kuandika baada ya kuona kuwa jambo hili limeanza kusambaa mitandaoni na kubeba hisia zaidi kuliko uhalisia na pengine kubeba upotofu mwingi zaidi kuliko ukweli.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki.
Uongo wa kiwango cha lami[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Umaarufu umempanda kichwani. Inabidi ajitafakari
*****************************

ASKOFU MWAMAKULA AZUNGUMZIA SUALA LA KUSIMAMISHWA KWA MCH. DKT. KIMARO

Taarifa za kupewa likizo na kusimamishwa kwa muda kwa Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Usharika wa Kijitonyama Mch. Dkt. Eliona Kimaro zimeanza kuenea katika mitandao ya kijamii na kuzua hisia nzito miongoni mwa waumini na wasio waumini wa KKKT. Kimaro ni miongoni mwa watu maarufu, hivyo suala hili haliwezi kuchukuliwa wepesi.

Hapa tumeweka tazamo wetu wa kitheologia ili kutoa mchango wetu katika hoja hii. Ni dhahiri kuwa misimamo binafsi ya Mch. Dkt. Kimaro imemtia katika misuguano mingi na uongozi wa KKKT kwa kipindi kirefu. Lakini, misimamo hiyo iliweza kuvumiliwa ndani ya KKKT na ndio maana alipewa kuongoza Usharika mkubwa katika Dayosisi ya Mashariki na Pwani.

Tumefuatilia kutoka kwa baadhi ya viongozi ndani ya Dayosisi ya Mashariki na kuelezwa kuwa matamshi ya Mch. Dkt. Kimaro aliyoyatoa hivi karibuni baada ya kutoka Marekani ndiyo yaliyopelekea uongozi wa Dayosisi kumuita na kumpa likizo ambayo imeibua hisia na mjadala mzito baada ya yeye Mch. Dkt. Kimaro kutoa hadharani jambo ambalo lilikuwa ni karipio la Kichungaji.

Kwa mujibu wa video iliyosambaa, Mch. Dkt. Kimaro amesikika akisema kuwa vijana wa Kikristo sio waaminifu bali vijana wa Kiislamu ndio waaminifu kuliko vijana wa Kikristo. Mch. Dkt. Kimaro amesikika pia akisema kuwa watu wote wanaosimama madhabahuni [Wainjilisti, Wachungaji na Maaskofu] ni matapeli na watu wote waliokaa kwenye viti [vya ibadani - Wazee wa Kanisa na waumini] ni matapeli pia. Mch. Dkt. Kimaro amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa takwimu [hajataja ni takwimu gani na taasisi iliyotoa takwimu hizo] zinaeleza hayo aliyosema.

Kitheologia tunapata tafsiri kuwa Mch. Dkt. Kimaro hana imani na maadili ya Kikristo, hana imani na mafundisho ya Kikristo na pia hana imani hata na watumishi wenzake wote wa Kikristo kutoka madhehebu yote nchini Tanzania. Tafsiri hapa ni kuwa Mch. Dkt. Kimaro anaonesha kuwa ana imani na maadili ya Kiislamu, mafundisho ya Kiislamu na hata Mashehe wa Kiislamu. Pia, Mch. Dkt. Kimaro anaonesha kuwa hana imani pia na hata vijana wake wa Kikristo ndani ya KKKT na nje ya KKKT ambao siku zote yeye mwenyewe amekuwa akiwafundisha katika ibada, mikesha, semina, morning glory, bali ana imani kubwa na vijana wa Kiislamu ndio maana akawaajiri hao katika miradi yake.

Mtumishi ye yote (Mwinjilisti, Mchungaji/Padre au Askofu) kutoka katika madhehebu yetu ya Katholiko (RC, Moravian, Lutheran, Anglikana na Orthodox) akitoa kauli kama hizo, ni lazima aitwe na uongozi wake, ahojiwe na hata ikibidi achunguzwe. Hicho ndicho kilichotokea kwake Mch. Dkt. Kimaro kuitwa na uongozi wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, kuhojiwa na kuchunguzwa. Kauli zake alizotoa zimepingana na imani, mafundisho na maadili ya Kikristo! Kauli ya Mch. Dkt. Kimaro hayakushambulia Ulutheri tu, bali kwa kujua au hata kutokujua, kauli yake ilishambuliwa Ukristo wote kwa ujumla katika nchi hii.

Kwa sababu hiyo, sisi Askofu tunatoa wito kwa waumini wote wa Kikristo nchini kuwa watulivu wakati KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani inashughulikia jambo la Mch. Dkt. Kimaro. Sisi tumelazimika kuandika baada ya kuona kuwa jambo hili limeanza kusambaa mitandaoni na kubeba hisia zaidi kuliko uhalisia na pengine kubeba upotofu mwingi zaidi kuliko ukweli.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki.
Huyu naye Pamoja na Uaskofu wake hawezi kufunga Gidamu za Viatu vya Kimaro. Kimaro ameiva Kiroho. Kimaro ameivisha Watu Kiroho . Kimaro hajailaza kazi ya Mungu. Ndiye Champion wa Morning na Evening Glory. Watu tulichelewa Vibaruani tukimsikiliza Asubuhi. Tulichelewa home tukimsikiliza Jioni. Mafundisho yaliyoshiba Neno la Mungu.
 
Huyu naye Pamoja na Uaskofu wake hawezi kufunga Gidamu za Viatu vya Kimaro. Kimaro ameiva Kiroho. Kimaro ameivisha Watu Kiroho . Kimaro hajailaza kazi ya Mungu. Ndiye Champion wa Morning na Evening Glory. Watu tulichelewa Vibaruani tukimsikiliza Asubuhi. Tulichelewa home tukimsikiliza Jioni. Mafundisho yaliyoshiba Neno la Mungu.
Acha kashfa basi ukijibu kwa busara unapungukiwa Nini?Ndio mafundisho hayo uliyofundishwa na mjivuni mwenzio Kimaro!hebu usimlinganishe Mwamakula na Watu wepesi wepesi kijana
 
Huyu naye Pamoja na Uaskofu wake hawezi kufunga Gidamu za Viatu vya Kimaro. Kimaro ameiva Kiroho. Kimaro ameivisha Watu Kiroho . Kimaro hajailaza kazi ya Mungu. Ndiye Champion wa Morning na Evening Glory. Watu tulichelewa Vibaruani tukimsikiliza Asubuhi. Tulichelewa home tukimsikiliza Jioni. Mafundisho yaliyoshiba Neno la Mungu.

Tatizo umeibuka kumshambulia Askofu Mwamakula badala ya kushambulia alichokisema....

Ni kweli Mch. Kimaro amefanya hayo anayotuhumiwa kufanya? Ni kweli ameonywa sana na wakuu wake lakini akakaidi? Yeye yuko juu ya kanisa ambalo ni taasisi? Aachwe tu kwa vile ni mtu maarufu?

Sasa hayo sijui ya gidamu, sijui mlichelewa kwenda kazini mkimsikiliza yanaingiaje hapa?

Kama haya anayoyasema Askofu Mwamakula ni ya kweli basi Mch. Kimaro ajishushe na aombe msamaha kwa wakubwa wake huko watamsamehe. Vinginevyo huu nao utakuwa ni mgogoro mwingine wa KKKT - kanisa lisilomaliza migogoro hata sijui tatizo huwa ni nini!
 
Acha kashfa basi ukijibu kwa busara unapungukiwa Nini?Ndio mafundisho hayo uliyofundishwa na mjivuni mwenzio Kimaro!hebu usimlinganishe Mwamakula na Watu wepesi wepesi kijana
Ad hominem attacks. Badala ya kuongelea hoja yeye anamshambulia mtoa hoja binafsi. Tena kawaka kweli kweli dah!
 
Back
Top Bottom