Mch. Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama ameishinda vita hata kabla haijaanza. Muda utazungumza

Mch. Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama ameishinda vita hata kabla haijaanza. Muda utazungumza

Vijana wengi wanaokidai ni wakristo ni wezi kweli. Sio uongo ni ukweli. Kwa nini tumumumye maneno? Kristo anao wake wasiopiga goti kwa baali ila ni wachache. Tena mno. Uaminifu kwa Wakristo wengi ni ziro japo na mimi ni mkristu. Waache kusingizia hapo
 
Lakini pia watu huwa wanasahau ukweli kuwa mchungaji yeyote naye ni mtu tu, na anaweza kufanya kosa kama mtu mwingine!! Tatizo ni kwamba kama tayari watu walikuwa wanamsagia meno kwa wivu kutokana na mafanikio yake, ikitokea wakaona kosa lolote wanakandamizia hapo hapo kumbe walikuwa na lao jambo hata kabla, bali walikuwa wanatafuta tu sababu za kuegemea!! Ndiyo maana nimesema kuwa simaanishi mch hana makosa (japo anaweza kuwa hana makosa), ila kama kuna makosa basi watu wameyatumia ili kutekeleza matakwa ya wivu wao!! Msingi wa kikristo ni KUSAMEHEANA!
Hi jamani kuna nini hapa? kwani nilazima ahubirie humo KKKT?!!!
 
Hili neno IMENILAZIMU linaonesha hajatii chochote.


Mkuu, kisheria (The Electonic Transactions Act, 2015) clip ya audio au ya video inakubalika kabisa mahakamani kama itafuata taratibu za kuiwasilisha. Huo mtazamo kuwa hazikubaliki mahakamani, sijui ni kwa mujibu wa nini
Clip kukubalika ni mpaka ichunguzwe na wataalam waliobobea ili kujua kama ni halisi/authentic! Na gharama ya kufuata mchakato huo siyo ya kitoto maana huchunguza hadi geoposition na actual date and time ambapo picha hizo zilichukuliwa. Siamini kama hgiyo clip inayotembea imepitia mchakato huo. Ndiyo maana kama mahakama haikubali ushahidi wa clip hadi ipitie mchakato huo niliousema!
 
Hili neno IMENILAZIMU linaonesha hajatii chochote.


Mkuu, kisheria (The Electonic Transactions Act, 2015) clip ya audio au ya video inakubalika kabisa mahakamani kama itafuata taratibu za kuiwasilisha. Huo mtazamo kuwa hazikubaliki mahakamani, sijui ni kwa mujibu wa nini
Kwa hiyo hii clip inayotembea imepitia huo mchakato wa kuiwasilisha? Unapozungumzia mchakato lazima ichunguzwe na wataalam waliothibitishwa kuchunguza kama clip hiyo ni halisi kwa maana watataja location/geoposition ya ilipochukuliwea, tarehe na saa ya tukio!! Huo uchunguzi siyo wa kitoto na gharama yake imekwenda shule!!!
 
Kama Kijitonyama ina sadaka kubwa, aliyehamasisha watu watoe ni Kimaro. Na siamini huyo mchungaji kiongozi atakayeletwa atakubalika kama Kimaro.

Tena, Kimaro anaweza kukubali kupata uhamisho aende atakapopelekwa, halafu baada ya miezi michache ajiuzulu uchungaji kama baadhi wa wachungaji wengine wamewahi kufanya
 
Kwa hiyo hii clip inayotembea imepitia huo mchakato wa kuiwasilisha? Unapozungumzia mchakato lazima ichunguzwe na wataalam waliothibitishwa kuchunguza kama clip hiyo ni halisi kwa maana watataja location/geoposition ya ilipochukuliwea, tarehe na saa ya tukio!! Huo uchunguzi siyo wa kitoto na gharama yake imekwenda shule!!!
Hiyo clip haipo mahakamani, ni mitandaoni tu, mwenye nayo (yaani anayeonekana videoni) ndiye anayeweza kusema kuwa ni ya uongo au la, mpaka sasa hajakana kuhusu clip hizo kuwa anayeonekana sio yeye au ni yeye ila maneno sio yake, hivyo inafanya ziaminike mpaka pale atakapozitolea neno.

Kuhusu mahakamani, hizo vitu hazikataliwi sababu kwa dunia ya leo, teknolojia imekuwa rahisi. Kazi ya kuthibitisha kuwa clip ni bandia nk ni ya anayeipinga, sio ya anayetaka kuitumia kama ushahidi. Na hana haja ya kuleta mageo position na metadata, bali anahoji tu maswali juu ya uhalali wa clip, hapo anaweza kuonesha ubandia wake. Gharama ni kumlipa wakili aulize maswali ya maana kama ya nguli Lissu au Kibatala, hivyo tu.
 
Kama Kijitonyama ina sadaka kubwa, aliyehamasisha watu watoe ni Kimaro. Na siamini huyo mchungaji kiongozi atakayeletwa atakubalika kama Kimaro.

Tena, Kimaro anaweza kukubali kupata uhamisho aende atakapopelekwa, halafu baada ya miezi michache ajiuzulu uchungaji kama baadhi wa wachungaji wengine wamewahi kufanya
Mkuu kama hufahamu Usharika wa Kijitonyama ulikuwa ndo unaongoza kwa matoleo ya sadaka na mapato kwa ujumla Kwenye Dayosis nzima kwa muda mrefu tu kabla ya ujio wa Mch. Kimaro.. umekuja kupitwa miaka ya karibuni tu hapa na Usharika wa Kimara pamoja na Mbezi Beach... Kwa hiyo kusema kuwa ujio wa mch kimaro ndo uliongeza sadaka si sahihi sana sema tu kuwa kimaro amejitahidi sana kuwaimarisha waumini kiimani na mafundisho yake mengine ya kuichumi kuwajengea waumini uwezo wa uzalizaji.
 
Clip kukubalika ni mpaka ichunguzwe na wataalam waliobobea ili kujua kama ni halisi/authentic! Na gharama ya kufuata mchakato huo siyo ya kitoto maana huchunguza hadi geoposition na actual date and time ambapo picha hizo zilichukuliwa. Siamini kama hgiyo clip inayotembea imepitia mchakato huo. Ndiyo maana kama mahakama haikubali ushahidi wa clip hadi ipitie mchakato huo niliousema!
Mahakama inataka kiapo tu kinachoeleza uhalali wa clip, kuwa ilirekodiwa lini, nani aliirekodi, alitumia vifaa gani, vilikuwa ni vizima au la, ilihifadhiwaje, nani aliyehifadhi, imehamishwaje kutoka kifaa kilichorekodi nk.. ukithibitisha hayo, clip inakubalika. Sasa wewe unayepinga kuwa sio halali ndio unaweza fanya hiyo michakato ya geoposition nk hiyo ndiyo position ya sheria kwenye mahakama zetu na si vinginevyo.
 
Niseme tu, hakuna marefu yasiyo na ncha.
Kilichokuwa kinatakiwa kufanyika ni kum demolish Kimaro tangu akiwa Usharika wa Kariakoo.

Kwa miaka mingi tumefanya mbinu na njama mbalimbali kumuondoa lakini hazikuwq na matokeo tuliyo yatarajia. Hivyo tukajaribu mbinu nyingine na nyingine tena, hatimaye leo mbuyu haujaanguka ila umemwagika.

Mara ya kwanza tulipofanya yetu akiwa pale Kariakoo alikimbia usharika na kwenda kujificha kwa Mapadre, na mapadre ndio waliofanya jitihada hadi akarudi tena usharikani, ila hii ya sasa harudi, na akirudi basi itakuwa zamu yetu kusalimu amri.

Kimaro alipokuwa Kariakoo, sio kwamba aliharibu taratibu za ibada hapana, hii ni cover tu, tunayoitumia.

Kimaro alipokuwa Kariakoo aliharibu biashara za wengi kwenye ulimwengu wa roho.

Watu walikuwa na madhabahu zao kubwa ambazo ziliprovide ulinzi wa pesa na mali, pia zikikuwa zikivuta mali kutoka kwa maboya wengine.

Alipofika Kimaro, wale ambao tulikuwa tukizivuta mali zao, wakaanza kumiminika kule kila alfajiri, ulinzi wa mali zao ukaanza kuongezeka, na zile biashara zao ambazo tulizifanya zisionekane na wateja zikaanza kuonekana, na taratibu taratibu wakaanza kukua na kutupora wateja wetu.

Kwa msio na ufahamu wa biashara, hamna biashara isiyo na madhabahu (iwe ya asili au hizo kama za Kimaro), hamna biashara isiye na kuhani, na wala hamna biashara isiyotolewa sadaka/kafara.

Watu wakaanza kufundishwa kutoa sadaka za maneneo na manuizi kwa ajili ya biashara zao, tukapata upinzani sana.

Kwa kushirikiana na wenzetu ndani ya kanisa, tukaanza figisu. Ibada hizo mpya zifutwe na ikiwezekana Kimaro ahamishwe Kariakoo.

Tukafanya Kimaro apitie magumu, tukakausha kabisa hali ya utoaji wa sadaka hadi kanisa likashindwa kulipia umeme na maji, tukahakikisha wanapitia kwenye hali ya ugumu kweli kweli.

Baadae Kimaro anajua alichokifanya, akapindua meza, hali ya uchumi wa kanisa ikaimarika sana, likawa pigo lingine kwetu.

Kipindi kile mkuu wa kanisa alikuwa yule jamaa wa Mbeya, tukafanya kila liwezekanalo ahamishwe. Ndipo akapelekwa Kijitonyama.

Zama zile Kijitonyama alikuwepo dogo mmoja anaitwa Kinyaha, hayo mambo ya ibada za asubuhi yalikuwa hayapo au yamekufa kabisa.

Ibada ilikuwa ikihudhuriwa na vizee vienne, wakizidi sana sita. Sasa alipokuja Kimaro sijajua alikuja na mguu upi, akaleta ibada za asubuhi na usiku.

Watu wakaanza kufurika, akaanza kununua nyumba za watu wetu na kuzifanya kuwa za kanisa. Kijitonyama yote ilikuwa ni ngome yetu.

Kata ya Kijitonyama ndio kata ina vijiji viwili mjini kati Dar es Salaam. Kijiji cha Mwenge na Kijiji cha Makumbusho. Jina na asili Kijitonyama sitaki kulielezea leo, lakini kaa ukijua kuwa ile ni ngome yetu na sehemu yetu ya kulia nyama na vitu vyetu vya kutuongezea nguvu. Kijitonyama ndiko kwenye madhabahu ya kuteketeza, ndio maana hata Wahindi miili yao huchomewa Kijitonyama.

Pale tulijaribu mbinu za kishushu, kuna kipindi tulitaka kumfitinisha na serikali kwa kupitia kijana aliyejinyonga kwa madeni aliyokuwa nayo, lakini alikwepa vihunzi kwa namna ya ajabu kabisa.

Kwetu sisi ni furaha, watu waharibifu aina ya KIMARO hawafai, wakakae huko vyuoni wafundishe. Na tutammaliza kwa njia hiyo.
 
Mch. Eliona Kimaro ameonesha ukomavu wa kiroho na wa kiutumishi wa hali ya juu sana. Baada ya kupewa barua ya kutakiwa kuchukua likizo ya siku 60 (ambayo hakuiomba bila shaka maana alipanga kuendesha semina), inayomlazimu kusitisha semina aliyokuwa ameianza hapo kanisani kwake, na kutakiwa kuripoti makao makuu ya KKKT baada ya likizo ili apangiwe kituo kingine, itikio na kauli yake ni hii hapa:

Amesema:
"Mimi ni Mchungaji wa Lutheran ninayeheshimu kiapo changu cha kichungaji na kuishi katika kiapo changu cha kichungaji na maadili pia ya kichungaji kwa neema ya Mungu. Kwa sababu hiyo imenilazimu kutii amri na kwenda kwenye hiyo likizo ya siku 60 na baadae kuripoti kwenye ofisi ya Askofu kama nilivyoelekezwa" Asante.


Kwa kauli hiyo keshaishinda tayari vita inayomkabili hata kama haijaanza. Ushindi mkuu kwa mtu wa Mungu ni kukubali kujivika UNYENYEKEVU! Mch. Kimaro ana nguvu sana hapo kanisani kwake na kila mtu anajua hivyo.

Angeweza kabisa kudai apewe maelezo kwa nini afanyiwe hivyo kwa ghafla na bila shaka angeweza kuliomba baraza lake la wazee lisimame kidete pamoja naye kupinga maamuzi hayo, na nina uhakika sehemu kubwa ya washirika wangemuunga mkono na pangetokea vurugu!! Yeye hakufanya yote hayo!!

Sijasema kuwa Mch Kimaro hana makosa maana sijui undani wa jambo lenyewe, lakini kuna dalili kuwa anaweza kuwa amechezewa mchezo "usio mzuri". Siyo siri kuwa Kanisa la kkkt kijitonyama ni kanisa tajiri na kuna fedha hapo!! KIla mmoja anaitazama hiyo bila kujua kazi kubwa iliyofanyika kuandaa mazingira ya kiroho na kiuwezeshaji hadi kuona matunda hayo yaliyo dhahiri kwa kila mmoja. Kanisa linaloweza kuchanga sh milioni 300 kwa nusu saa siyo mchezo. Usiniambie kuwa ni kwa sababu kuna matajiri hapo la hapana, bali wale watu wameandaliwa vizuri kwa Neno la Mungu, wamelelewa vizuri na mchungaji wao kisha kuweza kutoa maziwa mengi. Kuna mtu anaona maziwa tu lakini kumbe hayo maziwa ni matokeo ya uchungaji bora!

Watu wana asili ya WIVU!! sitashangaa kama sakata zima limejengwa juu ya wivu!! Ilikuwa ni haki ya mch Kimaro kufaidi matunda ya huduma yake hapo kama mchungaji. Hakuna namna ambayo mchungaji hawezi kufaidi maziwa ya kundi analochunga. Sasa wengine hiyo inawauma!! Biblia inasema hivi:

"Ni askari gani aendaye vitani wakati wowote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Je ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi. 1Wakorintho 9:7?"

Ninafahamu katika mazingira haya kuna uwezekano mkubwa wa Mch. Kimaro kutuhumiwa "kula pesa za kanisa" ili kuhalalisha hatua zilizochukuliwa, lakini Mungu wa mbinguni anajua yote!! Kwa wengine kwa mchungaji kunywa katika maziwa ya kundi analochunga kama Biblia inavyoagiza huko wanadai ni "kula pesa za kanisa".

Lakini ukweli ni kwamba kazi ya mchungaji ni pamoja na kula pesa au sadaka za kanisa. Mchungaji akila maana yake Mungu amekula!! Huo ni ukweli tukubali tusikubali!

Yawezekana kuna mtu ana mpango wa kula matunda ya jasho la mwingine, Mungu anajua!

Namtia moyo mch Kimaro kuwa tayari keshaishinda vita kabla hata haijaanza na Mungu atakuwa pamoja naye popote atakapoenda!! Baraka za Kweli za Mungu huwa hazifuatwi bali huwa ZINAMFUATA MTU WA MUNGU!! Ni suala la muda tu watu watalishuhudia hili.

Mch. Kimaro nenda kapige kazi popote Na baraka za Mungu zitakufuata!!! Kama kuna tatizo la msingi napo usikose kulitengeneza kwanza na Mungu atakuwa pamoja nawe!!
Huko Ofisi ya Askofu aangalie wasije wakamuwekea sumu, Malasusa na Dk. Shoo hawataki mtu awazidi umaarufu achukue uaskofu wao. Wana chuki sana kuliko hata yule mwovu.

Aangalie hizo chai na soda
 
Niseme tu, hakuna marefu yasiyo na ncha.
Kilichokuwa kinatakiwa kufanyika ni kum demolish Kimaro tangu akiwa Usharika wa Kariakoo.

Kwa miaka mingi tumefanya mbinu na njama mbalimbali kumuondoa lakini hazikuwq na matokeo tuliyo yatarajia. Hivyo tukajaribu mbinu nyingine na nyingine tena, hatimaye leo mbuyu haujaanguka ila umemwagika.

Mara ya kwanza tulipofanya yetu akiwa pale Kariakoo alikimbia usharika na kwenda kujificha kwa Mapadre, na mapadre ndio waliofanya jitihada hadi akarudi tena usharikani, ila hii ya sasa harudi, na akirudi basi itakuwa zamu yetu kusalimu amri.

Kimaro alipokuwa Kariakoo, sio kwamba aliharibu taratibu za ibada hapana, hii ni cover tu, tunayoitumia.

Kimaro alipokuwa Kariakoo aliharibu biashara za wengi kwenye ulimwengu wa roho.

Watu walikuwa na madhabahu zao kubwa ambazo ziliprovide ulinzi wa pesa na mali, pia zikikuwa zikivuta mali kutoka kwa maboya wengine.

Alipofika Kimaro, wale ambao tulikuwa tukizivuta mali zao, wakaanza kumiminika kule kila alfajiri, ulinzi wa mali zao ukaanza kuongezeka, na zile biashara zao ambazo tulizifanya zisionekane na wateja zikaanza kuonekana, na taratibu taratibu wakaanza kukua na kutupora wateja wetu.

Kwa msio na ufahamu wa biashara, hamna biashara isiyo na madhabahu (iwe ya asili au hizo kama za Kimaro), hamna biashara isiye na kuhani, na wala hamna biashara isiyotolewa sadaka/kafara.

Watu wakaanza kufundishwa kutoa sadaka za maneneo na manuizi kwa ajili ya biashara zao, tukapata upinzani sana.

Kwa kushirikiana na wenzetu ndani ya kanisa, tukaanza figisu. Ibada hizo mpya zifutwe na ikiwezekana Kimaro ahamishwe Kariakoo.

Tukafanya Kimaro apitie magumu, tukakausha kabisa hali ya utoaji wa sadaka hadi kanisa likashindwa kulipia umeme na maji, tukahakikisha wanapitia kwenye hali ya ugumu kweli kweli.

Baadae Kimaro anajua alichokifanya, akapindua meza, hali ya uchumi wa kanisa ikaimarika sana, likawa pigo lingine kwetu.

Kipindi kile mkuu wa kanisa alikuwa yule jamaa wa Mbeya, tukafanya kila liwezekanalo ahamishwe. Ndipo akapelekwa Kijitonyama.

Zama zile Kijitonyama alikuwepo dogo mmoja anaitwa Kinyaha, hayo mambo ya ibada za asubuhi yalikuwa hayapo au yamekufa kabisa.

Ibada ilikuwa ikihudhuriwa na vizee vienne, wakizidi sana sita. Sasa alipokuja Kimaro sijajua alikuja na mguu upi, akaleta ibada za asubuhi na usiku.

Watu wakaanza kufurika, akaanza kununua nyumba za watu wetu na kuzifanya kuwa za kanisa. Kijitonyama yote ilikuwa ni ngome yetu.

Kata ya Kijitonyama ndio kata ina vijiji viwili mjini kati Dar es Salaam. Kijiji cha Mwenge na Kijiji cha Makumbusho. Jina na asili Kijitonyama sitaki kulielezea leo, lakini kaa ukijua kuwa ile ni ngome yetu na sehemu yetu ya kulia nyama na vitu vyetu vya kutuongezea nguvu. Kijitonyama ndiko kwenye madhabahu ya kuteketeza, ndio maana hata Wahindi miili yao huchomewa Kijitonyama.

Pale tulijaribu mbinu za kishushu, kuna kipindi tulitaka kumfitinisha na serikali kwa kupitia kijana aliyejinyonga kwa madeni aliyokuwa nayo, lakini alikwepa vihunzi kwa namna ya ajabu kabisa.

Kwetu sisi ni furaha, watu waharibifu aina ya KIMARO hawafai, wakakae huko vyuoni wafundishe. Na tutammaliza kwa njia hiyo.
Umeandika vitu gani mkuu?
 
Vijana wengi wanaokidai ni wakristo ni wezi kweli. Sio uongo ni ukweli. Kwa nini tumumumye maneno? Kristo anao wake wasiopiga goti kwa baali ila ni wachache. Tena mno. Uaminifu kwa Wakristo wengi ni ziro japo na mimi ni mkristu. Waache kusingizia hapo

Samaleko Mkuu
 
Clip kukubalika ni mpaka ichunguzwe na wataalam waliobobea ili kujua kama ni halisi/authentic! Na gharama ya kufuata mchakato huo siyo ya kitoto maana huchunguza hadi geoposition na actual date and time ambapo picha hizo zilichukuliwa. Siamini kama hgiyo clip inayotembea imepitia mchakato huo. Ndiyo maana kama mahakama haikubali ushahidi wa clip hadi ipitie mchakato huo niliousema!

Umemsikia akikanusha Kua Sio Clip Zake??
 
Umeshaiona clip inayomhusu, au umeamua kuja na porojo tu..
Jee wewe umesoma na kuelewa mleta uzi alichomaanisha? Ndiyo maana mnashindwa mitihani kizembe,soma na uelewe kilichoandikwa kabla hujajibu
 
Samaleko Mkuu
Braza mimi Mkristo. Nimeona vingi mno. Wakristo tumeharubu mfumo wa nchii hii na kumuaibisha Kristo. Mfumo huu kila mtu ni mwizi. Waislamu wa Zanzibar wanaweza kuwa na changamoto nyingi ila uwizi sio mojawapo. Siwasemei wa bara maana wamekua ndani ya mfumo huu wa kikristo. Tunamuabisha Yesu mno. Nahisi akitazama kutoka mbinguni maumivu ni makali mno. Namuomba anioe neema ya kutokumuaibisha.
 
Huko Ofisi ya Askofu aangalie wasije wakamuwekea sumu, Malasusa na Dk. Shoo hawataki mtu awazidi umaarufu achukue uaskofu wao. Wana chuki sana kuliko hata yule mwovu.

Aangalie hizo chai na soda
Tatizo la karibu kabisa pale ni Mch. Anna!!!
Sijui why haoni ila yule bi mkubwa yuko pale kwa mkakati maalum kabisa.ndio aliemchomakwa mashtaka ya siri Jimboni kipindi kile.Bahati nzuri aliekua kaimu katibu ni yule mzee wa Kimara ambae ni jamaa yake sana Kimaro.Yyule mama kakubali kutumiwa na shetani kuharibu kazi ya Mungu
 
Tatizo la karibu kabisa pale ni Mch. Anna!!!
Sijui why haoni ila yule bi mkubwa yuko pale kwa mkakati maalum kabisa.ndio aliemchomakwa mashtaka ya siri Jimboni kipindi kile.Bahati nzuri aliekua kaimu katibu ni yule mzee wa Kimara ambae ni jamaa yake sana Kimaro.Yyule mama kakubali kutumiwa na shetani kuharibu kazi ya Mungu
Katika kipindi tulichonacho ni muhimu kusimama ktk kujua Mungu kibinafsi, maana ukimtegemea mchungaji akaondoka Imani inaweza yumba Sana, maana kipindi hiki wachungaji, maskofu wengi wapo kivyeo na si kumtumikia Mungu, ndio maana unaweza kuta mashtaka ya kupiga hela za kanisa at kutapeli waumini.. Na mbaya zaidi baadhi ya watumishi hao hao wapo ktk vyama vya waabudu mashetani. .. Hivyo ni rahisi kuharibu yeyote anaetishia himaya ya shetani makanisani
 
Vijana wengi wanaokidai ni wakristo ni wezi kweli. Sio uongo ni ukweli. Kwa nini tumumumye maneno? Kristo anao wake wasiopiga goti kwa baali ila ni wachache. Tena mno. Uaminifu kwa Wakristo wengi ni ziro japo na mimi ni mkristu. Waache kusingizia hapo
Hv ni kweli!! Wale wezi vibaka,panyaroad, mijambazi asilimia kubwa ni wa imani gani?
La msingi tukubaliane kuwa hakuna dini inayofundisha wizi na utapeli. Ni malezi na kiwango cha Roho wa Mungu alichonacho mtu. Hivyo inawezekana kwa kila dini bado vibaka na matapeli wapo ikiwa tu kibinafsi hawakukuzwa kwa malezi mazuri.
 
Back
Top Bottom