TANZIA Mchekeshaji Jumanne Alela maarufu kama "Mzee Matata" wa Mizengwe afariki dunia

TANZIA Mchekeshaji Jumanne Alela maarufu kama "Mzee Matata" wa Mizengwe afariki dunia

Poleni ndugu , jamaa na marafiki.

Mizengwe kipindi changu hicho no kukosa ITV Jumapili 21:05 - 21:30.
 
Taarifa zinaeleza kwamba amefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Muhimbili alikolazwa tangu tarehe 13 June

========


MWIGIZAJI wa Kikundi cha Maigizo cha Kashkashi kinachorusha mchezo wao wa kuchekesha wa Mizengwe kupitia Televisheni ya ITV, Jumanne Alela almaarufu Mzee Matata amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Juni 16, 2021 Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar alipokuwa amelazwa kwa matibabu toka Juni 13, 2021..

Kwa mujibu wa mwigizaji maarufu nchini, @madebelidai, mazishi ya Mzee Matata yatafanyika kesho kwenye Makaburi ya Buguruni,Malapa jijini Dar.

“Mwanatasnia mwenzetu Mzee Jumanne Alela (Mzee Matata) yatafanyika kesho saa saba mchana kwenye Makaburi ya Buguruni-Malapa.

“Msiba upo kwa ndugu zake, Chamazi kwa Mkongo (jijini Dar),” taarifa kutoka kwa @madebelidai.

Chanzo: Global Publishers
R.I.P Kwake japo alionekana ni Mdhaifu ( Mgonjwa ) Kitambo sana tu hata kwa Kumtizama Runingani.
 
Mara ya mwisho kuangalia mizengwe wiki kama 2 hivi waliyoigiza kuhusu mke kutaka kumpa mme talaka na mme kudai mgawanyo wa mali marehemu akiwa mwenyekiti wa mtaa hali yake ya kiafya haikuwa nzuri alikuwa kaisha na kuzeeka sana mpk nikawaza hili lililomtokea

Siku zake zimetimia Bwana awafariji familia
 
Mara ya mwisho kuangalia mizengwe wiki kama 2 hivi waliyoigiza kuhusu mke kutaka kumpa mme talaka na mme kudai mgawanyo wa mali marehemu akiwa mwenyekiti wa mtaa hali yake ya kiafya haikuwa nzuri alikuwa kaisha na kuzeeka sana mpk nikawaza hili lililomtokea

Siku zake zimetimia Bwana awafariji familia
Naam, hata mimi niliiona hiyo, japo sikufikiria kufa ila nilijisemea mzee wangu amedhoofika sijui Masigara wanayovuta!!!
 
Pumzika kwa amani mzee wetu. Alikuwa na style ya kipekee haifanani na comedian yeyote tz, nakumbuka ile shoe shiner wa pita usemwe
 
Yuko ndugu yangu kwake ni huko buza kwa mama kibonge , lakini alipofariki alizikwa makaburi ya Mburahati , kwa maelezo kwamba mama yake mzazi alizikwa kwenye makaburi hayo enzi hizo , kwahiyo kunakuwa na vijisababu fulani hivi visivyo na mashiko yoyote yale .
Wachaga wanaofia Dar, ni kama asilimia mbili tu, huzikwa Dar, wengi husafirishwa kwenda kuzikwa kwao.
 
Back
Top Bottom