Mchele kutoka nje na hatma ya wakulima wetu

Mchele kutoka nje na hatma ya wakulima wetu

Ukiona hivyo jua Kuna bossy nmoja ana meli inaleta mzigo zaidi ya tano elfu 40 ndio wamepush push hadi kupata mzigo kupata kushushwa.

Ila bora iwe soko huria tuu. Maana watu sahivi wanajiongezea bei kama serikali walivyoongeza bei ya mafuta
 
Mchele wa plastic huo.

Kansa kwa sana. Nunua mchele wetu wa kuzalisha wenyewe.
Mshapaniki tayari! Mtashusha tu bei, mtake msitake. Hamuwezi kutuuzia mchele kilo kwa shilingi 3600!! Hui ni uhujumu uchumi.

Na aliyeagiza hizo tani elfu 90, nampa pongezi za dhati. Na naamini atakuwa siyo yule kilaza Hussein Bashe.
 
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
Mchele wa Kyela na Kilosa kilo 3000?. Potelea mbali Mchina na mhindi alete tu
 
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
Hakutakuwa na athari yo yote kwa mkulima kwani ataendelea kuuza mchele wake bila tatizo.

Bei za sasa za mchele ni za wizi na ulanguzi hivyo mchele wa nje ukija wakulima watauza kwa bei halisi.
 
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
Wakulima wa nyakati hizi hawana akili kabisa.. kwao ni bora kushabikia mfumuko wa bei huku yeye mwenyewe haijui kesho yake na mazao yake yatakayomchwea ndani..
 
Mmoja anasema:
Mama hawezi kukubali wakulima wa nchi hii wakiumia tena, na maghala ya serikali yana chakula cha kutosha karibu tani 150 elfu...☺
Mwingine anasema:
Mama ametoa kibali cha kuagiza tani 90 elfu ya chakula kutoka nje, kwasababu hawezi kukubali kuona wananchi wake wanaumia kwa mfumuko wa bei ya chakula...😊
Serikali hii ni ya kipwagu na pwaguzi sasa kama maghala yamejaa kwa nini chakula hicho kisiuzwe ili kukabiliana na ugumu wa maisha uliyopo?
 
Mmoja anasema:
Mama hawezi kukubali wakulima wa nchi hii wakiumia tena, na maghala ya serikali yana chakula cha kutosha karibu tani 150 elfu...☺
Mwingine anasema:
Mama ametoa kibali cha kuagiza tani 90 elfu ya chakula kutoka nje, kwasababu hawezi kukubali kuona wananchi wake wanaumia kwa mfumuko wa bei ya chakula...😊
Wote hao Ni sirikali moja ya CCM na wanataka tuwaamini! Ni hizi tu mapoyoyo Kama Mwashambwa yalikua yanasifia kila kauli! Sasa Hilo la Thailand!
 
Una uhakika gani kama huo mchele unaoletwa ni makapi? Nyinyi mchele mnao wauzia Wakenya na Wasomali ni makapi?

Wewe kijana wa Moo mbona unaleta story za kufikirika! Unataka kusema hakuna mamlaka ya chakula na dawa nchini kwa ajili ya kuchunguza ubora wa huo mchele!
Muulize kwani Ni Mara ya know kwanza Tanzania kuingiza mchele kutoka nje!
Au umri na exposure itakua tatizo!?
Tanzania tuna mamlaka mbalimbali zinazosimamia uingizaji wa bidhaa ikiwemo bidhaa za chakula, dawa na vinywaji!
Uzuri wa serikali yetu Ni kutengeneza tatizo na baadae kulitatua!
 
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
Watanzania nawashangaa Sana. Mmesema kwamba Wakulima wanaruhusiwa kuuza mazao Yao popote pale Duniani na kwa bei wanayoitaka (Waziri WA Kilimo). Kama ni hivyo basi waacheni na Walaji wanunue mazao kutoka popote pale Duniani kwa bei ambayo wanaona inafaa.

Haiingii akilini mfungue mipaka ya kuuza CHAKULA nje tu na kusababisha mfumko WA bei za vyakula nchini Huku Mmefunga mipaka kwa wafanyabiashara kuingiza vyakula kutoka nje ya nchi ili kupunguza huu mfumko WA bei. Pakistan na Brazil na India Kuna Mchele WA kutosha na kwa bei chee. Cha msingi Serikali iangalie ubora na usalama WA vyakula kutoka nje kabla ya kuingia nchini.
 
Mtajua wenyewe. Nyinyi mnaona sawa kutuuzia kilo ya mchele kwa shilingi 3600! Si mlifurahia soko kufunguliwa, na hivyo kuuza chakula chenu nje ya nchi kwa bei mnayotaka!!

Sasa inakuwaje mnaanza tena kupagawa mchele kuingizwa nchini? Si ndiyo soko huria lenyewe hili!!! Nyinyi nendeni mkauze mchele wenu nje ya nchi kwa bei kubwa, na sisi tutanunua huo mchele wq kutoka nje kwa bei nafuu.

Ni wakati sasa wa kila mtu kushinda mechi zake. Msianze kulia lia hapa.
Wauze hata 5000 kilo moja, mlaji atachagua anunue wa ndani au wa nje, tusipangiane,
Hata bidhaa za ujenzi unachagua kununua nondo za Mrusi Kamaka au mhindi MM Steel

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
Mlipokuwa mnasikiliza ngonjera za Bashe niliwashangaa sana. Mpaka mwishoni mwa Novemba hakuna mkulima aliyekuwa na mpunga Bali walanguzi ambao wana connection na kina Bashe. Kwa sasa wameshauza mizigo yao ndo wanaruhusu mchele toka nje. Msidanganyike kirahisi eti Wakulima wataathirika.
 
Kwa hiyo kwako bora tuanze kula makapi ya bei rahisi, umenikumbusha wale sangara na sato wa ziwa Victoria waliokuwa wakipandishwa ndege kwenda ulaya, huku wabongo tunakula mapanki, hakika tumeshazoeshwa kula mitumba, afya kwetu sio issue tena, muhimu tumbo lijae!.
Kama kipato ni duni, kuna watakaonunua tu, hata mtaani kuna familia inatamani kula kuku, lakini wanaishia kula miguu, utumbo na vichwa,
Maisha hayafanani mkuu, kuna wengine wanakosa na kulala njaa, hata huo mchele mbovu hawaupati,

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Wauze hata 5000 kilo moja, mlaji atachagua anunue wa ndani au wa nje, tusipangiane,
Hata bidhaa za ujenzi unachagua kununua nondo za Mrusi Kamaka au mhindi MM Steel

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
Wakulima uchwara wameshapagawa tayari kutokana na hilo tamko. Maana walijiandaa kutuangamiza kwa bei zao za kubambika. Eti wanataka soko huria kwa upande wao tu! Hopeless kabisa.

Wao wakauze mchele wao Kenya na Somalia kwa bei waitakayo, na sisi tutakula huo mchele wa kutoka nje kwa bei tunayo imudu. Na hii ndiyo maana halisi ya soko huria.
 
Back
Top Bottom