Mchezaji wa Simba hawezi kula bata kila siku na wachezaji wa Yanga akabaki salama

Mchezaji wa Simba hawezi kula bata kila siku na wachezaji wa Yanga akabaki salama

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Nakumbuka mwanzoni mwa msimu huu nilipongeza usajili mzuri waliofanya Simba ila nikatoa angalizo moja kuwa wachezaji wa Simba wapigwe marufuku kuzoeana na wachezaji wa Yanga nje ya uwanja.

Naelewa hawa wachezaji wana maisha nje ya uwanja na naelewa pia wengine wana historia zinazoingiliana kwa hiyo mahusiano nje ya uwanja hayaepukiki, ila ni vizuri tukajua uhalisia wa mpira wetu na tuambiane ukweli.

Nakumbuka kushangaa Aubin Kramo kuendeleza ukaribu na kina Yao na Pacome kiasi kwamba alikuwa anaenda hadi airport kumpokea Pacome. Mwisho wa siku wote tunajua story yake.

Huyu Ahoua naye siku zake pale Simba zinahesabika. Nasikia naye anaendeleza ukaribu na wachezaji hao hao wa Yanga. Nadhani viongozi wa Simba hawakuona haja ya kumpa mwongozo ila athari zake tunaziona sasa. Kocha Fadlu naye akiendeleza kumkumbatia ataondoka yeye kwanza halafu huyo Ahoua atamfuata.

Ifike wakati tuambiane ukweli wanasimba. Kuwa na mchezaji kama huyu uwanjani ni kujikaba wenyewe. Ni kuwapa pressure mabeki wako kwa dakika 90 maana mnakuwa siyo tishio kule mbele. Mwisho wa siku kina Ateba wanaonekana butu kumbe hawalishwi nafasi zozote za maana.

NYONGEZA: Pamoja na kwamba tunasema kocha asiingiliwe ila naye ni binadamu. Anaweza kuleta chuki binafsi katika kazi ikamfanya aharibu timu kwa kuwapiga pini wachezaji au kuwabeba wasiostahili. Yuko wapi Karabaka mchezaji aliyethibitisha ana bahati ya kufunga? Mbona Awesu hapangwi katika mechi anazoonekana kabisa anaweza kusaidia?
 
Yani unawaacha Mavambo na Mukwala nje unaanza na Ngoma na Ahoua wakati ile timu ndio inaonekana tishio kuliko zote kwenye kundi letu tena wako kwao, simba bado inahitaji maboresho ya kikosi wasibweteke kama majirani zao kujiona walishamaliza kusajili na wana kikosi kipana laiti kama dili la kina Foday Trawally, Abdelhay Forsy, Philippe Kinzumbi na Jonathan Alukwu lingetiki basi baada ya dirisha dogo simba ingekuwa moto wa kuotea mbali, ila wacha tuone kina Mpanzu na Kimvuidi watakuwa na nini cha kuoffer hapo msimbazi
 
Ama kweli umbumbumbuni Kuna ma Mbumbumbu. Kama hufahamu maisha ya wachezaji na makocha ni ya kawaida kabisa na nitofauti na ushabiki wenu wa kishamba na chuki.

Wachezaji haijalishi mambo yenu ya timu pinzani, wao upinzani wao ni uwanjani tu na ndio maana mechi iki isha bila kujali Matokeo wanapongezana.
Na wanamaisha ya ukaribu Sana kuliko mashabiki.
 
Nakumbuka mwanzoni mwa msimu huu nilipongeza usajili mzuri waliofanya Simba ila nikatoa angalizo moja kuwa wachezaji wa Simba wapigwe marufuku kuzoeana na wachezaji wa Yanga nje ya uwanja.

Naelewa hawa wachezaji wana maisha nje ya uwanja na naelewa pia wengine wana historia zinazoingiliana kwa hiyo mahusiano nje ya uwanja hayaepukiki, ila ni vizuri tukajua uhalisia wa mpira wetu na tuambiane ukweli.

Nakumbuka kushangaa Aubin Kramo kuendeleza ukaribu na kina Yao na Pacome kiasi kwamba alikuwa anaenda hadi airport kumpokea Pacome. Mwisho wa siku wote tunajua story yake.

Huyu Ahoua naye siku zake pale Simba zinahesabika. Nasikia naye anaendeleza ukaribu na wachezaji hao hao wa Yanga. Nadhani viongozi wa Simba hawakuona haja ya kumpa mwongozo ila athari zake tunaziona sasa. Kocha Fadlu naye akiendeleza kumkumbatia ataondoka yeye kwanza halafu huyo Ahoua atamfuata.

Ifike wakati tuambiane ukweli wanasimba. Kuwa na mchezaji kama huyu uwanjani ni kujikaba wenyewe. Ni kuwapa pressure mabeki wako kwa dakika 90 maana mnakuwa siyo tishio kule mbele. Mwisho wa siku kina Ateba wanaonekana butu kumbe hawalishwi nafasi zozote za maana.

NYONGEZA: Pamoja na kwamba tunasema kocha asiingiliwe ila naye ni binadamu. Anaweza kuleta chuki binafsi katika kazi ikamfanya aharibu timu kwa kuwapiga pini wachezaji au kuwabeba wasiostahili. Yuko wapi Karabaka mchezaji aliyethibitisha ana bahati ya kufunga? Mbona Awesu hapangwi katika mechi anazoonekana kabisa anaweza kusaidia?
Nyie mkubali mlifanya usajili wa wachezaji wa Bei nafuu na viwango vyao ni vinaendana na pesa mliyowapa,,habari za ukaribu na wachezaji wa yanga ni porojo tu Ina maana karibu wachezaji wote Wenye viwango vibovu Wana ukaribu na wachezaji wa yanga? Kina mutale, barua, charabou, Ngoma, chasambi wote hao ni ukaribu wao na wachezaji wa yanga? Ebu acheni kujizima data kwani Mpira atuangalii au unaangalia wewe tu?
 
Yani unawaacha Mavambo na Mukwala nje unaanza na Ngoma na Ahoua wakati ile timu ndio inaonekana tishio kuliko zote kwenye kundi letu tena wako kwao, simba bado inahitaji maboresho ya kikosi wasibweteke kama majirani zao kujiona walishamaliza kusajili na wana kikosi kipana laiti kama dili la kina Foday Trawally, Abdelhay Forsy, Philippe Kinzumbi na Jonathan Alukwu lingetiki pengine baada ya dirisha dogo simba ingekuwa moto wa kuotea mbali, ila wacha tuone kina Mpanzu na Kimvuidi watakuwa na nini cha kuoffer hapo msimbazi
Kuna vitu navikubali kwa Ngoma ila kumchezesha namba 6 nadhani siyo sahihi. Tulimtegemea msimu uliopita ila timu ilikuwa inafungwa magoli daily.

Kosa la kwanza lililofanyika jana ni kujaza beki za kati. Hakukuwa na haja ya kufanya hivyo. Matokeo yake tunafungwa magoli ya ajabu maana watu hawajazoea kurundikwa wote wacheze pamoja.
 
Nyie mkubali mlifanya usajili wa wachezaji wa Bei nafuu na viwango vyao ni vinaendana na pesa mliyowapa,,habari za ukaribu na wachezaji wa yanga ni porojo tu Ina maana karibu wachezaji wote Wenye viwango vibovu Wana ukaribu na wachezaji wa yanga? Kina mutale, barua, charabou, Ngoma, chasambi wote hao ni ukaribu wao na wachezaji wa yanga? Ebu acheni kujizima data kwani Mpira atuangalii au unaangalia wewe tu?
Ww wachezaji wako wa bei ghali wako wapi...mnajikutaga mnajua bei za watu lakini bei zenu aaaaah
 
Yani unawaacha Mavambo na Mukwala nje unaanza na Ngoma na Ahoua wakati ile timu ndio inaonekana tishio kuliko zote kwenye kundi letu tena wako kwao, simba bado inahitaji maboresho ya kikosi wasibweteke kama majirani zao kujiona walishamaliza kusajili na wana kikosi kipana laiti kama dili la kina Foday Trawally, Abdelhay Forsy, Philippe Kinzumbi na Jonathan Alukwu lingetiki basi baada ya dirisha dogo simba ingekuwa moto wa kuotea mbali, ila wacha tuone kina Mpanzu na Kimvuidi watakuwa na nini cha kuoffer hapo msimbazi
Kimvuidi ndo nani bi dada...
 
Kuna vitu navikubali kwa Ngoma ila kumchezesha namba 6 nadhani siyo sahihi. Tulimtegemea msimu uliopita ila timu ilikuwa inafungwa magoli daily.

Kosa la kwanza lililofanyika jana ni kujaza beki za kati. Hakukuwa na haja ya kufanya hivyo. Matokeo yake tunafungwa magoli ya ajabu maana watu hawajazoea kurundikwa wote wacheze pamoja.
Sure iliwanyima usiriazi kwny kazi...
 
Nyie mkubali mlifanya usajili wa wachezaji wa Bei nafuu na viwango vyao ni vinaendana na pesa mliyowapa,,habari za ukaribu na wachezaji wa yanga ni porojo tu Ina maana karibu wachezaji wote Wenye viwango vibovu Wana ukaribu na wachezaji wa yanga? Kina mutale, barua, charabou, Ngoma, chasambi wote hao ni ukaribu wao na wachezaji wa yanga? Ebu acheni kujizima data kwani Mpira atuangalii au unaangalia wewe tu?
Hauna hoja
 
Ww wachezaji wako wa bei ghali wako wapi...mnajikutaga mnajua bei za watu lakini bei zenu aaaaah
Class ya wachezaji wa yanga uwezi kulinganisha na wachezaji wa Simba ata siku Moja,,kushuka kwa viwango vyao akuondoi class waliyonayo ulijue hilo,,nitajie wachezaji wenu ata watano Wenye class kama wachezaji wa yanga!
 
Class ya wachezaji wa yanga uwezi kulinganisha na wachezaji wa Simba ata siku Moja,,kushuka kwa viwango vyao akuondoi class waliyonayo ulijue hilo,,nitajie wachezaji wenu ata watano Wenye class kama wachezaji wa yanga!
Kwanza define "class". Hatuwezi kuwasikiliza nyie tena maana imeshaonekana mnaponda wachezaji wa Simba halafu Simba ikiwaacha mnawachukua.
 
Back
Top Bottom