Mchimbaji mdogo Laizer akabidhi jiwe lingine la Tanzanite lenye uzito wa kilo 6.33 Serikalini

Mchimbaji mdogo Laizer akabidhi jiwe lingine la Tanzanite lenye uzito wa kilo 6.33 Serikalini

Hofu Zangu ni hizi:

1. Very soon serikali itautaifisha huo mgodi wa Laizer,
2. Thamani ya Tanzanite Tanzania itapungua sana due to forces of supply and demand,
3. Itafik Mahala serikali itashindwa kununua hayo makilo yaTanzanite siku zinazosonga ikiwa Laizer atazidi kuyapakuwa wiki hadi wiki.
Mmh! Mkuu unataka kunambia supply ya Tanzanite itakuwa kubwa kuliko demand yake? Hili linawezekana vipi mkuu?
 
safi upo sahihi, mimi ndo nipo huku mirerani, hili walilificha ili wakauze nje, na wangepata hela nyingi zaidi ya lile ka kwanza, sema tu muingiliano uliotokea huko chini ndo siri ikafichuka na serikali kuingilia kati. Na pia muelewe laizer sio kama yeye ndo anapata hela kubwa kuliko wote ni hapana,, laizer yeye ni mwenye mgodi, ila kuna wahudumiaji mgodi na hao huwa wana percent kubwa zaidi ya lizer,, unaweza kuta kwenye ile bilioni saba yeye laizer akaambulia tatu tu, na nne ikaenda kwa wahudumiaji,, ila hili jiwe la sasa lina mgogoro na watu wanne, ni stori ndefu nikielezea hapa, na sivuri kiusalama.
Acha kuchanganya mafile hivi unajua Laizer week 2 au 3 zilizopita alitoa mawe likiwemo hilo la kilo 6?
 
Inategemea na level ya uwekezaji.. anatumia vifaa gani na ukubwa wa eneo lake. Madini unaweza ukashangaa umechimba hata kwenye ukubwa wa chumba cha kulala ukapata jiwe.
Hujamwelewa jamaa ww,huyo Laizer ana shopping mall maeneo ya sakina utamwita maskini?
 
Wanasemaga kuna mkanda..ukiupata huo we ni billionea mwanzo mwisho.. ndio mabilionea kina msuya waliuana sababu hiyo..huyo laizer ashukuru ulinzi umeimarishwa.
Nan anasemaga kuna mkanda?
 
hayo mawe wanayapata tangu zamani, zaidi ya kilo hizo wanazotangaza, ila walikua wanayavunja vunja, wanagawana kila mtu apate,, na tanzanite one ndo alikua anayatoa mengi tu, ila huwa anayavunjavunja vipande vipande, kwa sababu za kibiashar, ni stori ndefu nikielezea sababu za biashara kivipi.
- Unajua kwamba gemstones ukizivunja thamani yake inapungua?

- Unajua kwamba gemstone ikiwa na mipasuko bei inapungua.?

- unajua kwamba jiwe la kilo 5 lina thamani zaidi ya mara mbili ya mawe madogo madogo yenye jumla ya kilo 5?

- Ni sababu zipi hizo za kibiashara zinazosababisha mawe yavunjwe? Au unataka kupotosha watu humu.
 
Mmh! Mkuu unataka kunambia supply ya Tanzanite itakuwa kubwa kuliko demand yake? Hili linawezekana vipi mkuu?

Inawezekana kwamba huo mgodi umefika kwenye mkanda wa madini yenyewe maana kila wiki nI kilo zinapakuliwa... Serikali wakiamua ku-commercialise kwa kuleta vifaa bora vya kuchimbia kuna uwezekana wa kufanya over production na hii ikifanyika ndio maana bei yaweza kushuka humu Tanzania na hata pia kwenye soko la Dunia huko Antwerp- ni maoni tu , si lazima iwe kweli...
 
Inawezekana kwamba huo mgodi umefika kwenye mkanda wa madini yenyewe maana kila wiki nI kilo zinapakuliwa... Serikali wakiamua ku-commercialise kwa kuleta vifaa bora vya kuchimbia kuna uwezekana wa kufanya over production na hii ikifanyika ndio maana bei yaweza kushuka humu Tanzania na hata pia kwenye soko la Dunia huko Antwerp- ni maoni tu , si lazima iwe kweli...
Ni kweli unachosema lakini hofu yangu ni je uhitaji wa Tanzanite kwenye soko ukoje kiasi kwamba kuwepo na over production ya kupelekea deflation ya Tanzanite kiasi hicho? Mimi sidhani kama yanaweza kuwa mangi kiasi hicho mkuu.
 
Kwahi
Kwahiyo Leo wewe ni mchumi Kitaaluma? Maana jamiiforums unajitambulisha kwamba wewe ni usalama wa taifa (kachero) japo wapo ut wachumi 🤣🤣🤣🤣

Niwekee hapa ' Ushahidi ' wako wote ulionao au kutoka kwa Watu wengine kwamba Mimi GENTAMYCINE nimeshawahi ' Kujitanabaisha ' hapa Jamii Forums au hata kokote kule ni Mwana Usalama wa Taifa. Kama unao uweke hapa ili leo ' Niumbuke ' na ikiwezekana hata hao ' Watendaji ' wenyewe husika wa hiyo Taasisi ambao wapo wengi hapa na baadhi yao wananijua hadi ninapolala waje wanikamate na wakanishitaki kwa Kosa la ' Impersonation ' ili Mimi nitumike kama Mfano kwa wengine. Katika Maelezo yako mengi tu juu yangu kila mara huwa ' Unanidhihaki ' kuwa ni ' Mwendawazimu ' sasa hivi Idara yenye Heshima Kubwa na Ufanisi kama TISS inaweza ' Kuajiri ' Mtu kama Mimi. TISS ama kuwa nami au hata Kuniajiri itakuwa ni ' Tiketi ' ya Wao ' Kujidhalilisha ' na Kujishusha ' Thamani ' yao kwani sina hata 1% ya kuwa Miongoni mwao. Namalizia kwa Kusisitiza zaidi Kwako kuwa umesema Mimi huwa najitambulisha na nimewashawahi Kujitamulisha hapa kuwa ni Mtu wa Idara ( TISS ) hivyo nakuomba uweke hapa kila Kitu hadharani ili Vijana wa DG Afande Diwani Athuman Msuya waje ' wanidake ' hapa nilipo ambapo nakuthibitishia kuwa wanajua nilipo hadi ninapolala hivyo ' Kunikamata ' Mimi ni Kitu cha Sekunde tu kisha ' waniadabishe ' sawa? Pumbavu!
 
Kwani wewe ulitaka liuzweje ili isiwe kiki mkuu?
Alafu vipi zile habari za kupigwa kwenye bei ya hayo madini sijasikia likizungumzwa kwenye hili jiwe au tumsubiri Lema atoe neno tuunge mkono hoja?

Biashara ya kufanyia kwenye TV Ni Kiki. Kama ameridhika kuuza kwa serikali kwa bei hiyo, hiyo ni haki yake, ila angeliuza nje angepata pesa nyingi kuliko hizo anazilipwa na serikali. Hilo ni simple mbona.
 
Biashara ya kufanyia kwenye TV Ni Kiki. Kama ameridhika kuuza kwa serikali kwa bei hiyo, hiyo ni haki yake, ila angeliuza nje angepata pesa nyingi kuliko hizo anazilipwa na serikali. Hilo ni simple mbona.
Siasa inatawala hadi uchimi achia mbali poropanganda


Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app
 
Hujamwelewa jamaa ww,huyo Laizer ana shopping mall maeneo ya sakina utamwita maskini?
Kuwa na Shopping Mall hata kama anamiliki ndege hakumfanyi kuwa mchimbaji mkubwa. Inategemea ame invest kiasi gani kwenye hiyo migodi. Ambayo itaonekana kwenye equipment, number of employees, production, area etc
 
Ni kweli unachosema lakini hofu yangu ni je uhitaji wa Tanzanite kwenye soko ukoje kiasi kwamba kuwepo na over production ya kupelekea deflation ya Tanzanite kiasi hicho? Mimi sidhani kama yanaweza kuwa mangi kiasi hicho mkuu.
sijui uhitaji wa soko ukoje, lakini kwa kila mwezi wanapotangaza kwamba wamepata kilo fulani, dunia ina take note... kumbuka hakuna sehemu yeyote duniani humu mzigo wa kilo 9 na kuendelea wa Tanzanite umewahi kupatikana... thamani yake imekuwa juu kutokana na ugumu wa upatikanaji wake... sasa hawa mabeberu wakisha jua tu inapatikana kirahisi, maana yake ni kuipunguzia bei- more production - less demand - less price... yafaa sawa serikali iweke muongozo wa production na uuzwaji... kumbuka mafuta namna yanavyopanda na kushuka bei- ni principle hiyo hiyo inatumika kupanga bei ya malighafi duniani.. supply , demand and price... na ni principle hii hii inayo determine dola moja kuwa sh 2000 au zaidi au poundi kuwa zaidi ya Tsh 2500...
Deflation ya bei itategemea na sisi tunavyowatangazia huko ulimwenguni kwamba tunayo bwelele na ya kotosha... na hili kwa sasa linafanyika na akina laizer; duniani huko wakijua tu, basi bei lazima itashuka tu ...
 
Biashara ya kufanyia kwenye TV Ni Kiki. Kama ameridhika kuuza kwa serikali kwa bei hiyo, hiyo ni haki yake, ila angeliuza nje angepata pesa nyingi kuliko hizo anazilipwa na serikali. Hilo ni simple mbona.
Dah kwahiyo tukifanya biashara kwenye TV itakuwa ni kiki?

Usalama wa kuuzia serikali ni mkubwa zaidi kuliko huko nje lakini pia hii ndio maana halisi ya uzalendo au mkuu ulikuwa unafurahia Kenya kuwa nchi inayo ongoza kwa kuuza madini ya Tanzanite wakati hawana hiyo Tanzanite?
 
Back
Top Bottom