Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Sahihi kabisa,
Hakuna mkubwa kuliko kanisa
Na itabaki hivyo.
Najua hapa mwanzoni shetani anayetaka kuharibu umoja wa kanisa atawatishia sana Askofu na uongozi mzima wa Dayosisi lakini wasiogope.

Ni heri hao wanaodhani wana watu wengi waende wakafungue makanisa yao na waliache kanisa likiwa safi.
 
Word

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Nimeshangaa sana reasoning capacity ya Mwamakula kumbe ni bure kabisa.
Maneno hayo ukisema mtu kama wew ni poa tuu just assume aseme leo Samia??? So nani kasema na kasemea wapi ndo jambo kubwa inaweza kuwa neno dogo sana lakini likatela mpasuko na shida kubwa sanaa.
 
Dahh ..huyuu baba mpk kitabu chake nilikua nacho but why?
Waache wivu Mimi muislam lakini nampenda mnoo
 
Maneno hayo ukisema mtu kama wew ni poa tuu just assume aseme leo Samia??? So nani kasema na kasemea wapi ndo jambo kubwa inaweza kuwa neno dogo sana lakini likatela mpasuko na shida kubwa sanaa.
Maonyo na mahubiri huwa hayapigwi ngumu.
Yohana aliwaita wasikilizaji ni kizazi cha nyoka.
Hamyajui maandiko mnaleta aiasa uchwarwa

Imeandikwa kuwa neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili. Kanisa lijitafakari kama umefika wakati wanapinga kuonywa
 
Vilio na mjadala vimeibuka mara baada ya kusambaa kwa video ikimuonyesha Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama Eliona Kimaro akiwaaga waumini wake akieleza kuwa amepewa likizo ya siku 60 na uongozi.

Usiku wa jana, Januari 16, 2023 video ikimuonyesha mchungaji huyo akiwaeleza waumini wake kuwa amepewa likizo ya siku 60 baada ya kuitwa katika ofisi ya msaidizi wa askofu na kufanya kikao na mkuu wa jimbo, ilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

"Semina yetu ni ya wiki mbili (Semina ya neno la Mungu), lakini leo niliitwa ofisi ya msaidizi wa askofu, tulikuwa na kikao na Mkuu wa Jimbo la Kaskazini Mchungaji Mwangomola. Nimepewa barua ya likizo ya siku 60 kesho asubuhi atahubiri Mchungaji Anna na ataendelea kuwa Mchungaji wenu,"

“Kwa mujibu wa barua nitarudi Machi 17 (2023) na sitakuja hapa barua inanilekeza kuripoti Makao Makuu ya Dayosisi kwa hiyo mimi ni mchungaji wa Lutheran kwa hiyo nina heshimu kiapo changu cha kichungaji na kuishi katika kiapo na maadili…

“Pia kwa neema ya Mungu kwa sababu hiyo imenilazimu kutii na kwenda kwenye hiyo likizo na baadaye kuripoti kwenye ofisi ya askofu kama nilivyoelekezwa,” anasema Mchungaji Kimaro katika video hiyo.

Mbali ya video hiyo, ipo nyingine iliyosambaa ikiwaonyesha baadhi ya waumini wa usharika huo wakiangua vilio, wakati mchungaji huyo akifanya maombi ndani ya kanisa hilo wakati akiaga.

Mwananchi imefika kanisani hapo na kuwakuta baadhi ya waumini ambao wameeleza kuwa baadaye jioni watakuwa na jambo lao, ambalo walidokeza kuwa ni kutaka arudi kazini.

Akizungumzia suala hilo, mmoja wa waumini katika usharika huo, Friday John's ambaye ni muumini wa kanisa hilo amesema… “hatujajua watu watapokeaje hili. Mafundisho yake yametutoa mbali, watu wengi wamekuwa wakifuatilia na kupokea mafundisho yake.

“Tunataka mchungaji wetu arudi mafundisho yake yametusaidia ukiacha uchungaji amekuwa na roho ya kipekee ya kusaidia watu.”

Muumini mwingine, Enea Mwantika amesema mchungaji huyo ndio kwanza alikuwa ameanza semina ya wiki mbili na kwamba barua hiyo ya likizo imewaumiza.

“Kilio chetu kwa Dayosisi tunamtaka Mchungaji Kimaro arudi Kijitonyama kuna mtu amehusika. Sisi ndio tunayemfahamu mafundisho yake wapi yanatupeleka na ni nini tunachokipata,” amesema Mwantika.

Alipoulizwa na Mwananchi kuhusu suala hilo, Katibu Mkuu wa KKKT, Robert Kitundu alisema lipo chini ya Dayosisi ya Mashariki na Pwani.

“Kanisa la Kiinjili la Kilutheri lina dayosisi nyingi. Kunapokuwa na dayosisi maana yake kunakuwa na Askofu ambaye anamiliki lile eneo. Mimi kama katibu mkuu wa Kanisa labda nimeambiwe au vinginevyo kwa sasa wazungumzaji ni Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ambaye ni (Alex) Malasusa au Katibu wake,” alisema.

Mwananchi lilifika katika ofisi kuu za jimbo hilo, Azania Front ambako lilielezwa kuwa Askofu Malasusa yupo nje ya nchi kikazi.

Katibu wa dayosisi hiyo, Goodluck Nkini pia alikataa kuzungumzia suala hilo akieleza kuwa hayo ni mambo ya kichungaji taaluma ambayo alisema hana.

Mwananchi lilimtafuta msaidizi wa Askofu Chediel Lwiza ambaye anaidaiwa kuwa ndiye aliyefanya kikao na Mchungaji Kimaro na mara baada ya mwandishi wa Mwananchi kujitambulisha, alikata simu.

Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu utaratibu wa kuhamishwa kwa wachungaji katika Kanisa hilo, Askofu mmoja wa KKKT ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe amesema, “Kila dayosisi ina utaratibu wake. Hapo Dar es Salaam nasikia hata wakuu wa majimbo wanahamishwa.”

MWANANCHI
 
Na nyie msilifanye hilo jambo kuwa kuuuubwa. Kama mmeshindwa kugawana vizuri swadaqa za waumini mpige kimya.

Aliondoka martn luther huko rumi na hakuna kilicho haribika
 
Nguvu ya mamba kumayi,nje ya kkkt hana nguvu hata yeye analijua, kuanzisha kanisa sio kazi rahisi kihivyo
Usijidanganye wewe, hakuna kitu rahisi kuanzisha kama kanisa, tena kwa mtu kama Mch Kimaro akiamua akakohoa tu kho, Kanisa tiyar.
Huo ugumu unaosema sijui unamaanisha ni ugumu wa kuliandikisha au wa waumini??!!!
 
Paragraph ya pili wakulaumiwa ni muumini mwenyewe na sio KKKT.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…