Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Achaneni na makanisa ya kitapeli haya, viongozi wanawaza fitina na kulogana tu,kukamua sadaka za waumini
Haya madhehebu ni ushenzi tu

Watu wamekaa wakajianzishia vijitaasisi vya kupiga hela
πŸ˜‚πŸ˜‚
🀣🀣🀣🀣🀣 oya mkuu mbona una moto sana na makanisa! Umetoa ushauri wa kuchoma moyo.
 
Sawa mkuu mshana ni jambo jema kulifahamu hili, basi pia akubali kurekebishwa kama binadamu, haiwezekani yeye akirekebishwa tena kwa siri na watu au wakubwa wake aje hadharani na kuanza kuwasimanga, huo sio utaratibu.
Siku zote binadamu tunarekebishana ila ukionekana wewe ni kiburi na hutaki kusahihishwa pale unapo teleza watu watakuchoka na ikiwezekana watakuweka kando usimamie kile unacho amini wewe.

Tujiulize hili Wakati anatoka kkkt kariakoo anakuja kijitonyama kwa nini watu hawakuandamana? Kariakoo hakua anatoa huduma kama kijitonyama au kariakoo alikua bado mchanga? Aliyoyafanya kariakoo wakati anahamishwa kwa nn haikua ishu, ila imekua ishu alivyo hamishwa hapo kijitonyama! Kuna kitu cha ziada kwenye hili ila watu bado hawajaelewa.
 
Duh!, that is not fair!. Mimi ni Mkatoliki wa St. Peters, ila kukitokea events hapo huwa nahudhuria mara moja moja, nilihudhuria siku ya Mavuno, huo mpunga uliovunwa...!, nilipotoka nje haya mandinga! ya waumini, nadhani kwa KKKT, baada ya usharika wa Azania Front kwa matajiri wa Upanga, na Msasani kwa matajiri wa Osyerbay na Masaki, unafuata Usharika wa Kijitonyama.
Kwenye makanisa yetu haya ya kimasikini, ukijitokeza tuu utajiri na matajiri, shetani naye anajipenyeza hapo hapo kwa wachungaji kondoo wa Bwana kuanza kujiinua kwa jeuri ya pesa!. Nakumbuka ule mgogoro wa Same!.
Mungu awabariki hili limalizike salama.
P
 
1 mother nikusahihishe Kimaro hajapatia umaarufu K/ nyama bali K / koo nimewahi kuongea nae ni mtu anaejiongelea sana but hua yupo sahihi
 
Kabisa mkuu, mali ndio chanzo cha haya yote, pesa pesa pesa ndio inawagawanya
 
1 mother nikusahihishe Kimaro hajapatia umaarufu K/ nyama bali K / koo nimewahi kuongea nae ni mtu anaejiongelea sana but hua yupo sahihi
Sawa mkuu, tumuombee naye ni binadamu kuna kuteleza, nasi tunayo mapungufu hata zaidi yake utakuta, cha msingi ni kujitafakari pale unapo shtuliwa. Tumuombee mema
 
Mwajiri na mwajiriwa ebu acheni kutumika vibaya kesi ya boss na mfanyakazi wake nyie inawahusu nn

Bila ya uyo boss msingemjua mfanyakazi na uyo mfanyakazi mmemjua na mmempenda kupitia boss na rasilimali za boss
 
Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kumtetea huyu jamaa zaidi ya hao makanjanja wake, yeye aondoke aone kama kkkt itayumba au kutoweka. Taasisi ina misingi yake ukienda kinyume na hiyo misingi ujue unajiweka kando.
Miaka ya 2000 mwanzoni nadhani aliondoka mkuu WA dayosisi kabisa yaani kama malasusa hivi. Akaishia kukimbilia marekani watu wakajua ndio imeisha hiyo but siku zikaenda na watu wakasahau
 
Umeongea point muhimu sana kwa wakristo,waumini wameng'ang'ana bring back Kimaro,huyo Kimaro katekwa?Mchungaji amepewa likizo na hilo wanalijua,na Mchungaji anaweza kuhamishwa kwenda kuhudumu popote pale ambapo uongozi utaona anafaa,tukianza haya ya bringback fulani mbona hatutafika,wachungaji wanahamishwa kila siku na wao wanalijua hilo,sioni haja ya kukaa na mabango hebu wasome katiba ya kanisa wajielimishe waache ujinga.
 
Watu tumechangia sana, japo wengi wetu tumeongozwa zaidi na hisia ambazo si lazima ziwe sahihi. Tatizo la migogoro ni kwamba wahusika huwa hawawezi kusema kiini cha mgogoro hadharani kwa misingi ya maadili. Mungu atusamehe tu.
Unataka wasemee ili kujustify nini??? Wakisema utaamini??? Wew jua kakutwa na makosa ya kinidhamu na yeye kakubali kuunywa...kama anahisi ni mkubwa kuliko KKKT akaanzishe kanisa lakee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…