Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Achaneni na makanisa ya kitapeli haya, viongozi wanawaza fitina na kulogana tu,kukamua sadaka za waumini
Haya madhehebu ni ushenzi tu

Watu wamekaa wakajianzishia vijitaasisi vya kupiga hela
😂😂
🤣🤣🤣🤣🤣 oya mkuu mbona una moto sana na makanisa! Umetoa ushauri wa kuchoma moyo.
 
Dr Kimaro na Mchungaji mzuri tu Lakini kubwa, ni Binadamu. Sifa kubwa ya Binadamu ni mapungufu na kijisahau. Hata Musa alipotumwa na MUNGU akapige Mwamba Ili maji matamu yatoke Wana Israel wanywe, alifika akajisahau kuwa alipewa maelekezo ya ni Cha kusema na kufanya akaenda kujitukuza yeye. Matokeo yake hata Nchi ya ahadi aliyokuwa akupeleka watu hakuingia.[emoji817][emoji818]
Sawa mkuu mshana ni jambo jema kulifahamu hili, basi pia akubali kurekebishwa kama binadamu, haiwezekani yeye akirekebishwa tena kwa siri na watu au wakubwa wake aje hadharani na kuanza kuwasimanga, huo sio utaratibu.
Siku zote binadamu tunarekebishana ila ukionekana wewe ni kiburi na hutaki kusahihishwa pale unapo teleza watu watakuchoka na ikiwezekana watakuweka kando usimamie kile unacho amini wewe.

Tujiulize hili Wakati anatoka kkkt kariakoo anakuja kijitonyama kwa nini watu hawakuandamana? Kariakoo hakua anatoa huduma kama kijitonyama au kariakoo alikua bado mchanga? Aliyoyafanya kariakoo wakati anahamishwa kwa nn haikua ishu, ila imekua ishu alivyo hamishwa hapo kijitonyama! Kuna kitu cha ziada kwenye hili ila watu bado hawajaelewa.
 
Kiufupi ni kwamba kulikuwepo na mashtaka kwenye ofisi ya dayosisi kumhusu huyu kimaro, sasa kwenye dayoysisi hakuwepo katibu mkuu wakti huo kwa hiyo wakamtafuta katibu mkuu wa mda ambaye walimteua mchungaji wa kimara, sasa alivyoenda ofisini akakuta kuna mashtaka juu ya rafiki yake kimaro, ikabidi afatilie na kujua chanzo cha mashtaka
Baada ya kujua chanzo akavujisha siri na kumwambia pasta kimaro
Kwa sababy kimaro hana mambo ya kuficha ficha akaja kanisani na kuanza kuporomosha vijembe kwa viongozi wake lakini akajisahau akamtaja mpk aliyepeleka mashtaka kule kwa matamshi yake akisema ni huyo Anna. Na wakati anamsimanga huyo mchungaji alikuwepo mbele, aliyoongea hata mtoto mdogo akimsikiliza atajua kwamba anamsema yule mchungaji na viongozi wa dayosisi. Kimaro inabidi tu akubali kiburi kinamsumbua na kujiona yuko juu ya wengine sababu ya umaarufu alioupata baada ya kufika hapo kijitonyama.
Duh!, that is not fair!. Mimi ni Mkatoliki wa St. Peters, ila kukitokea events hapo huwa nahudhuria mara moja moja, nilihudhuria siku ya Mavuno, huo mpunga uliovunwa...!, nilipotoka nje haya mandinga! ya waumini, nadhani kwa KKKT, baada ya usharika wa Azania Front kwa matajiri wa Upanga, na Msasani kwa matajiri wa Osyerbay na Masaki, unafuata Usharika wa Kijitonyama.
Kwenye makanisa yetu haya ya kimasikini, ukijitokeza tuu utajiri na matajiri, shetani naye anajipenyeza hapo hapo kwa wachungaji kondoo wa Bwana kuanza kujiinua kwa jeuri ya pesa!. Nakumbuka ule mgogoro wa Same!.
Mungu awabariki hili limalizike salama.
P
 
Kiufupi ni kwamba kulikuwepo na mashtaka kwenye ofisi ya dayosisi kumhusu huyu kimaro, sasa kwenye dayoysisi hakuwepo katibu mkuu wakti huo kwa hiyo wakamtafuta katibu mkuu wa mda ambaye walimteua mchungaji wa kimara, sasa alivyoenda ofisini akakuta kuna mashtaka juu ya rafiki yake kimaro, ikabidi afatilie na kujua chanzo cha mashtaka
Baada ya kujua chanzo akavujisha siri na kumwambia pasta kimaro
Kwa sababy kimaro hana mambo ya kuficha ficha akaja kanisani na kuanza kuporomosha vijembe kwa viongozi wake lakini akajisahau akamtaja mpk aliyepeleka mashtaka kule kwa matamshi yake akisema ni huyo Anna. Na wakati anamsimanga huyo mchungaji alikuwepo mbele, aliyoongea hata mtoto mdogo akimsikiliza atajua kwamba anamsema yule mchungaji na viongozi wa dayosisi. Kimaro inabidi tu akubali kiburi kinamsumbua na kujiona yuko juu ya wengine sababu ya umaarufu alioupata baada ya kufika hapo kijitonyama.
1 mother nikusahihishe Kimaro hajapatia umaarufu K/ nyama bali K / koo nimewahi kuongea nae ni mtu anaejiongelea sana but hua yupo sahihi
 
Duh!, that is not fair!. Mimi ni Mkatoliki wa St. Peters, ila kukitokea events hapo huwa nahudhuria mara moja moja, nilihudhuria siku ya Mavuno, huo mpunga uliovunwa...!, nilipotoka nje haya mandinga! ya waumini, nadhani kwa KKKT, baada ya usharika wa Azania Front kwa matajiri wa Upanga, na Msasani kwa matajiri wa Osyerbay na Masaki, unafuata Usharika wa Kijitonyama.
Kwenye makanisa yetu haya ya kimasikini, ukijitokeza tuu utajiri na matajiri, shetani naye anajipenyeza hapo hapo kwa wachungaji kondoo wa Bwana kuanza kujiinua kwa jeuri ya pesa!. Nakumbuka ule mgogoro wa Same!.
Mungu awabariki hili limalizike salama.
P
Kabisa mkuu, mali ndio chanzo cha haya yote, pesa pesa pesa ndio inawagawanya
 
1 mother nikusahihishe Kimaro hajapatia umaarufu K/ nyama bali K / koo nimewahi kuongea nae ni mtu anaejiongelea sana but hua yupo sahihi
Sawa mkuu, tumuombee naye ni binadamu kuna kuteleza, nasi tunayo mapungufu hata zaidi yake utakuta, cha msingi ni kujitafakari pale unapo shtuliwa. Tumuombee mema
 
Mwajiri na mwajiriwa ebu acheni kutumika vibaya kesi ya boss na mfanyakazi wake nyie inawahusu nn

Bila ya uyo boss msingemjua mfanyakazi na uyo mfanyakazi mmemjua na mmempenda kupitia boss na rasilimali za boss
 
Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kumtetea huyu jamaa zaidi ya hao makanjanja wake, yeye aondoke aone kama kkkt itayumba au kutoweka. Taasisi ina misingi yake ukienda kinyume na hiyo misingi ujue unajiweka kando.
Miaka ya 2000 mwanzoni nadhani aliondoka mkuu WA dayosisi kabisa yaani kama malasusa hivi. Akaishia kukimbilia marekani watu wakajua ndio imeisha hiyo but siku zikaenda na watu wakasahau
 
Yesu akitumwa arudi leo, atajionea maajabu ya dunia. Wakristo wanatakiwa wawe watu wa hekima na busara sana. Mchungaji Kimaro ni mwanadamu kama Askofu Alex alivyo mwanadamu. Kuna aliekosea kuna aliepatia. Lakini Alex anaoperate kwenye mamlaka. Na hata iweje, mamlaka inapaswa kuheshimiwa.

Hata Mungu alijua umuhimu wa mamlaka akaagiza tuzitii hiyo haina mbadala. Katika familia mume, baba anaweza awe phaller flani lakini lazima heshima na adabu ziwepo maana haibadiliki..yeye ni baba. Mamlaka ina haki kubwa mbele za Mungu. I thought Christians tutakuwa better than this. I thought neno la Mungu lililohubiriwa kanisani hapo litakuwa limekuza watu kiimani kiasi cha kwamba hekima na busara zingekuwa zinafurika kwao.

Lakini matokeo ya leo..nimeona sisi waKristo kumbe bado sana. Yani tunaenda hzo Morning na Evening Glory kuombea shida zetu lakini si kubadilika kifikra na kukua kiimani. Tukirudi kwenye biblia, katika Matendo ya mitume, Paul, Petro walikamatwa na kuwekwa ndani mara ngapi?. Ni lini kanisa lilipanic likaenda kuvunja mlango wa Gereza?? Lini?? Zaidi sana kila wakiwekwa ndani either wao wafungwa ama kanisa liliomba kwa mzigo ili waachiwe. Na si tuliona milango ya gereza ikifunguka, tuliona chains zikidondoka. Ok tumuangalie Dorcas.

Dorcas alikufa ingali wale wajane wakiwa wanataka aendelee kuwa hai maana kawashonea sana kanzu na nguo mbalimbali. Lakini pale Orofani walibaki kulia tu..hakuna hata kuomba. Mpaka Petro akaja akaambiwa juu ya tukio akaenda akawakuta kule juu. Akawatimua nje wote. Petro akapiga magoti akaomba akamaliza akasimama akatamka Tabitha ondoka. Kuna kuomba hapa. Kuna faith hapa. Kuna declaration hapa. Kwenye issue serious kama hizi sio pa kupiga soga na kulia lia mitandaoni. Tunakuwa wakristo tantalila.

Wengne tunalaani mamlaka kana kwamba aliyeketi kwenye hicho kiti ni malaika. Neno linasema mtu wa kwenu akipatikana na mabaya na aombe. Haijasema kulalamika, laumu, chuki itatatua tatizo. Wengne wanampa uchizi mtumishi eti afungue Kanisa..hapo atakuwa amebugi kwa kiasi kikubwa sana.

Obedience ni jambo kubwa sana kwa mtumishi na mkristo yeyote. Ukiwa mtii automatically unakuwa mnyenyekevu. Yesu alijua hili ndo maana alikua mtii..wapi?? Tena kaja kufatwa akawekwe ndani na akatii. Mimi na wewe ingekua ndo Yesu si tungewapeperusha hao mandezi. Umewaponya, umewaombea na unawapenda afu wanakuja kukukamata. Wengne umewaosha na miguu.

Utii ni jambo muhimu sana kwa waKristo. Unajiita mKristo afu hutaki kuiga mfano wa your master...jitafakari upya, who you follow. Wanawake ndo wamenikosha. Nasikia leo hakukuwa na Ev. Glory kkkt kijitonyama. Wanazunguka na mabango bring back our Kimaro. Wengne wameanzisha na magroup kabisa. What are we?? Naona sisi ndo wale waGalatia waliohubiriwa nani katuroga jamani?? Kwaiyo tulikua tunamfata Kimaro..kwaiyo mtumishi akitwaliwa hatutaabudu??? Let us repent and Pray. Ukweli usimame..haki itendeke na mwisho Kanisa liendelee kuisambaza injili. Wisdom ni kipengele kwa wengi wetu. God forgive us![emoji29]
Umeongea point muhimu sana kwa wakristo,waumini wameng'ang'ana bring back Kimaro,huyo Kimaro katekwa?Mchungaji amepewa likizo na hilo wanalijua,na Mchungaji anaweza kuhamishwa kwenda kuhudumu popote pale ambapo uongozi utaona anafaa,tukianza haya ya bringback fulani mbona hatutafika,wachungaji wanahamishwa kila siku na wao wanalijua hilo,sioni haja ya kukaa na mabango hebu wasome katiba ya kanisa wajielimishe waache ujinga.
 
Watu tumechangia sana, japo wengi wetu tumeongozwa zaidi na hisia ambazo si lazima ziwe sahihi. Tatizo la migogoro ni kwamba wahusika huwa hawawezi kusema kiini cha mgogoro hadharani kwa misingi ya maadili. Mungu atusamehe tu.
Unataka wasemee ili kujustify nini??? Wakisema utaamini??? Wew jua kakutwa na makosa ya kinidhamu na yeye kakubali kuunywa...kama anahisi ni mkubwa kuliko KKKT akaanzishe kanisa lakee
 
Back
Top Bottom