Yesu akitumwa arudi leo, atajionea maajabu ya dunia. Wakristo wanatakiwa wawe watu wa hekima na busara sana. Mchungaji Kimaro ni mwanadamu kama Askofu Alex alivyo mwanadamu. Kuna aliekosea kuna aliepatia. Lakini Alex anaoperate kwenye mamlaka. Na hata iweje, mamlaka inapaswa kuheshimiwa.
Hata Mungu alijua umuhimu wa mamlaka akaagiza tuzitii hiyo haina mbadala. Katika familia mume, baba anaweza awe phaller flani lakini lazima heshima na adabu ziwepo maana haibadiliki..yeye ni baba. Mamlaka ina haki kubwa mbele za Mungu. I thought Christians tutakuwa better than this. I thought neno la Mungu lililohubiriwa kanisani hapo litakuwa limekuza watu kiimani kiasi cha kwamba hekima na busara zingekuwa zinafurika kwao.
Lakini matokeo ya leo..nimeona sisi waKristo kumbe bado sana. Yani tunaenda hzo Morning na Evening Glory kuombea shida zetu lakini si kubadilika kifikra na kukua kiimani. Tukirudi kwenye biblia, katika Matendo ya mitume, Paul, Petro walikamatwa na kuwekwa ndani mara ngapi?. Ni lini kanisa lilipanic likaenda kuvunja mlango wa Gereza?? Lini?? Zaidi sana kila wakiwekwa ndani either wao wafungwa ama kanisa liliomba kwa mzigo ili waachiwe. Na si tuliona milango ya gereza ikifunguka, tuliona chains zikidondoka. Ok tumuangalie Dorcas.
Dorcas alikufa ingali wale wajane wakiwa wanataka aendelee kuwa hai maana kawashonea sana kanzu na nguo mbalimbali. Lakini pale Orofani walibaki kulia tu..hakuna hata kuomba. Mpaka Petro akaja akaambiwa juu ya tukio akaenda akawakuta kule juu. Akawatimua nje wote. Petro akapiga magoti akaomba akamaliza akasimama akatamka Tabitha ondoka. Kuna kuomba hapa. Kuna faith hapa. Kuna declaration hapa. Kwenye issue serious kama hizi sio pa kupiga soga na kulia lia mitandaoni. Tunakuwa wakristo tantalila.
Wengne tunalaani mamlaka kana kwamba aliyeketi kwenye hicho kiti ni malaika. Neno linasema mtu wa kwenu akipatikana na mabaya na aombe. Haijasema kulalamika, laumu, chuki itatatua tatizo. Wengne wanampa uchizi mtumishi eti afungue Kanisa..hapo atakuwa amebugi kwa kiasi kikubwa sana.
Obedience ni jambo kubwa sana kwa mtumishi na mkristo yeyote. Ukiwa mtii automatically unakuwa mnyenyekevu. Yesu alijua hili ndo maana alikua mtii..wapi?? Tena kaja kufatwa akawekwe ndani na akatii. Mimi na wewe ingekua ndo Yesu si tungewapeperusha hao mandezi. Umewaponya, umewaombea na unawapenda afu wanakuja kukukamata. Wengne umewaosha na miguu.
Utii ni jambo muhimu sana kwa waKristo. Unajiita mKristo afu hutaki kuiga mfano wa your master...jitafakari upya, who you follow. Wanawake ndo wamenikosha. Nasikia leo hakukuwa na Ev. Glory kkkt kijitonyama. Wanazunguka na mabango bring back our Kimaro. Wengne wameanzisha na magroup kabisa. What are we?? Naona sisi ndo wale waGalatia waliohubiriwa nani katuroga jamani?? Kwaiyo tulikua tunamfata Kimaro..kwaiyo mtumishi akitwaliwa hatutaabudu??? Let us repent and Pray. Ukweli usimame..haki itendeke na mwisho Kanisa liendelee kuisambaza injili. Wisdom ni kipengele kwa wengi wetu. God forgive us!😓