Mchungaji Kimaro: Afrika itakuwa ya kwanza kupona Corona itafuatiwa na Asia na wa mwisho watakuwa Israel (Wazungu)

Mchungaji Kimaro: Afrika itakuwa ya kwanza kupona Corona itafuatiwa na Asia na wa mwisho watakuwa Israel (Wazungu)

Ndugu Habari.
Ni nani alikuambia Adam ndio binadamu wa kwanza? Je c14 inayopima umri wa mifupa inadanganya? Hata nami nilikuwa nabisha mwanzoni.

Ukweli ni kwamba, hii dunia iliumbwa mamilioni ya miaka na ilikuwa na watu na hao wanyama mnaita dinosaurs ambao wameishi miaka milioni kadhaa iliyopita. Ndio katika wakati huo lucifer alipewa mamlaka ila akaasi kwa kuwafanya viumbe walioishi wakengeuke na Mungu alishusha gharika la maji kuwaangamiza dunia yote ikafunikwa.

Biblia tunayosoma inaanzia pale roho wa bwana akiwa juu ya maji na ndio ukaanza uumbaji wa pili ambaye alikuwa Adam. Viumbe wote waliomuasi Mungu walipewa adhabu ya milele pasipo msamaha isipokuwa uzao wa adam sababu Mungu alituumba kwa mfano wake hata Baba yetu Adam alipofukuzwa katika bustani Mungu hakumuangamiza wala hakumlaani bali ililaaniwa ardhi kwa niaba ya Adam ila shetani katika umbo la nyoka alilaaniwa yeye.

Biblia ni muunganiko wa vitabu tofauti kati ya 68-72 sababu kuna biblia ya kawaida na ya kikatoliki ambayo ina vitabu zaidi.
Kuna vitabu ambavyo wakati wanavikusanya kutengeneza biblia waliviacha kwa sababu walizoziweka ama pia vilikuwa havijagunduliwa kwa wakati huo.

Mfano. Biblia yetu ya sasa inatueleza habari kuhusu Enoki kuwa aliishi kwa kutembea na Mungu na wala hakufa bali Mungu alimchukua.

Kuna kitabu cha enoki, ama apocryphal books ambaoo utakuta historia nzima Adam siku ya kwanza toka eden nk, nk
Kwa hiyo binadamu wa kwanza aliishi mamilioni ya miaka ni kweli.

Binadamu wa kwanza si Adam huyo mchungaji nani alimpotosha ya kwamba mwanadamu wa kwanza aliishi Tanzania??
 
Sijui unaweza kutuambia ulikoyatoa haya yote ndugu wakala wa shetani.
Au ni ufahamu wako binafsi?


Kutukana na kusoma maandiko matakatifu kama maandishi ya udaku ndicho mnachojua.

Kuhusu kufufuka kwake, Yesu mwenyewe kisha weka wazi kwa kutoa mfano wa Nabii Yona (the sign of Jonas) kuhusiana na tukio la msalaba.

Yona alikuwa nabii kwa watu wa Ninawi na alitoroka Ninawi baada ya watu wake kumkadhibisha, Mungu hakutaka atoroke hivyo alipokuwa ndani ya mashua iliyosukwasukwa na dhoruba ndipo ikapigwa kura ya kutupa watu majini kunusuru mashua isizame na kura y a kwanza ikamuangukia Yona na ndipo akatoswa baharini na akamezwa na Nyangumi na akaka ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku 3 mchana na usiku, akaka humo akiwa hai (katika hali ya kuzirai), Yesu naye akatoa mfano huo wa Yona kwamba naye baada ya kushushwa msalabani atakaa siku 3 mchana na usiku katika moyo wa nchi (pangoni), sasa utaona Yona aliingia ndani ya tumbo la samaki na akaishi humo kwa siku 3 mchana na usiku naye Yesu akaingia ndani ya moyo wa nchi (pangoni) na akakaa humo kwa siku 3 mchana na usiku na wote Yona na Yesu waliingia sehemu hizo husika wakiwa hai bali katika hali ya kuzimia.

Kwa habari ya Yona soma agano la kale kitabu cha Yona.

Kwa ajili ya huo mfano wa Yona Yesu aliowapa wanafunzi wake soma (Mathayo 12:39) hapa chini:--

Screenshot_20210207-175902.png
 
Hakuna anayebisha kuwa mafua ya Covid 19 hayapo!
Nilijua tu This is... atapata shida kwa johnthebaptist. Wa kwanza ni thinker na wa pili ni talker. Anaahidi jioni kusikiliza mchungaji tena apate mistari ya biblia! Anajua kuongea hajui kufikiri. Hata jinsia yake jf haifahamiki. Sijui ni mama/baba pekupeku. Asione au kusikia neno, tayari uzi. Ananukuu wazungu=israel. Kukimbilia jf na chochote!
Hapa ni mawazo ya haijawa kubwa na haipo, iko chache sana. Waliochanjwa wameleta corona ya ajabuajabu. Sio kama ipo lazima kuna watakaogua. Ipo kwa sababu tu tayari kuna wagonjwa. Hao ndio wanasababisha iwepo. Hakuna mgonjwa nchini hakuna uviko nchini. Baradhuli mmoja alisikika akisema: haijawa kubwa=haipo=iko chache sana!
 
Mchungaji wa KKKT Kijitonyama Dr Kimaro amesema kwa mujibu wa maandiko ya Biblia Mungu alishaitangazia uponyaji wa kwanza Afrika yanapotokea maradhi ya kiulimwengu kama Corona.

Hivyo kwa mujibu wa Biblia Afrika itapona ya kwanza, itafuatiwa na Asia na mwisho watakuwa Israel kwa maana ya waxungu wa Ulaya na Marekani amesema mchungaji.

Mchungaji Kimaro amefanya maombi maalumu ya kuliepusha taifa kutoka janga la Corona na ameahidi Tanzania itakuwa kimbilio la dunia nzima kwani hata sayansi inaitambua Tanzania kama ni nchi na ardhi aliyoishi binadamu wa kwanza katika uso wa dunia.

Source Upendo tv

Nawatakia Dominica yenye baraka!

Badala ya kusikiliza wana sayansi tunasikiliza wafanyabiashara ya dini! Binadamu wote ni sawa mbele ya Mungu hakupanga nani awe bara gani😂😂
 
Adamu ni binadamu wa Kwanza, kabla yake walikuwepo viumbe wengine ambao sio binadamu japo wanafana na binadamu!!!


Hiyo ndiyo shida ya Kukariri tu bila kutafakari.

Adam anayesemwa ndiye mtu wa kwanza kuumbwa duniani aliishi miaka takriban 6,000 iliyopita huko Mesopotamia (Iraq ya kale), fuvu la mtu wa kale (Zinjanthropus Boisei) lililovumbuliwa na Dr Leakey na mkewe Mary huko Oldivai Gorge hapa Tanzania linakadiriwa kuwa na umri wa takriban miaka 1,000,000, na bado yapo mafuvu mengi ya watu wa kale yaliyovumbuliwa sehemu mbalimbali duniani yakiwa na umri wa malaki ya miaka.

Sasa tofautisha kati ya Mtu na Binadamu, Watu wote kabla ya Adamu mfano Zinjanthropus hawa wanaitwa (watu/primitive men) na Watu waliokuja baada ya Adam (Homosapiens) hawa wanaitwa Wana wa adamu (binadamu/human beings), sasa utaona binadamu ni mtu mwenye sifa za Adam, sifa za Adamu ni zipi??, sifa za Adamu ni ustaarabu, yaani Adamu ni mtu wa KWANZA kuwa mstaarabu, Ustaarabu huo aliupata wapi??, aliupata kutoka kwa Mungu, hivyo Adamu anakuwa ni mtu wa kwanza kufundishwa na Mungu ustaarabu na yeye akawa ndiye mteule, mtume, nabii wa kwanza kutumwa na Mungu kwa watu wa zama zake ili awafundishe kumjua na Kumuabudu Mungu, baada ya Adam walifuata wateule au mitume wengi wa Mungu kuwafundisha watu dini ya Mungu lakini Adam bado anakuwa ni mteule wa kwanza wa Mungu katika hii circle yetu naye ndiye mstaarabu wa kwanza hivyo utaona Adamu anakuwa ndiye baba wa ustaarabu na ndiyo maana sisi tunaitwa wana wa Adamu (binadamu) kwa maana hiyo tu na wala sio kwa maana kwamba watu wote tuliopo leo dunia tumezaliwa kimwili na Adamu.
 
Mchungaji wa KKKT Kijitonyama Dr Kimaro amesema kwa mujibu wa maandiko ya Biblia Mungu alishaitangazia uponyaji wa kwanza Afrika yanapotokea maradhi ya kiulimwengu kama Corona.

Hivyo kwa mujibu wa Biblia Afrika itapona ya kwanza, itafuatiwa na Asia na mwisho watakuwa Israel kwa maana ya waxungu wa Ulaya na Marekani amesema mchungaji.

Mchungaji Kimaro amefanya maombi maalumu ya kuliepusha taifa kutoka janga la Corona na ameahidi Tanzania itakuwa kimbilio la dunia nzima kwani hata sayansi inaitambua Tanzania kama ni nchi na ardhi aliyoishi binadamu wa kwanza katika uso wa dunia.

Source Upendo tv

Nawatakia Dominica yenye baraka!
Huyu naye anachemka,matatizo huwezi kutatua kwa maombi pekee,inabidi ufanye kazi,hapo kanisani Kwake lazima Kuna vijana hawana ajira,apige "maombi" wapate ajira.
Corona na magonjwa mengine hayaondoki kwa maombi tu,ni tatizo la kitabibu linatatuliwa ki sayansi.
China hawapigi "maombi"lakini nchi yao ina baraka tele kuriko bongo.
 
Mchungaji wa KKKT Kijitonyama Dr Kimaro amesema kwa mujibu wa maandiko ya Biblia Mungu alishaitangazia uponyaji wa kwanza Afrika yanapotokea maradhi ya kiulimwengu kama Corona.

Hivyo kwa mujibu wa Biblia Afrika itapona ya kwanza, itafuatiwa na Asia na mwisho watakuwa Israel kwa maana ya waxungu wa Ulaya na Marekani amesema mchungaji.

Mchungaji Kimaro amefanya maombi maalumu ya kuliepusha taifa kutoka janga la Corona na ameahidi Tanzania itakuwa kimbilio la dunia nzima kwani hata sayansi inaitambua Tanzania kama ni nchi na ardhi aliyoishi binadamu wa kwanza katika uso wa dunia.

Source Upendo tv

Nawatakia Dominica yenye baraka!
Mpaka huu ugonjwa uishe tutakua tumeshuhudia na kusikia mengi
 
Back
Top Bottom